Neno La Leo: Hizi Ni Zama Za Mabadiliko

TANMO,

Ahsante sana. Sishangai kuwa sieleweki kwa wengine. Jamii yetu haina mazoea ya watu kama mimi. Lakini najua, kuna wanaonielewa. Natumai iko siku utanielewa.

Maana, kuna wanaofikiri, kuwa Maggid Mjengwa ni CCM. Kuna wanaofikiri kuwa mimi ni CHADEMA, kuna wanaofikiri kuwa mimi ni CUF, kuna wanaofikiri kuwa mimi ni Muislamu. Kuna wanaofikiri kuwa mimi ni Mkristo. Wote hao wanabahatisha.

Sijapata kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa. Ningependa nikumbukwe, kuwa Maggid Mjengwa alikuwa Mtanzania na Mjamaa aliyejitahidi kufanya yale aliyoamini yana maslahi kwa Tanzania, basi.

Maggid,
Iringa,
Jumapili, Februari, 12, 2011
mjengwa

Maggid,

Kuhusu jamii yetu kutokuwa na mazoea ya kuwaelewa watu kama wewe, sijui. Ila binafsi sikuelewi kwa misingi kuwa mwandishi yeyote makini huwa na itikadi pamoja na msimamo wake thabiti juu ya kile anachoandika. Kusema kwamba wewe huna Chama napata mashaka kwa maana kwamba, kama ni kweli, basi ungekuwa unaandika makala zako bila kuegemea upande wowote, vinginevyo unajenga mazingira ya kuonekana mnafki ilhali siyo mnafki au ndiyo matokeo ya watu kutokukuelewa kama inavyotokea kwenye makala zako nyingi.

Kwenye mikanganyiko kama hii kuna mjinga mwiongoni mwetu (siyo kwa maana ya tusi).. Hivyo tuweke hisia kando tuchekeche fikra zetu na tuuondoe ujinga wetu kwa manufaa yetu na Taifa kwa ujumla.

Ubarikiwe sana.


N.B.. Heri ya Jumapili huko kwenu.
 
wananchi wanaodanganywa kwa kutishiwa Amani siku zote huwa ni masikini na hiyo ndiyo hali hakisi ya Tanzania.
Nchi zote zilizoendelea kwa njia moja ama nyingine zilipitia au zinapitia social/political/economical conflicts like civil war in USA during MLK ndio hayo matunda ya USA kwa sasa.
Ukiangalia China pia utaona yale maandamano yaliyofanyika TianAnmen Square ingawa watu wengi waliuliwa hiyo ndiyo iliyokuwa turn up point kwa China , na mifano mingine mingi tu.
Ttaizo kubwa wa watz ni kuwa ni waoga na wanafiki sana katika mambo ya msingi.Mtu anaumwa amelazwa hospitalini unamwuliza anakujibu SALAMA, je hiyo salama iko wapi? tumezoelea?
hiyo ndio hali kadhalika yetu tumezoelea kila kitu, tumezoelea kutoa Rushwa na tunaona ni sehemu ya maisha yetu eti nisipotoa sitahudumiwa, wakati mwingine hata mhusika hajakuomba ila ni ujinga na uwoga wetu wenyewe mtu unaanza kutoa pesa mwenyewe?
Una nunua haki yako? je hao waliopewa kulinda haki hizo wanapoona hayo sio kwamba ndio wanaanza kupigilia kabisa.
Matatizo yetu mengi yamesababishwa na sisi wenyewe.
Wengine wanasema Bila CCM Nchi Itayumba
 
Maggid watu wanakushambulia sana bro mi naona kinachoongelewa ujue kina chanzo anza wewe kwanza na hayo mabadiliko ili tuwe na sauti moja, nia moja , adhma moja na hakika tutafika.
 
Ndugu Zangu,

Viongozi Afrika wanapaswa kutambua sasa, kuwa Mwafrika wa mwaka 1975 si Mwafrika wa mwaka 2011. Waafrika wameamka. Viongozi Afrika wana lazima ya kuendana na mabadiliko ya wakati. Hizi ni zama za mabadiliko. Na Mabadiliko ya amani Afrika yanawezekana, mwenye kuyazuia mabadiliko ya amani, atambue, kuwa mabadiliko yenye vurugu hayaepukiki. Hilo la mwisho lina hasara kubwa. Mungu Ibariki Afrika.

Maggid
Iringa,
Jumamosi, Februari 12, 2011
mjengwa



Kweli upepo wa Tunisia umeenea Misri na nchi nyingine za Kiarabu.Kwa sababu umeenea nchi za kiarabu haitunyimi nafasi ya kutafakari kama tupo kwenye mstari sahihi wa kuepukwa na kimbunga hicho

Kwetu watanzania yapo mambo ya msingi ya kuleta mabadiliko ili usawa na amani ya rohoni iwepo.katika mchano wake bungeni jana Mbunge wa Musoma mjini Vicent Nyerere amesema kwamba Tanzania kuna utulivu tu lakini amani hakuna.Amani hakuna kwa sababu amni inakaa rohoni .Watanzania sasa wanalala sehemu za hali ya chini , chakula shida na elimu kwa mtoto wa masikini ni ya hali ya chini sana ( shule za kata )

Tufanye nini?

