Rosh Hashannah
JF-Expert Member
- Sep 13, 2017
- 3,415
- 2,042
(sehemu 1)
Kwa mada hii nilikuwa na vichwa vingi vya kumwaga. Kwa mfano, ningeliweza kuiita “WAAFRIKA HATUKO SAWA NA WENGINE” au “WAAFRIKA WAMOJA, HATUVAI MBILI.” Vichwa vyote hivyo vingeliweza kuwa muhtasari sahihi wa maudhui ya mada hii.
Ninasema kwa jinsi tunavyofikiri, kuamua na kutenda, sisi Waafrika hatuko sawa na wengine: Wamerikani, Wazungu na Waasia. Polepole sijatukana. Najieleza.
Sisi tunafikiri, kuamua na kutenda kitoto zaidi kuliko watu wa mabara mengine. Ndiyo maana linapokuja suala la IQ ya jamii sisi ni wa mwisho karibu ya mataahira. Huu ni ukweli wa kuudhi, lakini heri tuuanike hadharani huenda vizazi vijavyo vitaamka na kuwa tofauti na sisi. Hivyo ninaposema hatuko sawa na wanadamu wengine simaanishi masuala ya maumbile yetu, au kuzaa na kula. Katika haya tunaweza kusema tuko sawa.
Tusipo sawa ni pengine. Ni katika namna tunavyofikiri, kuamua na kutenda. Tunaona sasa hivi habari za makongamano. Siku hizi kuna hatua za kufanya makongamano kukabiliana na matatizo yetu.
Hapa tumepotea njia ya watu wazima. Badala yake tumeanza kwenda njia ya watoto wachanga.
Nisikilize vizuri. Sisi Afrika tunafanya makongamano ya aibu wakati wenzetu wanafanya makongamano ya haiba. Yaani makongamano yetu ni ya kutia haya ya uso, ya kijinga, ya kitoto, ya aibu, wakati wenzetu wanafanya ya kuweledi, ya kiutu uzima, ya haiba, yenye kuheshimisha. Ona! Sisi eti tunafanya makongamano tupeane akili ya Kinjikitile na kutoana mapepo tukimwomba Mungu atutoe kwenye roho za ujane, umaskini, na maradhi kama ukimwi, asthma, ukoma, presha, kisukari, kuota ndoto mbaya, kuwaona wachawi usiku na kadhalika.
Ndipo eti tunajikusanya watu wazima na watoto wetu tumwombe Mungu atuauni katika matatizo ya kukosa ajira, kukataliwa, kurogwa na watu, “kulaaniwa na wazee wetu”, kukosa ustawi, kupagawa na mapepo, kupandwa na majini (maruhani), kuota ndoto za ajabu, nyumba kutembelewa na bundi, vyumbani kuingia popo, kuchukiwa na majirani, kutopendwa, pesa kutokukaa, kukojoa kitandani, kuumwa na nyoka na kadhalika. mbona wenzetu hawalalamiki kuhusu haya? Kweli tunasikitisha mno na kwa haya tunatembea katika ujinga mkubwa.
Halafu? Dawa tunayoichukua katika makongamano hayo kutibu matatizo yetu eti ni kuanguka, kuweweseka, kulia, kusali kwa sauti ya juu, kufunga kavu, kukesha, kutoana mapepo, kukata miti ya ukoo inayotusababishia laana na kutiana moyo kwamba kwa jina la Yesu wa Nazareti wachawi hawatatuweza tena na tukilala hatuona tena maruweruwe.
Eti tunamtupia kazi Yesu, tukiita kwa kelele nyingi, “ Hakuna Mungu kama wewe!” “Hakuna Mungu kama wewe!” “Yesu anaweza!” “Yesu anaweza!” Ha, Mungu atusaidie katika utoto wetu? Yesu atusaidie katika mambo ya kipuuzi hayo? Ujinga mtupu!
Niwaambieni kitu? Ningelikuwa Mungu ningelivamia makongamano ya Waafrika na kuwatawanya kwa mateke ya matumboni na ngumi za usoni! Yesu “aliwafanyia hivyo” wabadili pesa na wauza njiwa na wanyama hekaluni. Hakika hapa naielewa hasira ya Yesu (Mk 11:15-19).
