Nchi inaondeswa na mamisheni town

tz1

JF-Expert Member
Mar 19, 2011
2,121
534
Leo jiono kutoka namanga mpaka sayansi nimetumia masaa mawili kwa gari,
ni aibu kubwa sana.
Tatizo letu sisi wa tz tunauoga kuongelea na kudai haki zetu.
Mafuta ya gari kidogo unayokuwanayo yanaisha kwenye foleni,
wakati wanaojiona wajanja waruka angani,bila matatizo.


 
Hata zikijengwa fly overs,utashangaa kuona mtu atapewa kibali
cha kujenga kituo cha mafuta kwenye fly over.hii ndo bongo bwana
 
Leo jiono kutoka namanga mpaka sayansi nimetumia masaa mawili kwa gari,
ni aibu kubwa sana.
Tatizo letu sisi wa tz tunauoga kuongelea na kudai haki zetu.
Mafuta ya gari kidogo unayokuwanayo yanaisha kwenye foleni,
wakati wanaojiona wajanja waruka angani,bila matatizo.

MKUU

KWANI KUNA LAZIMA YA Kuja kulalama hapa.
nyie si ndio mnatawala. hayo si ndio maisha bora
na bado ungetumia masaa 8 ndio ungelewa vyema CCM imeshika hatamu
nadhani 2015 mtawaambia wadanganyika mtaanzisha safari za anga kutoka posta-tegeta,posta gogolamboto,posta kimara nk
 
Leo jiono kutoka namanga mpaka sayansi nimetumia masaa mawili kwa gari,
ni aibu kubwa sana.
Tatizo letu sisi wa tz tunauoga kuongelea na kudai haki zetu.
Mafuta ya gari kidogo unayokuwanayo yanaisha kwenye foleni,
wakati wanaojiona wajanja waruka angani,bila matatizo.



Kiukweli tumekuwa watumwa ndani ya nchi yetu. Matatizo kama haya sio mageni hapa duniani. Kuna mwanajursiprudensia mmoja alipata kunena kwamBa " Serikali ni mkataba kati ya watawala na watawaliwa" Hii inamaanisha kuwa uhusiano tulionao kati yetu na viongozi wetu ni mkataba kama mikataba mingine, Kama upande mmoja kati ya waliongia mkataba hautaridhishwa na mwenendo mbovu juu ya mkataba unaotendwa na upande wa pili wa aliyeingia mkataba, ni dhahiri kuwa upande uwo ambao hujaridhishwa na mkataba husika unaweza kuamua kuvunja mkataba uwo.

Kwa mwenendo wa serikali hii iliyopo madarakani imefikia hatua wananchi tunapaswa kuvunja nayo mkataba. Kwa tukio hili la janga la mafuta hapa nchini lililosababishwa na serikali dhidi ya wananchi wake, sisi wananchi tulitakiwa tushike mabango tuingie barabarani tukionyesha nia yakutaka kuvunja mkataba huu na serikali iliyopo madarakani.Hili janga la mafuta ni golden chance ambayo inatuwezesha wananchi kuamasisha serikali ijiengue kwa makosa inayofanya.

Watanzania tunahisia ya kumtoa mkoloni mweusi madarakani ila tunakuwa wanafki tunaishia kuongelea ili swala vyumbani mwetu. Swala la maandamano ya kuipinga serikali tusiwaachie vijana wetu wa sokoni na vijana wa vijiweni. Katika nchi mbalimbali ambazo wananchi wametimiza adhma yao kwa kutumia maandamano yamewajumuisha wakulima,wafanyabishara,wanavyuo,wafanya kazi ni wale wote wasio na kazi kwani wote hawa ndo waadhirika wa mfumo mbovu wa serikali. Watanzania tusiwe wanafki wala waoga na kuwaachia vijana wasio na kazi au wenye vipato vya chini pekee ndio washike mabango na kuandamana kupinga mfumo mbovu wa serikali yetu sote.

