Andindile
JF-Expert Member
- Mar 18, 2009
- 304
- 16
Nchi ya Zanzibar huenda ikafutika kwenye uso wa Dunia kama nchi iliyoungana na Tanganyika na kubaki kama mikoa ya Tanzania. Hii ni kwa sababu jina linalotakiwa kuzitambulisha nchi mbili zilizoungana (Tanganyika na Zanzibar) yaani Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania (JMT) au United Republic of Tanzania (URT) limeanza kutotumika katika sehemu muhimu za utambulisho wa nchi hasa yanayohusiana na muungano. Mfano kwenye sarafu, linatumika "shilingi ya Tanzania" badala ya "shilingi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" au "Tanzanian Sh". badala ya "United Republic of Tanzania Sh." (URT. sh.), kama ilivyo kwa "United States dollar" (US $), "United Kingdom Pound" (UK pound). Pia jina la ramani, huitwa Ramani ya Tanzania badala ya "Ramani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania". Timu ya Taifa huitwa "timu ya taifa la Tanzania" badala ya "Timu ya Taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania". Na sehemu nyingine nyingi ambako jina la URT lingetumika badala yake Tanzania ndilo hutumika.
Wazanzibari amkeni mhakikishe utambulisho unaotumika ni wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (JMT) au United Republic of Tanzania mahali popote pale ambapo maslahi ya nchi mbili huru zilizoungana yanawakilishwa la sivyo you will be forgotten forever!
Wazanzibari amkeni mhakikishe utambulisho unaotumika ni wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (JMT) au United Republic of Tanzania mahali popote pale ambapo maslahi ya nchi mbili huru zilizoungana yanawakilishwa la sivyo you will be forgotten forever!