Ndalichako: Tozo kwenye mshahara inaangaliwa upya

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Jan 29, 2021
573
2,553
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, vijana, ajira na wenye ulemavu) Mhe. Joyce Ndalichako amesema kuwa malalamiko ya wafanyakazi kuhusu makato ya mishahara yao yanashughulikiwa kwa kuwa serikali sikivu ya awamu ya 6 imesikia kilio chao.

Waziri amewataka wafanyakazi kuviamini vyama vyao kwa kuwa vimewasemea vizuri na sasa wataangalia upya makato haya ya tozo.

Amesema kuwa serikali itakuja na jawabu sahihi, waondoe wasiwasi na waendelee kuchapa kazi kwani hoja zao zote zitafanyiwa kazi.

Ili kusisitiza hoja hii, waziri ametanabaisha kuwa serikali iliwapandishia madaraja tena kwa mserereko na baadhi iliwabadilishia muundo wao wa kazi. Amewaomba wafanyakazi wote kuendelea kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan katika juhudi zake za kuijenga nchi.
 
Hii nchi mbona imekuwa danguro. Yani wanafanya mambo halafu watu wakihoji jibu linakuja kiwepesi tu kuwa litaangaliwa.

Sasa jopo lote la wabunge linafanya nini pale Dodoma kupitisha hizi sheria bila kuangalia athari zake?
Mwigulu matozo anakwambia tutaangalia, huyu mama nae asiejielewa anakwambia tutaangalia. Walishindwa vipi kuangalia kabla kupitisha.
 
Wizara nyingi zinaongozwa na akili ndogo sana zinazocheza kufuata upepo. Ona huyu murundi mwenzangu anavyoongea utadhani ni la 3C.

Burundi ndiko tunakoshauriwa turejee na boya mmoja hivi
 
Mpaka watakapomaliza kujiangalia wangapi watakuwa wamefunga akaunti benki? Hakukuwa na kujifunza kwenye tozo za miamala ya simu?

Kampuni za simu, mawakala na wengine kwenye mnyororo wa miamala ya simu wamesha recover from experiment ya tozo baada ya serikali kusikia vilio na kujirudi?
 
Mara huku wananchi walipitisha tozo huku serikal itapitia upya tozo mnatuchanganya mjue sisi hatutak hayo yote tunataka pambano la mandonga na kaoneka lirudiwe maana si ndo mnavyotaka
 
Yaani unaktwa mshahara... Ukienda kuuchukua benki, unapigwa panga tena.... Maninaaaa!!!!!
 
Back
Top Bottom