wana jamvi naomba matokeo ya mechi kati ya yanga na simba maana nimekutana basi la yanga linaenda bungeni sasa sijajua ni kwenda kupongezwa au kufarijiwa, ni hayo
nimeshajua nani kapakatwa jana ni yanga...jaribuni tena mwezi wa kumiUtajibeba! Bungeni mnyama hawezi kuingia......kombe la mbuzi kwenye bunge TUKUTU likafanye nini?? Mimi nilidhani mmekwenda kuling'oa lile bango pale Makumbusho!! Lol.
kama ni mshabiki au mpenzi wa takwimu hebu anzia mwaka 2001 mpaka leo halafu uje na matokeo..haha hahahaha pole sana yebo yeboNakubali yanga kapakatwa JANA TU, lakini simba tunampakata kila siku hapa Makumbusha na kwingineko! Tehe!
kama ni mshabiki au mpenzi wa takwimu hebu anzia mwaka 2001 mpaka leo halafu uje na matokeo..haha hahahaha pole sana yebo yebo
Kwanini tuanzia 2001 wakati timu zimeanzishwa 1930's? Tuanzia huko basi! Kipofu kaona mwezi na kombe lake la mbuzi!
kama vile JK na MBOWE wote YANGA lakini katika siasa wapo tofautiKaka, masuala ya siasa ukiyaingiza ktk sport maisha yako utayavuruga kabisa.
Hakuna cha kuihusisha Yanga na CCM zaidi ya rangi zao kufanana.
Sitta, Zitto Kabwe ni Simba damu lakin wanaelewa kutofautisha siasa na sports. Mpira ni burudani, sio kama siasa. Stress za siasa zisihamaishiwe ktk michezo. Hata ukiangalia maana na malengo halisi ya Sports ni kuleta amani ktk jamii na kuboresha afya za binadamu, ingawaje sasa ni sehemu ya ajira.
Wewe ndio unatakiwa upanue akili yako vizuri, jiulize ni kwa nini club ya Yanga imejengwa na Karume, halafu uwanja unaitwa Kaunda? wewe hakuna unachokifahamu.Panua akili yako, ona mbele zaidi. Kila mtu anasema, na hata Chadema na CUF wanakiri waziwazi kwamba CCM ya Mwalimu J.K. Nyerere ilikuwa na maadili ya uadilifu wa hali ya juu. Hii ndio sababu ya Yanga kuimba CCM, CCM kutokana na uadilifu huo.
Au la, wewe utakuwa ni mtoto wa miaka ishirini na kitu, ndio maana unaongea hivi.
Yanga wanashangilia hivyo tangu miaka ya 70, na sasa imekuwa kama mazoea tu