Nguvu ya umma kutumika kuondoa watawala badala ya sanduku la kura kulikoni?

Ndachuwa

JF-Expert Member
Mar 8, 2006
6,269
4,569
Hivi karibuni wimbi la wananchi kuandamana ili kishinikiza viongozi wao waondoke madarakani hasa nchi zinazozungumza kiarabu limekuwa kubwa sana. Ikumbukwe nchi hizi kila baada ya muda fulani hufanya uchaguzi unaoitwa wa haki na huru.

Nisichoelewa ni kuwa wanaopiga kura ni kina nani na wanaoandamana ni kina nani? Maana kama wananchi wanapewa fursa ya kupiga kura kwani nini wasitumie sanduku la kura kuondosha utawala wasioutaka na badala yake wanatumia nguvu ya uma?

Mojawapo ya mambo ambayo yanagharimu pesa nyingi nchi zinazoendea ni gharama za kuitisha chaguzi. Sasa kama uchaguzi unaitishwa viongozi wanapatikana lakini raia wanaandamana kuukataa uongozi, ni kina nani waliopiga kura? Jee wanaosimamia chaguzi hizi wanahesabu kura za wananchi au wanakuwa na majibu yao wanayotaka?

Kama uchaguzi hauwezi kutoa viongozi bora, ni wakati muafaka kwa nchi zinazoendelea kubuni njia mbadala ya kupata viongozi badala ya kutumia pesa nyingi kuendesha chaguzi ambazo matokeo yake hayatawakilisha utashi wa wapiga kura.
 
Labda tatizo si sanduku la kura - kwani hata madikteta wanaweza kuwapatia wananchi hilo. Tatizo labda ni mfumo wa uchaguzi ambao unafanya aliyeko madarakai hawezi kushindwa!
 
Rais aliyekimbia Tunisa-Ben Ali alipata asilimia 99 kwenye uchaguzi uliopita! Hapo ndipo utagundua kuwa chaguzi za Afrika ni kiini macho. Watawala wetu wanasahau ule msemo kuwa unaweza kudanganya baadhi ya watu kwa muda fulani, lakini huwezi kuwadanganya watu wote siku zote.
 
1. Nafikiri wengi wanaiba kura waingie na wengine waendelee kubaki madarakani.....siamini wanashinda kihalali kwenye free and fair elections ndo maana watu wanaenda barabarani kuwatoa kwa nguvu.

2.kuna baadhi ya nchi kwa sababu moja au nyingine si kila mtu anaweza kupiga kura kama inavyopasa,mazingira yanatengenezwa ili iwe hivyo...ndo yale umejiandikisha unakuta jina halipo,makaratasi yamechelewa sijui nini....etc,sasa kukosa haki ya kuchagua kiongozi na kupata wasiomtaka ndo inachochea watu kwenda barabarani

3.Vitisho au sheria kandamizi na rushwa ...fikiria sheria kama zile za matokeo hayawezi pingwa,au mahakama hazina nguvu ya kwenda tofauti na mtawala ambaye pengine ndo kateua majaji, so watu hawawezi kwenda mahakamani as hamna haki..wanaamua kwenda kuwang'oa mahasidi wenyewe.
 
Katiba iliyoandikwa na Wananchi kwa faida ya wananchi ndiyo suluhisho.

Katiba ya Tanzania kwa mfano ni matokeo ya kuweka viraka vingi katika katiba ya Mkoloni,Katiba yetu hai reflect mawazo mtizamo na mwelekeo wetu Watanzania na hailengi katika kuwaondoa Watanzania katika umasikini na kuwafanya taifa lenye kujenga uchumi imara.
Katiba yetu iliandikwa kumlinda Nyerere kama Rais , kuwalinda wapambe wake na baadaye yalifanyika marekebisho kadhaa ilikuwalinda Marais wengine waliomfuata wapambe wao na mashabiki wao. Aidha kuna vifungu vingi vyenye kutoa mwanya kwa Rais au serikali kutoa tafsiri yeyote kadri ipendavyo.

Katiba ya Tanzania inatoa mwanya kwa Rais kuendeleza unyanyasaji wa Raia kwa kutumia sheria za kikoloni.
Katiba ya Tanzania inajenga mazingira ya kuwaenzi viongozi wa serikali katika ngazi zote hadi vijijini.
Katiba ya Tanzania inawanyima sauti wananchi na kuwapa nguvu Viongozi walio teuliwa na Rais au Wapambe wake.

Uchaguzi siku zote ni Rubber Stamp ya kuendeleza Utawala wa Mabavu.

Hata hivyo Uchaguzi wa viongozi wa Kitaifa ni Muhimu sana. Pingamizi lake kubwa ni sheria ya uchaguzi.Watawala wengi duniani hupindisha sheria za uchaguzi kwa gharama yeyote kwa Sababu wanaogopa sana Sauti ya Wananchi kupitia Sanduku la Kura kuliko waogopavyo mauti zao.
 
Labda tatizo si sanduku la kura - kwani hata madikteta wanaweza kuwapatia wananchi hilo. Tatizo labda ni mfumo wa uchaguzi ambao unafanya aliyeko madarakai hawezi kushindwa!


