Black Madonna vilikuwa ni vikundi vya watoto wa shule za msingi waliokuwa wakikutana huko Dodoma Mlimani chini ya kiongozi wao Edward Ndomba nakumbuka ni marehemu na kifo chake kilitokea katika purukaushani za namna hiyo hiyo kwa mtu kuchomwa na mshale kichwani. Hawa watoto walikuwa ni wale wa Halaiki za Chipukizi
Wababe wa Dodoma waliodumu kwa muda mrefu ni km kina Abdul Yusuf (kwa sasa km miaka 3 ni marehemu) huyu ndiye tuliyemuogopa kwani akikuona una Demu au kitu km gari atakufuata umlipe asikufanyie fujo anweza kujilengesha kwenye bumper la gari ukiendesha na kudai umemgonga umlipe la sivyo vagi.
Matajiri wa Enzi hizo walipenda kumuweka baunsa milangoni wakati wa filami za kina Bruce-Lee au SHOLAY huko N.K. na PARADISE
Siku za mwishomwisho alitandikwa na watoto wadogo wa vyuo walokuwa hawamjui km ni Baunsa wa Dodoma
Mwingine ni Liondo naye amefariki mwaka huu, naye alikuwa yumo katika list ya wanaoogopewa au kujua Mission town za nani ataibiwa na hivyo kuwafanya Matajiri wa hapa mjini na wenye mabaa kumpa kazi ha za ubaunsa
daah huyo DAME namkumbuka sana enzi shule ya msingi Mashujaa ya Sinza wakati tupo wadogo tukimwona tu tunamkimbia na alishawahi kula chips na kudai chenji wakati halikuwa hajatoa hela
huyu mshikaji aliolewa ndo kisa cha kupotea kwenye ramani.
nammkumbuka huyu mdau aliwahi kunipiga ngeta miaka hyo pale kitanzini wakati napandisha kwenda mjini akanipora dumu la ulanzi ni kitambo sana
kulikuwa na ka mtindo flani songea miaka ya themanini. Nilikuwa std three tulipohamia songea nikakuta watoto wagomvi shuleni vibaya mno, ugomvi nje nje mkizipiga ukimdunda utasikia naenda kuagizia, hapo anamaanisha anakwenda kumtafuta mtu au kikundi waje wakudunde. Utashangaa mmetoka maeneo ya shule unakutana na wababe wanakusubiri kitakacho endelea hapo ni kichapo hahaaa
Hivi Lintu mdogo wake na Gado wa Daily Nation kafa?
dah unanikumbusha pale songea ttc kulikua na kota mtaa wa chini na mtaa wa juu basi ukionekana mtaa usio wako kichpo chake hko.!uu-siniambie na kwenda kuiba viaz thn unachoma kabumbila..dah zaman raha
hahahhaha kapalampya wengi wamemwelezea huyu mbabe na visa vyake lakini cha kwake kinafurahisha na kuchekesha sana natamani kama ungetuhadithia mengi zaidi.
Ebwana Huyu mchizi R.I.P alikuwa balaa alikuwa ni pande la mtu ukimuona nilazima ukubali mwenyewe nadhani walikuwa na anaasili ya Kiarabu[Handsome fulani vile] alikuwa anaishi Ubungo Kibo alishawahi kuwa Shem wangu, Wadogo zake ni washikaji zangu mpaka leo mmoja anaitwa Salum na Akraby, Jamaa Ubongo mpaka Kibo yote walikuwa wanamtambua Cool 9 kama ngumi jiwe chokoza moto uwone,Nakumbuka siku moja alizinguana na Dada yangu kwny mambo yao ya kimapenzi akamwangaliaaa...huku akisikitika kulikuwa na nguzo ya chuma pembeni kwa hasira aliipiga ngumi moja nzitooo... nikaona kama nyumba inatikisika ilikuwa ni kwa Mzee Kumekucha nyuma ya Msikiti wa Kibo kwa wanaopafahamu mi nilikuwa bado mdogo niliogopa nakutoka mbio nikaona Jamaa kama muaji kwajinsi ile ngumi ilivyotikisa nguzo ya nyumba nilihisi ingetua kwny mwili wa Sister sasa hv angekuwa marehemu,Tupe basi stori zake je unamjua mdogo wake anayeitwa Van Dame wa magomeni?unasema kwao iringa mi najua kwao ni ubungo kwa baba yake na ndo alikokuwa anakaa na nyumba yao hadi leo ipo.kati ya yeye na ayati nani alikuwa mkubwa nasikia alikuwa na dada yake alikuwa anapiga naye? mkatabafeki usituache hewani tupe stori zake bwana,je jina lake la kuzaliwa ni nani mana hilo kool9 ni la kizungu?.