Sikilizeni Waafrika wenzangu. Tunafanya mambo kinyume na mategemeo ya Mungu mwema. Sawa na watu wengine, Mungu alitupa akili na utashi tuvitumie kutatulia matatizo yetu na yeye aje kubariki na kufanyia wepesi jitihada zetu tu (Zab 90:17). Usinibishe. Ndiyo kisa Mungu alituagiza tufanye kazi siku sita kati ya siku saba za juma. Sisi tunafanya kinyume chake, tunatumia siku sita kusali na kufanya mikutano na makongamano ya kijinga na kufanya kazi kwa shingo upande labda siku moja kwa juma. Hapo Mungu atusaidie kwa sababu gani? Tunafanya kinyume na alivyotupangia, tutampendezaje hata atujali? Sisi ni wa kupuuzwa tu, maana “hatunazo kichwani”.
Sasa sikiliza. Wakati sisi tunafanya makongamano hayo ya aibu, au ya kijinga katika majimbo yetu, parokia zetu na mitaa yetu, wenzetu Wamarekani, Wazungu na Waasia wanafanya makongamano ya haiba, ya kujipanga kiutu uzima, ya kiuchumi.
Nakukumbusheni. Tumesikia habari, kwa mfano, ya Kongamano la Kiuchumi la Singra-La, Kongomano la Kiuchumi la St. Petersburg, Kongamano la Kiuchumi la Qatar, Mkutano wa G7, Mkutano wa G20 na kadhalika.
Wenzetu wanajikusanya katika makongamono hayo wapange namna ya kufanya biashara kati ya nchi zao, makampuni yao yajulishane fursa za uwekezaji mitaji yao, jinsi ya kufanya biashara na nchi maskini za Afrika na Amareka ya Kusini, jinsi ya kutengeneza ajira kwa watu wao na jinsi ya mabilionea wao kuingia katika kushamirisha huduma za jamii kama elimu, afya na mahitaji kama umeme na gesi na mafuta.
Sasa hebu linganisha na makongamano ya kwetu. Ya wenzetu ni ya akili tupu, ubongo unatumika na suluhu zitakuwa zenye mapato ya kweli na ya kudumu. Kinyume chake, sisi tunaishia kudumazana na kulialia kama watoto wanywa uji wa chekechea. Je, hapo tupo sawa nao kweli? Mwogope Mungu, useme ukweli!
Sababu za Matatizo Yetu
Chanzo cha makongamano yetu ni ya aibu. Ni sababu za matatizo yetu tulizokosea. Eti sisi tumejiaminisha kwamba sababu ya matatizo yetu ni kurogwa, laana, mikosi, mapepo, majini na kadhalika. Jamani hizi ni sababu za kitoto, za kitaahira, za kujidumaza, za mtu kuwa chini ya viwango vya kuwa sura na mfano wa Mungu. Yaani ni sababu za chini ya mtu. Kinyume chetu ni wenzetu. Wenzetu huishi kwa utafiti na kujijali na kujihesabu kama wenye uwezo wa kufikiri na kufanya maamuzi hata magumu kabisa. Wenzetu wanajisikia kuwa “makamu wa Mungu” wakati sisi tunajiona kama hayawani fulani tu (Zab 8:3-8). Kutokana na kujitambua kwao, wenzetu wamekataa sababu za matatizo yao kuwa kurogwa, laana, mikosi, mapepo, majini na kadhalika. Katika kuyasoma mazingira na kutafiti wenzetu wameona sababu za matatizo yao ni pamoja na kutindikiwa rasilimali, mabadiliko ya tabia nchi, elimu isiyotosheleza mahitaji ya kisasa, teknolojia ndogo na magonjwa tandavu kama saratani na COVID -19. Kinyume chao, sisi ndiyo hizo sababu za kijinga.
