Ni kwamba Watanzania wengi tuna roho mbaya au wivu na husuda tu? Lini tutabadilika?

Nimemkumbuka Ma-samaki wa TRA na tuhuma za kumiliki nyumba sijui sabini na ngapi kumbe uongo tu,mwingine sijui anaingiza milion 7 kwa dakika daah mambo ni
Habari zenu wanabodi.

Kuna jambo niliobserve kwa muda sana na leo nimejikuta natype hapa ili kushare na wenzangu ambao wamewahi kulifikiria hili .

Miaka ya hivi karibuni husasani kipindi hiki cha awamu wa 5 na haswahaswa Sasa hivi kumekuwa na trend za tumbuatumbua na kuhoji watumishi na viongozi wengine hadharani Huku wananchi wakipiga kelele kuonesha either mtumishi huyo au kiongozi husika hafai na kama ilivyotokea leo huko nachingwea mtu alipopewa fursa ya kuongea alisema yeye anachotaka ni mtu kutumbuliwa tu.

Nimekuwa nikipitia post mbalimbali hususani pale mtu anapotumbuliwa au kushtakiwa unakuta wengi wanasema huyo ni mhujumu uchumi etc etc lakini ukija in details unakuta mtu huyo wala sio mbaya na wengi wanaocomment wala hawamjui zaidi ya kumsikia siku hiyo,ila unakuta ndo kwanza wanataka asulubishwe asulubishwe.

Najiuliza hii mob ya wapiga kelele kwenye mikutano na mitandaoni huwa haina ndugu ambao ni watumishi wa umma? Haina jamaa na marafiki huko kwenye utumishi? Kwa nini inahukumu bila ata kujua ukweli uko wapi ? Likimpata mtu ambaye mpiga kelele au watoa hukumu hao wanavinasaba naye will it be the same ?

Hiki kitu nashindwa kuelewa ni notion iliyopandikizwa kuwa kila mtu anayedhalilishwa ni mwizi kweli au ni wivu wetu tu sisi Watanzania? Ni husda au ni chuki tu na watu ambao ata hatuwafahamu muda mwingine?

Kuna muda binafsi huwa najikuta naumia na kushangaa kwa nini tunafika hapa.Naomba mawazo yenu wanabodi kuhusu hili jambo ni nini hiki kimetufanya hivi? Tunafurahia matatizo yanapompata mtu ata kama hatumjui?
Watumishi wa Umma waheshimiwe.Wanasiasa lazima Waheshimu Watumishi wa Umma
 
Kuna mtaalamu mmoja wa Karne ya 15 mfaransa Philippe Duvour alisema kuwa mtu ambaye hufurahia kuona mtu mwenye uwezo akitaabika au muonea Wengine hupata majibu maeneo yafuatayo la kwanza aweza pigika kiafya kwa maradhi mabaya yeye binafsi au wanafamilia,pili Watoto wake kutofanikiwa ,na yeye kutoishi maisha ya furaha .
90% ya wananchi wangekua wamepitia hizo hali unazosema maana tumegeuka taifa la ma-sadist.
 
Zamani ulikua unasikia usimuone vile yule jamaa ni mtumishi yule,siku hizi hata kujitambulisha ni aibu sana kwa kweli.
 
90% ya wananchi wangekua wamepitia hizo hali unazosema maana tumegeuka taifa la ma-sadist.
Wengi wanapitia hizo Hali kafanye utafiti kaangalie mfano mtu maskini anayefurahia mwenye maendeleo kufilisika kaangalie Hali za watoto wake Kama anao
 
Mbona kuna wengine wana madaraka makubwa tu na ni ma-sadist na wana dunda tu fresh kabisa wao na watoto wao.

Wengi wanapitia hizo Hali kafanye utafiti kaangalie mfano mtu maskini anayefurahia mwenye maendeleo kufilisika kaangalie Hali za watoto wake Kama anao
 
Ni kama tu wenye uwezo wanavyofurahia maskini akitaabika ndivyo hivyo hivyo maskini hufurahia mwenye uwezo akipata majanga.
Fikiria,watu wanakaa mahali,kwa sababu ya shibe yao,wanapendekeza mtu akiacha kazi asipewe mafao,kwa sababu hajui kutumia pesa yake!Halafu mtu anayefanya hivi ni msomi wa Chuo kikuu!Kwa nini wasiwachukie?

