Ni kheri arudi urais Benjamin Mkapa kuliko uongozi wa Jakaya Kikwete: What does that tell us?

Kwa hakika inatia kichefuchefu sana ,ukweli waacheni watanzania watapata kiongozi wao wakati ukifika.
 
Huwezi kumlinganisha Ben na JeyKei hata siku moja. Ben alikuwa kiongozi mwenye mipango yake na utekelezaji wake. Bwana Jey yeye anasikiliza vijiwe na vyombo vya habari then anafikiri anaweza kutekeleza matakwa yake. Siioni vision yake, hana contribution yeyote ya ridhaa ya kuweka habari hewani. Mambo mengi yamefumuka na yataendelea kufumuka kutokana na kitu inaitwa Wanamtandao ambao yeye ndo alikuwa kiongozi wao, kupinduana na kumwagana ndo kitu kinachotufanya tuyapate yote haya na bado yanakuja mengi.
 
Hili la eti JK kaachia mambo yawe hadharani bado linanitatiza bado siamini kwamba ni mkakati alioupanga kwa makini manake kama ni hivyo hao mainjinia wa huo mkakati wana ulakini chukulia mfano suala la IPTL,baadhi ya mikataba tata ya madini au tuhuma zinazomkabili Porf.Mahalu hizi zinamgusa kwa namna moja au nyingine JK kwani zilitokea kipindi yeye akiwa ndo kiranja kwenye hizo wizara, ndo maana bado naamini yote yametokea bila ya wao kutegemea na bila ya kujua jinsi ya kujilinda, na hii ikichangawia zaidi na staili ya JK ya 'divide and rule' kwa kukumbatia zaidi watendaji waliomsapoti wakati wa uchaguzi wa ndani ya CCM 2005 kwahiyo wale waliosapoti wagombea wengine waliwekwa kando 'labda wakaamua' liwalo na liwe.
Lazima tukubali zama zinabadilika inawezekana enzi za Mkapa watu walikuwa na cha kupoteza hivyo wakaamua kukaa kimya na/au kuugulia kimyakimya tofauti na sasa ambapo tunakaribia kufika point of no return na wananchi hawana chachote cha kuhofia.,Kama alivyosema Jasusi Mkapa atalaumiwa daima kwa kukubali kuachia nchi kwa Mtandao wa visa na kujilimbikizia mali wakati anageweza kutoa chaguo sahihi zaidi..
 
Wakuu nadhani tumeanza kusahau kidogo, mwishoni mwa enzi za Mwinyi Tanzania ilikuwa inaelekea kuwa a failed state (yes I mean it) failed state si lazima uwepo wa vita. Nchi somehow ilikuwa haitawaliki, kila mtu uliweza kufanya upendavyo ili mradi una hela tu, you could steal,maim, even kill tena hadharani!!!!, Government was broke, discredited and confused. Ndiyo haswaa mwanzo wa ngonjera ya ukosefu wa madawati, walimu kukosa mishahara, ukosefu wa uwajibikaji, misheni town etc. Migomo ya wafanyakazi, wanafunzi.

The main thing ambayo Mkapa atakumbukwa Daima ni kurudisha credibility ya serikali, if you don't know what this is, just look at Somalia, Congo na hata Pakistan (Tofauti kuu ambayo tungekuwa nayo na hao labda ni ukosefu wa vita). Ni wakati huu wa Mkapa serikali ilipoonekana kumbe ikiamua inaweza, makusanyo ya kodi yaliongezeka kwa asilimia karibu elfu moja (1000%) kutoka Bilioni 25 kwa mwezi mpaka bilioni 200 - 250. This is the time ada ya shule ya msingi ikafutwa, migomo vyuoni ikapungua sana , Ajira ya serikali ikarudishwa heshima, inflation ikawa truly contained na si hii ya sasa ya data za kupika. (Kwa mwananchi wa kawaida this is the centre of all the troubles) For the first time miradi mikubwa kama ya barabara ikaanza kufanyika kwa hela zetu wenyewe. It is in Mkapa's term Tanzania ikaondoka kwenye the best 5 if not 2 poorest countries in the world. Tukaona madirisha na milango hadi ceiling boards zikirudi shule za msingi mambo yaliyoanza kuwa historia. (Kwa faida ya wengine shule nyingi tu enzi za Nyerere zilikuwa mpaka na vyoo vya "kuflash"). Kifupi serikali ikawa na hela na ndiyo sasa gateway ya ufisadi mkubwa mkubwa ikajitokeza. Who would steal the monies we didn't have in Mwinyi and Nyerere's era??????? Another big plus ya wakati wa Mkapa ni uongozi, serikali ilieleweka inasimamia nini na what was the vision. The big issue with Mkapa though na hayo aliyoyafanya ni "at what price??"