Tunadai Tunajua hata Pasipo Utafiti
Kwa bahati mbaya, Waafrika hatufanyi utafiti kujua sababu halisi ya matatizo yetu isipokuwa tunarukia majawabu kumbakumba: kurogwa, laana, mikosi, mapepo, majini na kadhalika. Kwa huruma, hapo mwaka 2009, Baba Mtakatifu Benedikto XVI alitusaidia kutufahamisha moja ya sababu ya uduni wetu na akatupendekezea suluhu baada ya Sinodi II ya Afrika. Ajabu lakini, pamoja na msaada huo, hatutilii maanani alichosema na wengi sana wala hatuna habari na alituambia. Ni hivi, katika jukumu lake la kutuchunga hata Waafrika Baba Mtakatifu Benedikto XVI alituandikia akidokeza imani katika uchawi kati ya sababu zinazotudumaza akisema:
“Uchawi, ambao msingi wake ni dini za jadi, kwa hivi karibuni hutiwa tena nguvu. Woga wa zamani unaibuka tena na unatengeneza pingu poozeshi za kutojiamni. Wasiwasi kuhusu afya, ustawi, watoto, hali ya hewa, na kujikinga na pepo wabaya mara nyingine husababisha watu kukimbilia kwenye mazoezi fulani ya dini za jadi za Kiafrika ambayo hayapatani na mafundisho ya Kikristo. Tatizo la ‘kujisajili kuwili’ – kwenye Ukristo na kwenye dini za jadi za Kiafrika – linabaki ni changamoto. Kwa njia ya katekesi na utamadunisho wa kina, Kanisa huko Afrika linahitaji kuwasaidia watu kugundua ukamilifu wa tunu za Injili. Ni muhimu kuweka wazi maana ya kina ya mazoezi haya ya ushirikina kwa kuainisha mambo mengi ya kiteolojia, kijamii na kiuchungaji yanayohusu janga hili” (Africae Munus 93).
Mzigo wa Suluhu za Ovyo
Wataalamu wanasema, “Wrong diagnosis, wrong prescription”, yaani “Ubainishaji ugonjwa uliokosewa, utoaji dawa uliokosewa.” Tunavyong’ang’ania sisi ni suluhu za ovyo tu. Kwa kuwa tulishakosea sababu ya matatizo yetu, tunachong’ang’ania kama suluhu ni bure: eti kwenda kwa waganga wa kienyeji, kwenda kwa wachungji na manabii, kufanya makongamano ya Roho Mtakatifu, maombi kwa Mungu na kwenda kuomba nchi za nje.
Tunakwenda kwa waganga wa kienyeji watusaidie kupata mali, kupata ajira na kuponywa maradhi yetu. Wao, kama wajinga wenzetu, wanatupatia hirizi na kututoza mbuzi, kuku, ng’ombe na pesa taslimu. Wanatufilisi ndiyo maana sisi tunabaki pale pale. Hawajui chochote hao ndiyo maana hawana tofauti na sisi wenyewe. Sisi maskini na wagonjwa kama wao pia. Hayupo aliyempita mwenzake hasa, hali yetu moja tu.
Tukitoka kwa waganga wa kienyeji, tunakwenda kwa wachungaji, manabii na mitume watuombee. Tunaombewa kwa sauti za kupasua anga, tunapigwa mateke ya upako, tunanyweshwa maji waliyooga wao, tunanunulishwa chumvi za upako, maji ya upako, chupi za upako, kunyonywa matiti, “kujambiwa ushuzi” na kadhalika eti tupate utajiri na matatizo yetu yakome. Wajinga sisi!