Mtu anakaa mahali fulani, anafikiri jinsi ya kuweka vikwazo maskini wasisome,ili wabaki wao wachache kwenye mifumo ya ajira nzuri,kwa nini maskini asifurahie unapoanguka chini?

Watu wanakaa mahali fulani,wanaanzisha kodi nyingi hadi mtu anashindwa kufanya biashara,wao kwa sababu tu wameshiba,kwa nini maskini asifurahie kuanguka kwa wanaofanya haya?

Maskini anajikongoja,anapata pesa ya kuagiza gari,anatozwa kodi kubwa kuliko hela aliyonunulia gari,hii kama sio kukomoa mtu ni nini?Wanaokomoa hivyo wamefanikiwa na hawataki watu wengi wawe kama wao.Kwa nini maskini asifurahie ukipata matatizo?

Mtu akiwa navyo,anaanza kutukana waliokosa,kwamba hawana akili,ijapo wanaona jinsi unavyowaibia,unadhani nani anapenda kudharauliwa kuwa hana akili wakati ninyi ndio mumemuwekea mazingira magumu ya kufanikiwa?Kwa nini asifurahie mnapoanguka?
 
Kama unafanya mema yanayowapendeza Binadamu wenzako hata wakifanya fitna huwezi kutumbuliwa.
Wema na Uzuri hujitetea wenyewe. Walioko kwenye nafasi za juu za uwajibikaji wanatakiwa kuwapenda na kuwaheshimu na kushirikiana vyema na walio chini yao.
Usidhani mtu anasema tu bila sababu yoyote ya msingi eti Mimi ninachotaka ni mtu fulani atumbuliwe.
Ni mpumbavu pekee anaweza kufanya hivo.
Ukijimwambafai na wenzako wakipata nafasi ya kujimwambafai wanakutia adabu.
Hakuna mtu aliye timamu anayefurahia mwingine kuumia isivyo halali.
 
Kama unafanya mema yanayowapendeza Binadamu wenzako hata wakifanya fitna huwezi kutumbuliwa.
Wema na Uzuri hujitetea wenyewe. Walioko kwenye nafasi za juu za uwajibikaji wanatakiwa kuwapenda na kuwaheshimu na kushirikiana vyema na walio chini yao.
Usidhani mtu anasema tu bila sababu yoyote ya msingi eti Mimi ninachotaka ni mtu fulani atumbuliwe.
Ni mpumbavu pekee anaweza kufanya hivo.
Ukijimwambafai na wenzako wakipata nafasi ya kujimwambafai wanakutia adabu.
Hakuna mtu aliye timamu anayefurahia mwingine kuumia isivyo halali.
Sasa unakuta mtu anashadadia kwa mtu ambaye haya hamjui
 
Ni kama tu wenye uwezo wanavyofurahia maskini akitaabika ndivyo hivyo hivyo maskini hufurahia mwenye uwezo akipata majanga.
Fikiria,watu wanakaa mahali,kwa sababu ya shibe yao,wanapendekeza mtu akiacha kazi asipewe mafao,kwa sababu hajui kutumia pesa yake!Halafu mtu anayefanya hivi ni msomi wa Chuo kikuu!Kwa nini wasiwachukie?

Mtu anakaa mahali fulani, anafikiri jinsi ya kuweka vikwazo maskini wasisome,ili wabaki wao wachache kwenye mifumo ya ajira nzuri,kwa nini maskini asifurahie unapoanguka chini?

Watu wanakaa mahali fulani,wanaanzisha kodi nyingi hadi mtu anashindwa kufanya biashara,wao kwa sababu tu wameshiba,kwa nini maskini asifurahie kuanguka kwa wanaofanya haya?

Maskini anajikongoja,anapata pesa ya kuagiza gari,anatozwa kodi kubwa kuliko hela aliyonunulia gari,hii kama sio kukomoa mtu ni nini?Wanaokomoa hivyo wamefanikiwa na hawataki watu wengi wawe kama wao.Kwa nini maskini asifurahie ukipata matatizo?

