Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Siku moja nikiwa foleni pale NMB morogoro,kuna wanachuo wawili wa SUA walikuwa wakirushiana miziki na videos kwa simu zao.Mbele yangu alisimama mzee mmoja na mvi zake,mkononi kashika simu lake kubwa la mchina huku amelisahau likiwa bluetooth on.Mara simu yake ikatoa request ya bluetooth connection,huku kapigwa na butwaa,aka-accept.File likaanza kuwa loaded,1%,15%,94%,100%...new video received,open it?,mzee akabonyeza,'YES'.Kilichotokea ni balaa kubwa duniani na homa kilo 10,ilikuwa ni PORNOGRAPHIC VIDEO!.Ndani ya benki pakiwa na utulivu wa hali ya juu ilishamiri miguno ya kingono ngono tena kwa sauti ya juu kabisa ya simu ya kichina.Mzee wa watu alichanganyikiwa,macho yote kwake,kila akijaribu kuizima ndo kwanza akawa anaongeza volume ya sauti.Mzee akaona isiwe shida,akang'oa battery ya simu na hatimaye pale ndani pakawa shwari huku kila mtu akiwa haamini alichokisikia na kukiona.Simulia sana ila usiombe yakukute.OVER.