Ni hivi karibuni tu uchaguzi uliokwisha Rais Ali hassan mwinyi alitamka matamshi sawa na uliyotamka wewe na kusemsa CCM haishindwi.
 
ha ha ha i love this spirit...
but keep in mind,this is not Tunisia....
 
Hivi karibuni wimbi la wananchi kuandamana ili kishinikiza viongozi wao waondoke madarakani hasa nchi zinazozungumza kiarabu limekuwa kubwa sana. Ikumbukwe nchi hizi kila baada ya muda fulani hufanya uchaguzi unaoitwa wa haki na huru.

Nisichoelewa ni kuwa wanaopiga kura ni kina nani na wanaoandamana ni kina nani? Maana kama wananchi wanapewa fursa ya kupiga kura kwani nini wasitumie sanduku la kura kuondosha utawala wasioutaka na badala yake wanatumia nguvu ya uma?

Mojawapo ya mambo ambayo yanagharimu pesa nyingi nchi zinazoendea ni gharama za kuitisha chaguzi. Sasa kama uchaguzi unaitishwa viongozi wanapatikana lakini raia wanaandamana kuukataa uongozi, ni kina nani waliopiga kura? Jee wanaosimamia chaguzi hizi wanahesabu kura za wananchi au wanakuwa na majibu yao wanayotaka?

Kama uchaguzi hauwezi kutoa viongozi bora, ni wakati muafaka kwa nchi zinazoendelea kubuni njia mbadala ya kupata viongozi badala ya kutumia pesa nyingi kuendesha chaguzi ambazo matokeo yake hayatawakilisha utashi wa wapiga kura.
Hivi unategemea viongozi wa Afrika utawatoa kwenye uongozi kwa njia ya kupiga kura ,thubutuu,uliza akina Zenawi,Museveni,Bob,Mwai na wengine siwataji nisije funguliwa mashtaka bure ,
 
Nilipata kufikiri wakati fulani...kwamba kwanini wanazuoni wetu wasiende mbali zaidi kwa kubuni mfumo ambao ni wakudumu na ulio wazi zaidi?
Hivi kweli watu wa Telecom/ Electronic Eng/comp Science/IT wanashindwaje kubuni card ya kielektroniki ambayo inakua na detail za mwananchi na ifikapo wakati wa Uchaguzi mwananchi aweze kutumia haki yake ya msingi bila kulazimika kujipanga ama kurudi kwenye maeneo waliojiandikishia....km imewezekana kwa Master Card/Visa card na driving license kwa wenzetu kwanini msijipatie PHD zenu hapa.....

Taaluma yangu ni tofauti na nilizotaja ila nafikiri naweza kueleza kwa ufasaha namna mfumo naofikiri unavyoweza ku operate kwa hakika na salama na kupunguza migogoro na migongano isiyokwisha hususan kwa nchi zetu zinazoendelea! Embu tuthubutu!
 
Nilipata kufikiri wakati fulani...kwamba kwanini wanazuoni wetu wasiende mbali zaidi kwa kubuni mfumo ambao ni wakudumu na ulio wazi zaidi?
Hivi kweli watu wa Telecom/ Electronic Eng/comp Science/IT wanashindwaje kubuni card ya kielektroniki ambayo inakua na detail za mwananchi na ifikapo wakati wa Uchaguzi mwananchi aweze kutumia haki yake ya msingi bila kulazimika kujipanga ama kurudi kwenye maeneo waliojiandikishia....km imewezekana kwa Master Card/Visa card na driving license kwa wenzetu kwanini msijipatie PHD zenu hapa.....

Taaluma yangu ni tofauti na nilizotaja ila nafikiri naweza kueleza kwa ufasaha namna mfumo naofikiri unavyoweza ku operate kwa hakika na salama na kupunguza migogoro na migongano isiyokwisha hususan kwa nchi zetu zinazoendelea! Embu tuthubutu!

Tunashindwa kuinua Kilimo Tanzania kwa kufanya jambo dogo tu la kununua Matrekta,tena USED ,na kuachana na jembe! Tutaweza hiyo kitu yenye kuingiza techknowhow??
Tatizo si umasikini wetu ila ni jinsi tulivyo amua kwa moyo mmoja kuridhika na umasikini

Kuorodhesha wapiga kura si tatizo hata kidogo pia si chanzo cha tatizo.
tatizo ni jinsi dafatari la wapiga kura linavyonajisiwa na CCM ili waendelee kushinda chaguzi
Nia na Madhumuni ya kuleta migongano katika orodha ya wapiga kura iko wazi kuvuruga uchaguzi ili kuwezesha wao CCM kufanya watakalo.
 
Mkuu Madela wa Madilu nakusoma...pamoja na ukweli kwamba nchi inaenda km hakuna kiongozi nilikosa haki yangu ya msingi/Kikatiba kupiga kura.Hii ilitokana na mfumo uliowekwa ambapo wakati wa uandikishaji wa mwanzo nilikua Umalila kwa Wandali,wakati wa kuboresha ukanikuta Kihonda Morogoro na wakati wa kupiga kura nikawepo Mto wa mbu-Monduli!
 