Mtu akiwa navyo,anaanza kutukana waliokosa,kwamba hawana akili,ijapo wanaona jinsi unavyowaibia,unadhani nani anapenda kudharauliwa kuwa hana akili wakati ninyi ndio mumemuwekea mazingira magumu ya kufanikiwa?Kwa nini asifurahie mnapoanguka?

Mkuu Pascal Mayalla nisaidie kuelewa hiki kitu tafadhali
 
Ni hulka ya mwanadamu kuona yule aliyejuu mambo yake yakienda kombo.rejea magazeti yote huuza vzr kwa kuwasema vibaya wale mastaa
Na unajua wanunuzi wakubwa ni wale wananchi wa kawaida.
Kwa haya yanayotokea kwa jiwe usishngae kamati ya roho mbaya ilikua inafanya kazi zake kwa kificho sasa huyu mambo hadharani
 
Zama zile wapigaji walijimwambafy sana,, walikuwa wanatishia watu kuwaweka ndani muda wowote kwa kutumia mkwanja wa kufisadi, walitisha hata kukupiga halafu akulipe,, hawa ndiyo walioanza kujenga chuki na wanannchi,,, sasa anapotokea baunsa ambaye anaweza kuwafiligisa ni lazima hawa walioonewa kwa muda mrefu watafurahia tu, kwani wameshapata tabu sana kwa majigambo na dharau za hao waheshimiwa.


Ushauri ;- unapofanikiwa usiwe mtu wa kuwakoga , kuwadharau au kuwatisha waliofulia,, kwani siku ukianguka utakosa angalau hata wa kukuonea huruma.

Na wanannchi :- "hii tabia ni vema tukaiacha sasa kwasababu pengine tunachochea kutumbuliwa hata kwa ambao hawakustahili adhabu hiyo.
 
Sasa unakuta mtu anashadadia kwa mtu ambaye haya hamjui
Kuna watu uchafu wao ndio unaowafanya wafahamike mfano akina dada wanapenda kutumia njia ya kuweka picha za utupu mitandaoni.
Sasa mtu akifahamika kwa njia hii hatakama hukumfahamu utashadadia tu kuunga mkono wanaomzomea.
Ni sawa pia ikifanyika hivi katika maeneo Mengine.
 
Zama zile wapigaji walijimwambafy sana,, walikuwa wanatishia watu kuwaweka ndani muda wowote kwa kutumia mkwanja wa kufisadi, walitisha hata kukupiga halafu akulipe,, hawa ndiyo walioanza kujenga chuki na wanannchi,,, sasa anapotokea baunsa ambaye anaweza kuwafiligisa ni lazima hawa walioonewa kwa muda mrefu watafurahia tu, kwani wameshapata tabu sana kwa majigambo na dharau za hao waheshimiwa.


Ushauri ;- unapofanikiwa usiwe mtu wa kuwakoga , kuwadharau au kuwatisha waliofulia,, kwani siku ukianguka utakosa angalau hata wa kukuonea huruma.

Na wanannchi :- "hii tabia ni vema tukaiacha sasa kwasababu pengine tunachochea kutumbuliwa hata kwa ambao hawakustahili adhabu hiyo.
Logic mkuu
 
H
Kuna watu uchafu wao ndio unaowafanya wafahamike mfano akina dada wanapenda kutumia njia ya kuweka picha za utupu mitandaoni.
Sasa mtu akifahamika kwa njia hii hatakama hukumfahamu utashadadia tu kuunga mkono wanaomzomea.
Ni sawa pia ikifanyika hivi katika maeneo Mengine.
hahahahahaha
 
Habari zenu wanabodi.

Kuna jambo niliobserve kwa muda sana na leo nimejikuta natype hapa ili kushare na wenzangu ambao wamewahi kulifikiria hili .

Miaka ya hivi karibuni husasani kipindi hiki cha awamu wa 5 na haswahaswa Sasa hivi kumekuwa na trend za tumbuatumbua na kuhoji watumishi na viongozi wengine hadharani Huku wananchi wakipiga kelele kuonesha either mtumishi huyo au kiongozi husika hafai na kama ilivyotokea leo huko nachingwea mtu alipopewa fursa ya kuongea alisema yeye anachotaka ni mtu kutumbuliwa tu.

