Nchi za Afrika zinaendelea kuunga mkono sera ya kuwepo kwa China moja

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
1706077118720.png

Kwa muda mrefu sasa jumuiya ya kimataifa imeendelea hatua kwa hatua kuitambua sera ya kuwepo kwa China moja kama ilivyo kwenye sheria ya kimataifa, sera inayosema kuwa kuna China moja tu duniani, na Taiwan ni sehemu isiyotengeka ya China. Nchi mbalimbali duniani ambazo kwa sababu moja au nyingine licha ya kutambua ukweli huo, zilikuwa na uhusiano wa kidiplomasia na kisiwa cha Taiwan, zimevunja uhusiano huo na sasa zina uhusiano wa kibalozi na China. Nchi ya karibu zaidi kufikia hatua hiyo ni Nauru.

Katika siku hizi hivi karibuni watu wa Taiwan walifanya uchaguzi wa kiongozi wa kisiwa hicho, na kumpigia kura aliyekuwa makamu wa mkuu wa kisiwa hicho Bw. Lai Ching-te kuwa kiongozi ajaye. Kuchaguliwa kwa Lai kunaendeleza uwepo madarakani wa chama Democratic Progressive Party (DPP), ambacho kuna nyakati sera zake zimekuwa na utata na kuleta migongano kuhusu uhusiano kati ya pande mbili za China bara na Taiwan.

Suala la Taiwan ni suala nyeti la ndani la China, lakini kwa bahati mbaya suala hilo limeendelea kwa muda mrefu kuwa kichochoro cha baadhi ya nchi za magharibi kuingilia mambo ya ndani ya China. Kwa upande mmoja, wanasiasa wa Marekani wamekuwa wakilitumia suala hilo kama daraja la kujitafutia uungaji mkono kutoka kwa baadhi ya watu wa Marekani hasa wale wenye asili ya Asia, na kwa wale wanaopendelea siasa za kibeberu. Kwa upande mwingine, wanasiasa wa ndani wa Taiwan wamekuwa wakitumia kampeni za kipindi cha uchaguzi kujaribu kuchochea hisia za ufarakanishaji, ili kupata uungaji mkono kwenye uchaguzi. Wakati mwingine, wanasiasa hao wanakuwa ni vibaraka wa nchi za magharibi, na wanakuwa ni daraja la kuingilia mambo ya ndani ya China.

Lakini suala hilo limekuwa ni kipimo muhimu kwa ukaribu na kuaminiana kisiasa kati ya China na bara la Afrika kwa ujumla. Kuna wakati nchi 30 za Afrika zilikuwa na uhusiano wa kibalozi na Taiwan, lakini sasa ni nchi moja tu ya Eswatini (Swaziland), ndio imebaki kuwa na uhusiano na Taiwan. Sababu ya nchi za Afrika kuhamisha uhusiano huo ni kutokana na ukweli kwamba imekuwa na uhusiano mzuri na nchi za Afrika tangu enzi ya harakati za kupigania uhuru, kujitokeza kuzisaidia nchi za Afrika wakati wa majanga na matatizo, na hata kuwa na nchi za Afrika zinapokabiliwa na shinikizo kwenye jukwaa la siasa za kimataifa.

Hivi karibuni Baraza la Wawakilishi la Marekani lilipitisha muswada wa sheria inayoitwa “Sheria ya Kutoibagua Taiwan ya 2023”, ambayo inaiagiza wizara ya fedha ya Marekani kutumia nguvu yake ya ushawishi kwenye Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kuunga mkono uanachama wa Taiwan katika shirika hilo. Kwa mujibu wa sheria za kimataifa, Taiwan si nchi, bali ni sehemu ya nchi, kwa hiyo kimsingi haina sina ya kuwa “nchi mwanachama”. Lakini Marekani ina kawaida ya kupuuza sheria za kimataifa na kutumia vigezo viwili, kila inapotafuta mwanya wa kuingilia mambo ya ndani ya nchi nyingine.

Hata hivyo jumuiya ya kimataifa inaendelea kutambua ukweli kwamba kuna China moja tu, Nauru imethibitisha hivyo, na hivi karibuni wakati waziri wa mambo ya nje wa China Bw. Wang Yi alipokuwa ziarani nchini Togo, waziri mkuu wa nchi hiyo, kama ilivyo kwa viongozi wa nchi nyingine za Afrika, alisisitiza kuwa Togo itaendelea kufuata sera ya kuwepo kwa China moja.
 
Nikiwa mdogo nilikua naona bidhaa Made in Taiwan, hivi bado zipo? Siku hizi naona Made in China pekee.
 
Back
Top Bottom