Mwanamke hapigwi bwana,ila kwa kipande cha khanga,Mwanamme nae hapigwi.Nimewahi kufanya uchunguzi kwa binadamu, wanyama na ndege kuhusu mahusiano ya jinsia ya kike na kiume na sikuwahi kona wanyama wala ndege wa kiume akipigana na mwenzake wa jinsia ya kike, hilo halina ubishi. Lakini nikabaini kwamba ni binadamu tu wa kiume yaani wanaume hupiga wanawake tofauti na wanyam na ndege. Kwa kweli sikupata jibu.
Je, wanaume (binadamu) ni katili ?
Wanawake ni wachokozi ?
Je, binadamu kakosa busara hata anazidiwa na wanyama na ndege ?
Je, kuna jinsia imesahau wajibu wake wa jinsia yake ?
Je, sababu ni nini ?
Naomba wana JF mnisaidie.
Mzee Kibiongo - Nisaidieni nisije nikazidi kupinda kwa kibiongo changu.
Hata siku moja isijetokea wapenzi mkapigana,ni kosa kubwa sana.
WANAUME; yapo maneno ambayo ukimwambia mwanamke,adhabu yake ni ubwa zaidi ya fimbo 100 na kwa kweli hata sahau na harudii tena kosa.
WANAWAKE; mwanaume akikuudhi sana sana,usimpige wala kumkoromea we anza kulia taratiiiiiiiiibu kwa uchungu mkubwa.Hiyo inafanya kazi sana kuliko uwe mkali au umpige mmeo si unajua tena huruma zetu sisi wanaume? nitakuonea huruma na kukuomba radhi kiutu uzima baada ya mechi mambo yameisha sirudii tena,wanaume wachache wanaovumilia kuona wake/wapenzi wao wakilia