Hivi unategemea viongozi wa Afrika utawatoa kwenye uongozi kwa njia ya kupiga kura ,thubutuu,uliza akina Zenawi,Museveni,Bob,Mwai na wengine siwataji nisije funguliwa mashtaka bure ,
Ungemtaja tu Kikwete. Tunajua naye alitumia mfumo wa Mubarak kubaki mamlakani Tanzania.
 
Viongozi wa Africa wakishaingia kwenye madaraka hawapendi kuondoka ,sijui kuna nini kwenye Ikulu zetu na kama itaonekana yuko katika hati hati za kuondolewa madarakani ,Ni lazima ataagiza ifanywe kila namna aendelee kubaki madarakani,
Hivyo basi masanduku ya kura si mwamuzi wa nani atawale bali ni nguvu za kibabe ndio zinaamua
 
Zaidi ya wachangiaji kumi wanaeleza kuwa haki haitendeki kwenye sanduku la kura. Swali, wanaosimamia upigaji kura na wale wanaoandamana si wamoja? Nina maana wahudumu kwenye vituo vya kupigia kura mfano hapa Tanzania si raia wa kawaida wanaokusanywa tuu mitaani? Wanaacha kutenda haki kwa faida ya nani wakati wao ni sehemu ya jamii inayotawaliwa?
 
Katiba iliyoandikwa na Wananchi kwa faida ya wananchi ndiyo suluhisho.

Katiba ya Tanzania kwa mfano ni matokeo ya kuweka viraka vingi katika katiba ya Mkoloni,Katiba yetu hai reflect mawazo mtizamo na mwelekeo wetu Watanzania na hailengi katika kuwaondoa Watanzania katika umasikini na kuwafanya taifa lenye kujenga uchumi imara.
Katiba yetu iliandikwa kumlinda Nyerere kama Rais , kuwalinda wapambe wake na baadaye yalifanyika marekebisho kadhaa ilikuwalinda Marais wengine waliomfuata wapambe wao na mashabiki wao. Aidha kuna vifungu vingi vyenye kutoa mwanya kwa Rais au serikali kutoa tafsiri yeyote kadri ipendavyo.

Katiba ya Tanzania inatoa mwanya kwa Rais kuendeleza unyanyasaji wa Raia kwa kutumia sheria za kikoloni.
Katiba ya Tanzania inajenga mazingira ya kuwaenzi viongozi wa serikali katika ngazi zote hadi vijijini.
Katiba ya Tanzania inawanyima sauti wananchi na kuwapa nguvu Viongozi walio teuliwa na Rais au Wapambe wake.

Uchaguzi siku zote ni Rubber Stamp ya kuendeleza Utawala wa Mabavu.

Hata hivyo Uchaguzi wa viongozi wa Kitaifa ni Muhimu sana. Pingamizi lake kubwa ni sheria ya uchaguzi.Watawala wengi duniani hupindisha sheria za uchaguzi kwa gharama yeyote kwa Sababu wanaogopa sana Sauti ya Wananchi kupitia Sanduku la Kura kuliko waogopavyo mauti zao.

Mkuu mifano yako ungeielekeza kule haya mambo yanapotokea kabla ya kuingiza Tanzania kwenye huu mjadala; tatizo linatokea nchi zinazozungumza kiarabu, lenga huko
 
Rais aliyekimbia Tunisa-Ben Ali alipata asilimia 99 kwenye uchaguzi uliopita! Hapo ndipo utagundua kuwa chaguzi za Afrika ni kiini macho. Watawala wetu wanasahau ule msemo kuwa unaweza kudanganya baadhi ya watu kwa muda fulani, lakini huwezi kuwadanganya watu wote siku zote.

Kikwete alipata 44% lakini ndiye raisi wenu!
 
Tunazungumzuia yanayotokea kwenye nchi zinazozungumza kiarabu. Waswahili hatuna shida maneno mengi........... BTW Hujagonga

Hakuna demokrasia ya kweli kwenye nchi za kiarabu kama ilivyo kwenye nchi zetu! wale wasiotakiwa hulazimisha kuongoza hata kama si kwa ridhaa ya wananchi. Sulutisho rahisi ni kuingia mitaani kama ilivyo Egypt na Sudan
 
Hakuna demokrasia ya kweli kwenye nchi za kiarabu kama ilivyo kwenye nchi zetu! wale wasiotakiwa hulazimisha kuongoza hata kama si kwa ridhaa ya wananchi. Sulutisho rahisi ni kuingia mitaani kama ilivyo Egypt na Sudan

Una maana matokeo ya kura yanayotangazwa si ya kura zilizopigwa na wananchi? Naona kama unanichanganya
 
Una maana matokeo ya kura yanayotangazwa si ya kura zilizopigwa na wananchi? Naona kama unanichanganya

Ndiyo maana yake! Ben Ali alishinda kwa 99% huyu Mubarak 95% kama ingekuwa kweli watu wasingekuwa mitaani! Look at the mirror and reflect what I have just said.
 
Back
Top Bottom