Tatizo naloliona kwa JK ni kama vile amepewa uraisi kwa kushtukizwa whilst he's on record kujiandaa for more than 10 yrs. Suala la mambo kuwa exposed au the so called uhuru wa vyombo vya habari ni debatable! ni sawa na kusema Obama ana-interact sana na wananchi kwa njia za kisasa kama twiter, emails etc. wakati Clinton alituma email moja tu in the white house. in 8 years. JK kwanza amemaliza hela zote alizoacha Mkapa, kwa mara ya kwanza tunashuhudia serikali ikikopa toka benki za biashara, Ask any govt employee (wale wa kawaida) entitlements zao ndiyo kama zimeyoyoma hivyo. Ametuletea shule za kata, barabara haziishi, Giza, ufisadi ndiyo haswaa umepamba moto, Uongozi sifuri, ule ujanja ujanja wa enzi za mwinyi ulioanza kuondoka umerudi kwa kasi ya ajabu na maradufu. Nepotism at it's best, ofcourse huwezi kukwepa hili maadili yakikosekana na jamii ikiwa corrupt.

Kwa maoni yangu there's pieces of Mkapa's work unaweza kuziweka kwenye uongozi wa JK na mambo yakaenda kiasi flanni lakini I doubt if there is any piece of JK (The good side) unayoweza kwenda kuichanganyisha na utawala wa Mkapa to get the country going.

Hitimisho langu though hao wote Mkapa na JK wameacha makovu (JK anaendelea) yatakayochukua miaka mingi sana kuwa properly healed.
 
Hii misingi yote mibovu ya kiutawala na ya kiutendaji ni matunda ya Benjamini Mkapa, ambayo kamkabidhi JK.
JK na Mkapa wote ni marais wabovu walipata kutokea hapa Tanzania tumeona kwenye vipindi vyao mambo mengi ya UFISADI na uporaji wa mali za umma yamefanyika sana wakati wa vipindi vyao.
Tofauti ya Mkapa na Jk, ni moja tu, Mkapa ni mkali na Jk ni mpole.
 
Ije BALAA yeyote (kiongozi) Tanzania lakini sio SLAA.....................This dude is an IMMORAL con artist !
 
Hii misingi yote mibovu ya kiutawala na ya kiutendaji ni matunda ya Benjamini Mkapa, ambayo kamkabidhi JK.<br />
JK na Mkapa wote ni marais wabovu walipata kutokea hapa Tanzania tumeona kwenye vipindi vyao mambo mengi ya UFISADI na uporaji wa mali za umma yamefanyika sana wakati wa vipindi vyao.<br />
Tofauti ya Mkapa na Jk, ni moja tu, Mkapa ni mkali na Jk ni mpole.
<br />
<br />
bila hiana,zengwe,mtima nyongo wala kumungunya maneno MKAPA ALIKWENDA IKULU AKIJUA KAZ ANAYOKWENDA KUIFANYA,pls ana mapungufu kama binadam lakn maisha yalkwenda vema hasa wananch mackini,hafanan na jk hata kidogo
 
Wote wanamaovu yao, lakini bora Mkapa kuliko JK. JK IS DA WORSE P.R IN TZ. Akishirikiana na hao mafisadi wengine ambao ni marafiki zake.
 
Kweli Mkapa alikwenda ikulu akijua kazi anayokwenda kuifanya.
Ya kuuza Migodi yetu kwa wazungu na kuuziana nyumba za serikali kwa bei ya kutupa, wewe unaonekana wazee wako walikuwa kwenye serikali ya Mkapa ndio maana unasifia eti maisha yalikuwa mazuri labda kwenu
 
