The Monk
Platinum Member
- Oct 12, 2012
- 19,254
- 42,873
Tunapoelekea mwisho wa mwaka, nikaona nijaribu kuleta kwenu hii hoja ambayo imekua ikiibuka Mara nyingi hasa Kwa wanandoa wanaume.
Hapa naongelea Mme ameoa, anaamua kuchepuka anasema hawezifanya hicho kitendo na mwanamke mwingine kwenye Kitanda anacholalia na Mke wake.
Sasa kama unamheshimu mkeo kiasi Cha kuthamini Kitanda unacholalia nae, mwili wako si ndio unatamani zaidi ya Kitanda? Kwanini umpe mwili wako mchepuko na kuhangaika kufanyia eneo lingine kisa heshima Kwa Mke wako?
Ukishaamua kusaliti, hua hapo hakuna Tena suala la heshima haijalishi utafanyia kwenye mti, vichakani, hoteli ya nyota 5 au ufukweni. Tuache kujifariji.
Niwatakie heri, afya njema na mafanikio wanajukwaa wote wa JF tunapoingia mwaka 2023.
Hapa naongelea Mme ameoa, anaamua kuchepuka anasema hawezifanya hicho kitendo na mwanamke mwingine kwenye Kitanda anacholalia na Mke wake.
Sasa kama unamheshimu mkeo kiasi Cha kuthamini Kitanda unacholalia nae, mwili wako si ndio unatamani zaidi ya Kitanda? Kwanini umpe mwili wako mchepuko na kuhangaika kufanyia eneo lingine kisa heshima Kwa Mke wako?
Ukishaamua kusaliti, hua hapo hakuna Tena suala la heshima haijalishi utafanyia kwenye mti, vichakani, hoteli ya nyota 5 au ufukweni. Tuache kujifariji.
Niwatakie heri, afya njema na mafanikio wanajukwaa wote wa JF tunapoingia mwaka 2023.