waje na hapa JF
mwanasheria mkuu wa Zanzibar said:Tatizo la siku za mwanzo kabisa la Muungano lilijitokeza mwaka 1965 wakati jambo jipya la Muungano lilipoongezwa katika orodha ya mambo ya Muungano; inaonyesha bila ya makubaliano baina ya Serikali hizi mbili. Mawasiliano yaliopo katika kumbukumbu baina ya Waziri wa Fedha wa Zanzibar na Waziri wa Fedha wa Serikali ya Muungano yanaonyesha kuwa mawazo ya Serikali ya Zanzibar katika uundaji wa Benki Kuu hayakusikilizwa. Baada ya muelekeo wa kuwa na Shirikisho la Afrika Mashariki kufifia, nchi za Afrika Mashariki zikitanguliwa na Uganda zilichukua hatua za kuanzisha Benki Kuu zao hata kabla ya kuivunja rasmi Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki. Katika hali hiyo ndipo Serikali ya Muungano ilipochukua hatua za haraka za kuanzisha Benki Kuu ya Tanzania bila ya maafikiano rasmi na Zanzibar na hivyo kupelekea Zanzibar kukosa haki zake katika Bodi ya Sarafu na ndani ya Benki Kuu ya Tanzania.
Kutokana na hatua hiyo Rais wa Zanzibar Sheikh Abeid Amani Karumed aliunda Kamati ya watu 12 ikiongozwa na mtaalamu wa Masuala ya Benki Bw. E. Ebert ili kuishauri Serikali juu ya kuanzisha Benki ya Serikali ya Zanzibar. Kamati hiyo iliwasilisha ripoti yake mwishoni wa mwaka 1965. Ripoti hiyo pamoja na mambo mengine ilipendekeza kuwa Benki hiyo iwe ndio Benki ya Serikali na itumike kusimamia hesabu za (Accounts) Serikali. Kamati ilipendekeza hadi ifikapo July, 1966 accounts zote za Serikali ziwe zimehamishiwa Benki hiyo. Hapo ndipo ilipoanzishwa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) ambayo iliendelea kuwa ndio Benki ya SMZ hadi mwaka 2001 wakati Benki Kuu ya Tanzania ilipoanza rasmi kuwa Benki inayotumiwa na Serikali ya Zanzibar. Hivyo pamoja na kuwepo Benki Kuu kama chombo cha Muungano lakini kuanzia awamu ya kwanza hadi ya Tano za Serikali ya Zanzibar, haikutumia Benki hiyo. Serikali ya Muungano ilikuwa siku zote ikililalamikia jambo hilo.
mwanasheria mkuu wa Zanzibar said:Kodi ya Mapato, Mikopo ya nje na Biashara za Nje bado yamefanywa ni mambo ya Muungano. Kodi ya Mapato ambayo ni nyenzo kuu ya uchumi wa visiwa ambao ni Service oriented badala ya kuwa resource based kama ilivyo kwa Bara, bado ni jambo la Muungano kisera, ingawa mapato halisi yanatumika Zanzibar.
Hivi kweli Werema alikuwa Jaji? Je kuna watu walionyongwa kutokana na hukumu iliyotolewa na Werema? Kama kuna mtu ana ndugu aliyenyongwa kutokana na hukumu ya huyu jamaa, basi ajue kuwa huenda alimpoteza ndugu yake huyo bila sababu yoyote bali ukilaza wa Werema.
Sakata la kuundwa kwa Katiba mpya limeanza kuchukua sura mpya, baada ya Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi ya Elimu ya Juu, Sayansi, Teknolojia, Habari na Utafiti nchini (RAAWU)....
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
Hivi kweli Werema alikuwa Jaji? Je kuna watu walionyongwa kutokana na hukumu iliyotolewa na Werema? Kama kuna mtu ana ndugu aliyenyongwa kutokana na hukumu ya huyu jamaa, basi ajue kuwa huenda alimpoteza ndugu yake huyo bila sababu yoyote bali ukilaza wa Werema.