Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kuna chuki imepandikizwa dhidi ya serikali yetu; chuki ambayo inawafanya watu wawe na hamu ya kuona serikali iliyoko madarrakani inaangushwa au kuanguka (collapse). Chuki hii inawafanya baadhi ya watu kufanya kila wawezalo kufichua uozo na uovu mbalimbali serikalini. Ni chuki hii inayowafanya watu hata kuamua kubadili uanachama kutoka chama tawala kwenda vyama vingine. Ni chuki ambayo inaonekana kuzidi kukua na kuongezeka kila siku ijayo.
Swali langu ni NANI HASA (mwenye wajibu wa kwanza kabisa) ANAYESABABISHA AU KUPANDIKIZA CHUKI HII?
a. Waandishi wa habari
b. Vyama vya Upinzani (wanasiasa wa upinzani)
c. Wanaharakati wa kisiasa (political activists)
d. Mitandao ya Kijamii
e. Serikali yenyewe
f. Vyote hapo juu!
Lakini swali la msingi ni jinsi gani mhusika huyo anapandikiza chuki hiyo?
Tukijua ni nani anapandikiza chuki tutatarajia hatua dhidi yake....
Swali langu ni NANI HASA (mwenye wajibu wa kwanza kabisa) ANAYESABABISHA AU KUPANDIKIZA CHUKI HII?
a. Waandishi wa habari
b. Vyama vya Upinzani (wanasiasa wa upinzani)
c. Wanaharakati wa kisiasa (political activists)
d. Mitandao ya Kijamii
e. Serikali yenyewe
f. Vyote hapo juu!
Lakini swali la msingi ni jinsi gani mhusika huyo anapandikiza chuki hiyo?
Tukijua ni nani anapandikiza chuki tutatarajia hatua dhidi yake....