Nimekuwa nikipitia post mbalimbali hususani pale mtu anapotumbuliwa au kushtakiwa unakuta wengi wanasema huyo ni mhujumu uchumi etc etc lakini ukija in details unakuta mtu huyo wala sio mbaya na wengi wanaocomment wala hawamjui zaidi ya kumsikia siku hiyo,ila unakuta ndo kwanza wanataka asulubishwe asulubishwe.

Najiuliza hii mob ya wapiga kelele kwenye mikutano na mitandaoni huwa haina ndugu ambao ni watumishi wa umma? Haina jamaa na marafiki huko kwenye utumishi? Kwa nini inahukumu bila ata kujua ukweli uko wapi ? Likimpata mtu ambaye mpiga kelele au watoa hukumu hao wanavinasaba naye will it be the same ?

Hiki kitu nashindwa kuelewa ni notion iliyopandikizwa kuwa kila mtu anayedhalilishwa ni mwizi kweli au ni wivu wetu tu sisi Watanzania? Ni husda au ni chuki tu na watu ambao ata hatuwafahamu muda mwingine?

Kuna muda binafsi huwa najikuta naumia na kushangaa kwa nini tunafika hapa.Naomba mawazo yenu wanabodi kuhusu hili jambo ni nini hiki kimetufanya hivi? Tunafurahia matatizo yanapompata mtu ata kama hatumjui?

Sasa kama mtu. Anafurahi ndege ya Tz imekamatwa
Wewe ukifanikiw inakuwaje ?
Roho itampasuka kwa wivu
 
Tungeanza na rais, ambaye ndiye huwasimamisha watendaji hadharani. Nia yake ni nini, na je ni ya dhati? Kuna mtu alikuwa msimamizi wa stendi ya ubungo, hakuwepo kwenye hadhara siku hiyo,bila mkuu wa mkoa kamchongea na rais anaiuliza hadhira nimtumbue ,nisimtumbue, unafikiri walijibu nini? Sasa ni utendaji gani huu wa rais?
 
Nimemkumbuka Ma-samaki wa TRA na tuhuma za kumiliki nyumba sijui sabini na ngapi kumbe uongo tu,mwingine sijui anaingiza milion 7 kwa dakika daah mambo ni mengi.

Wizi mtupu alafu watanzania hilo hawalioni, mtu anaingiza 7mil kwa dakika kwa siku ana 10 billion, kwa mwezi ana 300 billion, huyo amekua TRA? In short ndani ya muda mfupi angekua anafukuzia level za Dangote hiyo hela hata Tanzania hatuna labda kama alikua anaibia dunia nzima kwa mpigo.
 
Wengi wa wanatanzania tumeingia kwenye umasikini na mdidimio wa kiuchumi hivyo ikitokea kuna member mpya anaetaka kujiunga nasi haswa aliekuwa juu kuna ile kufurahi na kujiona hatupo peke yetu kweny hii dhiki na huwa tunafurahishwa kuona kuna mwingine anataka kushushwa na kujiunga nasi.
IN SHORT ROHO ZA MASIKINI NA WALIOKATA TAMAA NDIVYO ZILIVYO NA NDIYO MAANA HATUBARIKIWI NA TUNAZIDI KUOZEA KWENYE DHIKI.
Napenda sana huo mtazamo wako, wengi watz watabaki kuwa masikini sababu kaa unafurahia janga la binadamu mwenza je wewe ni binadamu au ni myama?masikini anaona raha sana pale mtu wingine anajiunga na hilo kundi la umasikini, nimeona jiwe kamufuta kazi mkuu takukuru pale mkoa wa mtwara, na ni sababu tu hakuwa pale kwa mkutano, je magufuli alijiuliza kaa huyu mkubwa wa takukuru ako mgojwa, ako likizo au mtoto au mke wake kalazwa hosipitalini? na uliona vile watu walivyosangilia ni kaa wao ndio watapewa hicho cheo,TZ KUNA UJINGA WA AJABU
 
Back
Top Bottom