My take , awamu ya nne inamapungufu yafuatayo
  1. Uteuzi wa watu haujafuata uwezo. Zaidi imefuata kujuana. Hii ni across the board.
  2. Reaction towards kero/matatizo hakuna. km Scandal ya EPA, Richmond, . Panakuwa na mild actions zinzochukuliwa hasa baada ya kelele kuwa nyingi.
  3. Ubinafsi among watendaji umezidi.
  4. Priorities hazijawa defined. Fate will decide course of action/decisions.
  5. Collective responsibility hakuna. Wengine wako juu.
  6. Kutoa maamuzii inakuwa shida. Karibu kila kitu ni kwa kuunda tume.
 
duh! mjadala mkubwa lakini tabu inabaki kwetu raia unajua athali za uongozi atuzioni sisi hapa mijini heli ya enzi za mwinyi ingawa alikuwa remoted na kambarage lkn kulikuwa na viwanda,ukulima,mashirika yaliyotoa fulsa ya ajira kwa waliokosa elimu. Sasa dah! Kwa hawa BM na JK maskini labda imekuwa kama awajui majukumu yao hivi mnajua unaweza ukawa presdent lkn huna presdency yan ukabaki rais kwa kuteua na kulindwa pamoja na kuishi ikulu maisha yamekuwa ya kikimbizi ndani ya taifa lenye kujiamria mambo yake lenyewe kila sekta ovyo tu kweli tuwaonee huruma ndugu zetu kule vjjni hawana hata matumaini. Mf. Umevunjika mfupa opareshen MOI si chini ya mil. 2 atujui hata kodi zetu walizosomeshewa madaktar na wauguz tunachanga kwa manufaa gani au ili iweje inauma sana.
 
Jasusi ... unazungumzia la Jairo hili la juzi... angalia ungozi mzima wa JK... mangapi yamekua exposed?? matatizo mangapi saizi yamekua as a result of that exposure?? Na umejiuliza hayo yoote yalokua exposed ni since when yalianza na mizizi yake iko tangled vipi?? JK yupo kwenye politics like forever - swali napenda nijue ni kwamba alijua yoote hayo, alifanya hivo kwa malengo gani kama hawezi ya solve??
Tuseme ukweli, hata wakati wa Mkapa mambo mengi yalikuwa exposed, particularly first term. Maana nakumbuka issue za akina Mbilinyi, idd Simba, Hasi Kitine and several others ambao walikuwa wakifanya ufisadi tu Mkapa hawaangalii usoni anawatimua instantly. Mkapa alikuja tu kuchanganyikiwa miaka miwili ya mwisho, but the guy real did his best. Awamu ya kwanza na ya pili mwanzoni hakufumbia macho upuuzi na alikuwa anajitahidi kuweka kila kitu wazi. Na alichokuwa anakifanya kila mtu alikuwa anaweza kukiona na kuappreciate. Ni wakati wa Mkapa ambapo serikali ilikuwa inaweza kufanya mambo mengi kwa bajeti yake yenyewe. Hata Kikwete alipoingia madarakani alikiri kwamba alikuta fedha kibao za kigeni na za ndani. Leo zimepukutika zote na kilichofanyika cha maana hakipo.

Tujiulize zimekwenda wapi? Nawaambieni Kikwete naye atakapotoka madarakani halafu akaja kiongozi mwenye kutaka sifa kama yeye, basi tutasikia ufisadi mkubwa mno na wa kutisha. Maana yeye Kikwete aliamua kuexpose mambo ya mwenzie ili kujiongezea sifa kwa wananchi. Sasa na Rais anayefuata akiwa kama yeye naamini hali yake itakuwa ni mbaya kuliko ya Mkapa. Hamjiulizi ni kwa vipi makusanyo ya mapato yameongezeka, halafu hali ya uchumi wa serikali na wa wananchi inazidi kuwa ngumu? Hayo makusanyo yaliyoongezeka yanafanya nini ilihali bajeti yetu bado inategemea misaada kwa kiasi kikubwa? Kuna shida ndugu zangu, nyie jifarijini tu kuhusu Kikwete, but kusema ukweli Kikwete ni fisadi mkubwa sana tu, ni vile kwamba kutokana na nafasi yake hakuna anayeweza kuhoji, same as it was to Mkapa.
 