Tukitoka hapo, kila mwaka tunatengeneza “Makongamano eti ya Roho Mtakatifu” eti tumwombe Mungu tupate ajira, majumba, pesa, visa za kwenda Marekani au Ulaya na kadhalika. Hapo napo tunafanyiana mambo ya kitoto kutoana pepo, kuwingana majini, kukata mizizi ya laana na kadhalika. Papo hapo tunamtania Mungu, tukisali, kufunga na kukesha, kukemea, kupayuka payuka na kadhalika. Jamani, haya tunayong’ang’ania ni mambo ya kitoto ndiyo kisa hayatutatulii lolote; maradhi yapo pale pale, kukosa ajira kuko pale pale, ufukara upo pale pale. Ndiyo kisa wagonjwa wetu wapo pale pale. Ukosefu wa ajira unaendelea. Umaskini unaendelea na kadhalika. Mkinibisha niambieni kwa takwimu tangu shughuli za makongamano ya Wapentekoste, Walokole na Karismatiki zianze ni ajira ngapi zilizopatikana nchini? Mbona maelfu wanatafuta ajira bado? Au tuseme, kwa mfano, je, Karismatiki wetu wote wana ajira? “Wanaowabomu” pesa watu si wao pia? Wagonjwa wangapi waliopona, Karismatiki wenyewe hawaumwi? Hivi hawapo pamoja nasi katika foleni za hospitalini? Viwete wangapi wanaotembea? Bubu wangapi wanaosema? Viziwi wangapi wanaosikia? Wakoma wangapi waliotakaswa? Wafu wangapi waliofufuliwa? Bila shaka hakuna. Kama wapo, ni wa kuwasingizia kwa usanii tu. Ni aibu! Ndiyo maana hata “wajanja na mabingwa wa miujiza” waliokuwa wanatudanganya wenzao kwamba wana uwezo wa kutufanyia miujiza wengine wamekufa, wamezikwa na wameoza makaburini mwao. Wenzao wala hawakuwaponya wasife na hata walipokufa hawakuwafufua. Je, niwataje kwa majina? Orodha yao ninayo hapa mezani pangu.
Kulia ndiyo kutia uchafu wa kunuka sebuleni kwetu Waafrika. Ni aibu kubwa. Wanaume wazima wanatumaini kulia kutatulia matatizo yetu! Akina mama wetu wazima wanatumaini kulia kutatulia matatizo yetu. Vijana wazima wanatumaini kulia kutatulia matatizo yetu. Ndipo basi watoto wetu watakuwa malofa hivyo hivyo maana mtoto wa kakakuona ni kakakuona. Hii ni aibu kubwa kabisa kwa bara letu. Hivi bara gani lingine duniani ambalo watu wazima wanalia ili kutatua matatizo yao, kama si Afrika peke yake? Hivi ni watu wa ngozi gani nyingine duniani ambao watu wazima wake wanalia ili kutatua matatizo yao kama si watu weusi na machotara wetu? Hivi watu gani wengine wanaomtwisha Mungu kazi ya kuwatunza na kuwalisha kama ndege kama si watu weusi na machotara wetu? Ndipo aibu hii ni ya hapa Afrika, Kusini mwa Sahara, na Amerika ya Kaskazini na Kusini walipo jamaa zetu weusi na vizalia vyetu. Ni aibu kweli kweli. Ndiyo maana wasiotutakia mema wanatuona sisi nusu masokwe au chimpanzee. Unadhani wanatuonea? Hapana. Tunayayoyatenda kwenye makongamano yetu ndiyo yanayotustahilisha kutukanwa huko. Hebu tuamkeni jamani!
Mzee wetu Pd. Titus Amigu
Kwa mada hii nilikuwa na vichwa vingi vya kumwaga. Kwa mfano, ningeliweza kuiita “WAAFRIKA HATUKO SAWA NA WENGINE” au “WAAFRIKA WAMOJA, HATUVAI MBILI.” Vichwa vyote hivyo vingeliweza kuwa muhtasari sahihi wa maudhui ya mada hii.
Ninasema kwa jinsi tunavyofikiri, kuamua na kutenda, sisi Waafrika hatuko sawa na wengine: Wamerikani, Wazungu na Waasia. Polepole sijatukana. Najieleza.
Sisi tunafikiri, kuamua na kutenda kitoto zaidi kuliko watu wa mabara mengine. Ndiyo maana linapokuja suala la IQ ya jamii sisi ni wa mwisho karibu ya mataahira. Huu ni ukweli wa kuudhi, lakini heri tuuanike hadharani huenda vizazi vijavyo vitaamka na kuwa tofauti na sisi. Hivyo ninaposema hatuko sawa na wanadamu wengine simaanishi masuala ya maumbile yetu, au kuzaa na kula. Katika haya tunaweza kusema tuko sawa.
Tusipo sawa ni pengine. Ni katika namna tunavyofikiri, kuamua na kutenda. Tunaona sasa hivi habari za makongamano. Siku hizi kuna hatua za kufanya makongamano kukabiliana na matatizo yetu.
Hapa tumepotea njia ya watu wazima. Badala yake tumeanza kwenda njia ya watoto wachanga.