Kwanza lazima wabunge wetu waache taarabu bungeni wajue kwamba wakiwa bungeni wamebeba matarajio ya mamilioni ya watanzania.Sasa inashangaza kwamba mbunge anasimama na badili ya kuishauri serikali cha maana anaanza kushambulia chama flani ( CDM ) ili tu ajipendekeze kwa watawala.Hajui kwamba kazi yake pale sio kutumikia chama bali mwananchi.


Pili Serikali lazima itumie kodi zetu kwa uwazi na kupunguza ubadhirifu serikalini.kwa njia hii pekee ndo itapunguza kutoaminiana kati ya serikali na watu wake.Serikali ya chama tawala lazima warudishe mifuko iliyoibiwa ili fedha hizo zijeuzwe kuwa huduma kwa wananchi.Tumjue mmiliki wa Kagoda ili bil 40 tuzijeuze nyumba za walimu ili kwamba mwalimu au wataalamu wakipanga kwenda kutenda wajibu wao sehemu mbalimbali ya nchi hii waende na waridhike na mazingira.Kama hawamjui mmiliki wamwulize Yusuph Manji kwani alikopa fedha kutoka kagoda kupitia kampuni yake ya Quality Finance.

Kilimo kimekuwa kinatajwa tu na wanasiasa kwamba kinachangia asilimia kubwa katika uchumi wa mtu mmojammoja tanzania.Kenya kwa sasa kilo moja ya kahawa inauzwa mnadani dola 15 hadi 20 wakati hapa Tanzania wanunuzi wananunua kahawa mnadani dola 3 hadi 5.3 hili ni Tusi.Kenya wao wameweka sera inayochochea mkulima kuongeza ubora wa kahawa yake.Huku kwetu mkulima ananyongwa tu .Sheria inazipa halmashauri idhini ya kukusanya ushuru wa mazao kutoka kwa mkulima kwa asilimia 5% ya bei ya shambani.Sasa halmashauri zinafanya nini na huu ushuru? Mbona bado hakuna mradi wowote mkubwa wa umwagiliaji ili kilimo kiwe endelevu? Serikali inahitaji kuchukua hatua za haraka kuhuisha uchumi wa vijiji vyetu ili watu walime wauzi na wapante nguvu ya kununua bidhaa nyingine (Purchasing power) vinginevyo upepo wa tunisia hatutaukwepa!

Hop mmenisoma.
 
Mggid ndugu yangu,

Naona kabisa bado hujajibu hoja ya TANMO

Jitahidi ujibu hoja hiyo. Wengi hatukuelewi si kwa sabubu wewe ni CCM, CDM, CUF or UDP au wewe ni Mkristo, Islam au Kafiri --- bali wengi hatukuelewi kwa jinsi makala zako zinavyopinzana. Hii ndo hoja ... ebu iweke sawa ili tukuelewe.
MASUALA YA UDINI NI MAGENI KWETU - Usiyalete hapa. Jitahidi ujibu hoja.

TANMO,

Ahsante sana. Sishangai kuwa sieleweki kwa wengine. Jamii yetu haina mazoea ya watu kama mimi. Lakini najua, kuna wanaonielewa. Natumai iko siku utanielewa.

Maana, kuna wanaofikiri, kuwa Maggid Mjengwa ni CCM. Kuna wanaofikiri kuwa mimi ni CHADEMA, kuna wanaofikiri kuwa mimi ni CUF, kuna wanaofikiri kuwa mimi ni Muislamu. Kuna wanaofikiri kuwa mimi ni Mkristo. Wote hao wanabahatisha.

Sijapata kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa. Ningependa nikumbukwe, kuwa Maggid Mjengwa alikuwa Mtanzania na Mjamaa aliyejitahidi kufanya yale aliyoamini yana maslahi kwa Tanzania, basi.

Maggid,
Iringa,
Jumapili, Februari, 12, 2011
mjengwa
 
Matola ndugu yangu,

Kwanza,

Nimefurahi sana kusikia ni msomaji wangu wa miaka mingi.
Pili, nakushukuru kwa kuniomba radhi. Huo ndio uungwana. Nimekusamehe na sina kinyongo nawe. Unajua, niliudhunika niliposoma haya uliyoyaandika, nakunukuu " Kwangu mimi mnafki ni mnafki tu, labda utueleze ni lini umejiondoa kwenye payroll ya CCM, sidhani kama napaswa kukuheshimu kama mwandishi huru zaidi ya kukuweka kwenye kundi la waganga njaa na mtaji wenu ni kalamu tu, shame on you." Mwisho wa kukunukuu.

Kijana wangu wa miaka 15 alishangaa sana aliposoma hayo. Kwamba baba yake nina mshahara mwingine ambao hata yeye hajausikia, eti niko kwenye payroll ya CCM! Na tangu lini nimejiunga na chama hicho?

Nikwambia mwanangu, kuwa hawa wenye kujiita ' Great Thinkers' ni binadamu kama wengine. Wakati mwingie hughafilika.
 
Back
Top Bottom