Mmmh mimi nadhani hatujawahi kupata RAHISI kama huyu......kwa urefu, rangi, tabasamu na kicheko,urembo, mhudhuria misibanI na mpiga picha na wananchi, zaidi ya yote mkimya kupita kiasi kwenye burning issues....

mix with yours
 
AshaDii,
Nadhani hoja nzima ilikuwa fikra za watu wanaosema ni kheri ya Mkapa angerudi kuliko uongozi wa JK kuwa msingi wa hoja yako kuwashangaa watu hawa lakini sikutegemea kwamba hata wewe unaona bora ya JK ktk kipimo cha viongozi wawili wabovu. Binafsi siku zote humpima kiongozi sio kwa jambo moja na wala simpimi kiongozi kwa kufanikisha sheria zisiyokuja Uchumi wa nchi kwani hakuna sifa kama hiyo ktk uongozi bora kama huboreshi maisha ya wananchi..

Niliwahi kusema kwa wanaomsifia Mkapa kwamba aliweza piga hatua tatu mbele muhimu za ufanisi ktk uchumi wa Tanzania lakini akatudisha nyuma hatua saba hivyo kwa ujumla wake Mkapa aliturudisha nyuma hatua nne sawa na JK ambaye aliukuta uchumi upo hatua nne nyuma katurudisha hatua nyingine mbili zaidi na kufika hatua sita nyuma. hatua mbili nyuma hazina unafuu wowote kwa sababu gari lililokwama huwezi jaribu kuliendesha ktk tope bila kutafuta mbinu za kulikwamua kwanza.


Mkandara&#8230; sioni sababu ya kusifia lolote hali they are both responsible katika situation tuliopo in one way or another&#8230;. Unamsifia Mkapa saizi kwa results za vigezo alivotumia kuweza imarisha uongozi wake&#8230; na kuendesha inchi kana kwamba ni ya watu wa CCM peke yake&#8230; Tawala zoote zipo ni sawa &#8211; where as tackling na decision making ndo tofauti thus the end results za hizo actions tofauti&#8230;.

Mkapa is very intelligent&#8230; Pro-active and the most calculated Leader in the recent three decades.. He has absoulute decisions, Hivo issue yoyote ambayo ilikua ni dhahiri yaweza stress utawala wake ulikua inazimwa at speed! Issues zoote was all about sweeping under the carpet &#8211; Inshort alikua achekei kitu chochote ambacho ni dhahiri kua itakua kikwazo kwake; The man never entertained the media.. a tool of communication of which is the most reliable kwa Mtanzania wa kawaida kupata habari kama ilivo sasa&#8230;..

Kikwete&#8230;. Genuinely simuelewi&#8230; To me a complex personality (as much as most Tanzanians wesha conclude what he is all about&#8230; He is soooo Robust; at a time when inchi ipo katika hali mbaya mno (leaving the leadership period ya Mwalimu aside&#8230;..) Thus najiuliza WHY?? Hizo guts anatoa wapi?? And what does that say about him as a leader and as a person?? (najua for a fact kupata jibu saizi sio rahisi &#8211; but hilo litaonekana with time, for saizi mainly ni assumptions na prejudgements&#8230;.) Siwezi sema yooote yalokua exposed wakati wa uraisi wake ni coincidence&#8230;. Katika politics hakuna such things as coincidences&#8230;. (thou just my IMO)

Hivo basi hapo in blue is the only thing namsifu Mkapa&#8230; Uchumi unaweza ukawa haukuwa mzuri but ulikua Stable&#8230; WHERE AS Jakaya namsifu kwa kulegeza kamba as much as katuweka pabaya Mno!! Hali kweli ni mbaya jamani... tokeni huko mjini nendeni huko vijijini.... Dah!

Kwa nini wananchi wanasikia uchungu zaidi leo wakati wa JK kuliko wakati wa Mkapa au Miwnyi?..ni kwa sababu tulikuwa ktk kuporomoka tayari (hatua nne nyuma) hivyo ongezeko lolote la kuporomoka chini linakuwa na machungu zaidi kuliko tungekuwa ktk hali nzuri ya kiuchumi na tukashuka kama nchi za Ulaya leo hii.

Sasa sababu hasa ya wananchi kushindwa kufikia maamuzi mazuri na ya busara ktk mapendekezo kama haya ni kwa sababu hatujawahi kuona maendeleo ya kiuchumi zaidi ya miaka ya mwanzo ya Nyerere between 1972 na 1978 kabla ya vita ya Uganda ambapo GDP yetu ilikuwa ikipanda kwa zaidi ya asilimia 6 na hadi 10 kwa mara ya kwanza ktk historia ya nchi yetu. Lakini kwa bahati mbaya ni ktk miaka ya 80's ndio watu wengi tunayo kumbukumbu yake kwa sababu tulishuka hadi kuanza kula mtaji na kifo cha Ujamaa ndio kilitumaliza kabisa.