Tuonyeshe kujitambua na kuionyesha serikali nia ya wazi ya kutokubaliana na mwenendo wake kwa kudai haki yetu ya msingi kwa njia ya maandamano kama mataifa mengine yalioonyesha utayari huu. Tunayoyasoma kwenye historia yasiishie kwenye vitabu tu, bali yatupe motisha wa kufanya yaliyofanywa na wenzetu waliotangulia kufanya. Tusione aibu kushika bango linaloonyesha haki ya msingi tunayoidai.

Hili ni janga la taifa zima kwa ujumla hatunabudi kuweka pembeni hisia zetu za vyama kwa kuzingatia ukweli na haki. Kwa pamoja tupaze sauti na kuikemea serikali pale inapokosea, Tukubali ukweli na kupingana na uongo, tuweke misimamo yetu ya kichama pembeni ili kwa pamoja tukatae giza na kukubali mwangaza. Tusigawanywe na vyama alafu tufumbwe na tupumbazwe ili tusiseme ukweli na kudai haki.

Tukipaza sauti kwa pamoja pasipo kupumbazwa na hisia za kivyama hakika tutasika na mkoloni mweusi atadondoka pale anapotunyima tusulubu kwa mfumo mbaya wa uongozi.

Kenyatta mkubwa alishawai kumuambia Mwl Julius Kambarage Nyerere kuwa "Mwalimu unaongoza maiti" akiwa anamaanisha Watanzania wamepumbaa kiasi cha kupelekeshwa kwa namna yoyote viongozi wao watakavyoamua.

Tubadilike tufanye maamuzi magumu sote kwa pamoja tuseme ndio pale tunaporidhiswa na mfumo mzuri wa serikali, pia tupaze sauti kwa pamoja tuseme hapana pale ambapo hatutaridhishwa na mfumo mbovu wa serikali. Tusikubali tena kupoteza golden chance ya kuinyooshea serikali kidole kwa kuandamana tutakayoipata pale mfumo mbovu wa serikali utakapojitokeza.

TUAMKE USINGIZINI WATANZANIA.
 
Daudi mchambuzi;

Mkuu Imekugusa sana!!

.... KUPUMBAA (Hypnotic Zombie) NI TATIZO LA KIUFAHAMU !

... Ni taofauti na tatzo la Kiakili!!

... Watanzania ..akili na janja ..Nyingi ...Ufahamu sifuri

... Till when we can distingusih the two ... we r in hot soup!!






 
pole sana mdau ndio jiji la bongo hilo hakuna hata program za kutanua
Leo jiono kutoka namanga mpaka sayansi nimetumia barabara za mijini wenzetu nairobi na kampala ndo wanatuacha hivyo kwa ma fly over masaa mawili kwa gari,
ni aibu kubwa sana.
Tatizo letu sisi wa tz tunauoga kuongelea na kudai haki zetu.
Mafuta ya gari kidogo unayokuwanayo yanaisha kwenye foleni,
wakati wanaojiona wajanja waruka angani,bila matatizo.


 
MKUU

KWANI KUNA LAZIMA YA Kuja kulalama hapa.
nyie si ndio mnatawala. hayo si ndio maisha bora
na bado ungetumia masaa 8 ndio ungelewa vyema CCM imeshika hatamu
nadhani 2015 mtawaambia wadanganyika mtaanzisha safari za anga kutoka posta-tegeta,posta gogolamboto,posta kimara nk
Mkuu jaribu kuangalia vizuri namaanisha nini na nipo upande gani.
Tumia umaakini kuangalia,utanielewa zaidi.
Karibu
 
Azimio jipya,umenigusa HYPNOTIC ZOMBIE wao si tu wanaruka angani bali anapotaka kwenda mahali hapa dar njia hiyo inafagiliwa kwa hiyo adha halisi ya foleni haipati,na ndio maana leo wanatuzungusha kama pia, kunakuwa na tatizo la umeme halijaisha unaletewa tatizo la mafuta yote haya ni kwa sababu serikali kama kipofu anayepapasa papasa wala haijui njia mitafaruku kila leo,na bahati mbaya uelewa wa tz waliowengi O Ni wajanja tu wa kutafuta hela ya kula mengine anasema aaah hayo ya wakubwa. Huo ndio msiba mkubwa tulionao sijui tutoke vipi hapo.
 
Back
Top Bottom