Ni vigumu sana kumpata mtu leo hii anayekumbuka Tanzania ya mwalimu Nyerere ambayo ilikuwa nchi ya pili duniani kwa kuproduce Chai, halafu ukitazama pamba, kahawa, korosho na katani tukiwa ktk best 10 bila kusahau Zanzibar ikiongoza duniani kwa kuzalisha Karafuu na spices nyinginezo. Leo hii ni historia ktk vitabu, hatupo hata katika picha ya wazalishaji pamoja na kuwa tumeingia ktk Ubepari - Pamoja na kwamba Ardhi bado tunayo na nguvukazi imeongezeka maradufu.. hatuna cha kujivuania zaidi ya kuhesabu madeni na mchango wa misaada ktk GDP yetu wakati hakuna mfumo bora wa kutoza na ukusanyaji kodi..

Bado mahotel yanabadilishana mikono kwa majina kila baada ya miaka mitano na Jk hawezi kuwalazimisha wenye Hotels wasiuze kwa sababu hiyo ni biashara ya mtu sio ya serikali. Biashara ikishuka hakuna sheria ya kumfunga mtu kulazimishwa abakie na biashara isiyolipa, ingawa tunajua wanatengeza faida kubwa. Hayo Madini, Wanyama pori, Viwanda na uwekezaji woote ulotanguliwa na mikataba/ubinafsishaji wa Mwinyi na Mkapa ulikuwa Mbaya sana kiasi kwamba JK hawezi kurekebisha kitu unless yeye mwenyewe achukue maamuzi magumu..Nakumbuka Jk alisema mashirika ya madini yataanza kulipa ushuru wa mapato mwaka 2010 lakini ktk bajeti sikusikia hilo likizungumziwa na limeongeza pato la taifa kwa kiasi gani..

Ni yapi hayo maamuzi magumu.. nadhani hapa ndipo napoweza kumpongeza Lowassa kwa kauli yake ingawa sina hakika kama alikuwa na maana sawa na yangu. Maamuzi magumu ni kuvunja mikataba yote mibovu, mikataba iisiyokuwa na faida kwa nchi yetu zaidi ya kuuza utu wetu kwa fedha. Kuchukua maamuzi kama ya rais Chavez wa Venezuela kwa sababu mikataba yote iliyotanguliwa na Mwinyi au Mkapa imeifunga serikali ktk gereza, hali ambayo sii rahisi kujikwamua na labda niseme kwamba serikali imekamatwa pabaya kama shirika la Tanesco ktk sekta zote za Uzalishaji...Ubinafsishaji umekuwa Ukoloni mamboleo tunalipa madeni yasiyokwisha, kuwadhalilisha wananchi zaidi badala ya kuwajenga.

Na maadam JK ameshindwa kusimama imara na kusoma alama za nyakati na kuchukua maamuzi magumu kama Lowassa alivyofanya na Citywater matokeo yake ndio maana JK anaonekana kiongozi dhaifu na asiyeweza kuongoza kutokana na urithi alochukua na kuapa kuboresha maisha ya wananchi...Kifupi JK kashindwa kuongoza, GDP inayoongezeka kwa mauzo ya mashirika ya nje hali mfuko wa Taifa haifaidiki na rasilimali/ maliasili zilizopo ni sawa na kujaribu kujaza maji ndoo iliyotoboka..Haisaidii kitu kupanda kwa GDP ikiwa hakuna kitu kinaongezeka ktk mfuko wa Taifa kulingana na mahitaji na kupanda kwa maisha..

Jibu langu hili limeangukia zaidi katika blue hio for the below paragraphs ni sum up ya hio paragraph of interest to me&#8230;. Unauliza ni kwa nini wanachi wanasikia uchungu zaidi leo&#8230; Hiyo ndio major question (na my whole point of this thread ni kua wale ambao walikua hawana habari kabisa na Siasa hapo nyuma ndo hao nilikuta wanabishana; it piqued my interest na kunifanya nikae nisikilize for long)

Sababu za kwa nini tokana na Mtazamo wangu&#8230;.

Majority Tanzanians tunataka CHANGE&#8230; change katika system of governance&#8230; Change katika Chama kinachoongoza na most importantly Change katika individual level ya mwananchi wa kawaida&#8230;. Kwa sasa what is happening or should I say what is not happening is bad, pressing and depressing.. BUT yet to me it is the best thing that has happened so far&#8230; for the Tanzanians needed that to wake up in their world of wonderland and unnecessary dreams&#8230;. Oh Tanzania inchi ya amani, Oh ya upendo&#8230;. What is Amani na Upendo kama wahusika sio Wazalendo na nchi yao na wala they don't give a damn what is happening- eti in the name ya Uongozi/Wanasiasa ndo wahusika&#8230; INABOA!!!

Watanzania kuwa interested saizi sio tu eti sababu ya Uongozi mbovu wa JK&#8230;. Bali pia na matukio ambayo yamekua exposed&#8230; Haya basi yamekua esposed na NO actions taken.. alafu hao watu ambao tuna hasira nao bado wapo katika Uongozi&#8230;.For instance toka zile scandals za Lowassa leading to his resignation; kaka for three years hajatamka kitu chochote Bungeni, only then anapoamua anaponda Uongozi huo huo wa Chama chake (thou yeye alikataa hakumaanisha &#8211; ila mjuvi anaelewa) kwa kushindwa toa maamuzi&#8230; Khaa!! Twaweza ona ka upuuzi vile - BUT kitu gani kinampa Lowassa such confidende?? Kitu gani kinamfanya JK ashindwe toa maamuzi?

Sisemi JK ni bora kuliko Mkapa &#8211; ila nasema woote hawafai hata kidogo kusifiwa&#8230; ndio kuweka siasa pembeni wana mazuri yao&#8230; thou mabaya yana overrun hayo mazuri&#8230; IMO Uongozi wa zaizi na madhaifu yake yootes ni bora for umeamsha Watanzania usingizini na kuwarudisha katika Tanzania ambayo
 
Tatizo la nchi hii siyo kiongozi mmoja mmoja kama watu wanavyotaka kutuaminisha. Tatizo ni mfumo wa kikatiba na kisheria unaotoa mwanya wa viongozi wabovu kuzalishwa, kulelewa na hadi kushika nafasi za juu za uongozi. Kwa taarifa yako tatizo la uongozzi nchi hii limeshuka toka kwa raisi mpaka kwenye ngazi za juu na za kati za uongozi wa serikali na kwa bahati mbaya hapo ndipo maamuzi makubwa ya matumizi ya pesa za walipa kodi yanapoanzia. Hata utamaduni wa utendaji kazi wa serikali hautuwezeshi kwenda mbele kwani umesababisha wataalamu kuwa mabingwa wa kusoma matakwa ya wanasiasa na kutoa ushauri unaoendana na mambo ambayo wanasiasa wanapenda kuyasikia. Kwa ufupi tupo kwenye tope zito "quagmire"na tunaendelea kuzama.

Tata hii post inakua kama conclusion ya my whole issue... tatizo sio JK or Mkapa pekee tatizo ni mfumo wao woote ambao ni mbovu...
Hio ikichanganywa na kiti kukaliwa na mtu mwenyewe sio mfikiri kama Mzee Ruksa ndo disaster zaidi.... inakua hadi pesa twatengeneza kila siku....
 
Naona hapa "great thinkers" wako bize wanajadili nani zaidi utadhani wako kwenye kipindi cha nani zaidi kwenye muziki cha redio one. Ninavyojua "simple minded people" ndio wanaopoteza muda wao kujadili watu.
 
Naona hapa "great thinkers" wako bize wanajadili nani zaidi utadhani wako kwenye kipindi cha nani zaidi kwenye muziki cha redio one. Ninavyojua "simple minded people" ndio wanaopoteza muda wao kujadili watu.

Nimeruka posts zijajibu for mpaka niifikie hii hamu itakua imekimbia....

If you read between the lines utagungudua there is more to it... and hata kama
we are looking at the differences... if they affect maisha yetu moja kwa moja
kuna ubaya gani.... Kama ni Mpenzi wa Soccer nafikiri utanielewa hua inakuaje\
ukikutana na mpinzani wako na the way waweza watetea or waponda wahusika...

Understanding the whole situation inabidi kuangalia from every angle possible plus all related aspects such as leadership...
 
Back
Top Bottom