Nisikilize vizuri. Sisi Afrika tunafanya makongamano ya aibu wakati wenzetu wanafanya makongamano ya haiba. Yaani makongamano yetu ni ya kutia haya ya uso, ya kijinga, ya kitoto, ya aibu, wakati wenzetu wanafanya ya kuweledi, ya kiutu uzima, ya haiba, yenye kuheshimisha. Ona! Sisi eti tunafanya makongamano tupeane akili ya Kinjikitile na kutoana mapepo tukimwomba Mungu atutoe kwenye roho za ujane, umaskini, na maradhi kama ukimwi, asthma, ukoma, presha, kisukari, kuota ndoto mbaya, kuwaona wachawi usiku na kadhalika.
Ndipo eti tunajikusanya watu wazima na watoto wetu tumwombe Mungu atuauni katika matatizo ya kukosa ajira, kukataliwa, kurogwa na watu, “kulaaniwa na wazee wetu”, kukosa ustawi, kupagawa na mapepo, kupandwa na majini (maruhani), kuota ndoto za ajabu, nyumba kutembelewa na bundi, vyumbani kuingia popo, kuchukiwa na majirani, kutopendwa, pesa kutokukaa, kukojoa kitandani, kuumwa na nyoka na kadhalika. mbona wenzetu hawalalamiki kuhusu haya? Kweli tunasikitisha mno na kwa haya tunatembea katika ujinga mkubwa.
Halafu? Dawa tunayoichukua katika makongamano hayo kutibu matatizo yetu eti ni kuanguka, kuweweseka, kulia, kusali kwa sauti ya juu, kufunga kavu, kukesha, kutoana mapepo, kukata miti ya ukoo inayotusababishia laana na kutiana moyo kwamba kwa jina la Yesu wa Nazareti wachawi hawatatuweza tena na tukilala hatuona tena maruweruwe.
Eti tunamtupia kazi Yesu, tukiita kwa kelele nyingi, “ Hakuna Mungu kama wewe!” “Hakuna Mungu kama wewe!” “Yesu anaweza!” “Yesu anaweza!” Ha, Mungu atusaidie katika utoto wetu? Yesu atusaidie katika mambo ya kipuuzi hayo? Ujinga mtupu!
Niwaambieni kitu? Ningelikuwa Mungu ningelivamia makongamano ya Waafrika na kuwatawanya kwa mateke ya matumboni na ngumi za usoni! Yesu “aliwafanyia hivyo” wabadili pesa na wauza njiwa na wanyama hekaluni. Hakika hapa naielewa hasira ya Yesu (Mk 11:15-19).
Sikilizeni Waafrika wenzangu. Tunafanya mambo kinyume na mategemeo ya Mungu mwema. Sawa na watu wengine, Mungu alitupa akili na utashi tuvitumie kutatulia matatizo yetu na yeye aje kubariki na kufanyia wepesi jitihada zetu tu (Zab 90:17). Usinibishe. Ndiyo kisa Mungu alituagiza tufanye kazi siku sita kati ya siku saba za juma. Sisi tunafanya kinyume chake, tunatumia siku sita kusali na kufanya mikutano na makongamano ya kijinga na kufanya kazi kwa shingo upande labda siku moja kwa juma. Hapo Mungu atusaidie kwa sababu gani? Tunafanya kinyume na alivyotupangia, tutampendezaje hata atujali? Sisi ni wa kupuuzwa tu, maana “hatunazo kichwani”.
Sasa sikiliza. Wakati sisi tunafanya makongamano hayo ya aibu, au ya kijinga katika majimbo yetu, parokia zetu na mitaa yetu, wenzetu Wamarekani, Wazungu na Waasia wanafanya makongamano ya haiba, ya kujipanga kiutu uzima, ya kiuchumi.
Nakukumbusheni. Tumesikia habari, kwa mfano, ya Kongamano la Kiuchumi la Singra-La, Kongomano la Kiuchumi la St. Petersburg, Kongamano la Kiuchumi la Qatar, Mkutano wa G7, Mkutano wa G20 na kadhalika.
Wenzetu wanajikusanya katika makongamono hayo wapange namna ya kufanya biashara kati ya nchi zao, makampuni yao yajulishane fursa za uwekezaji mitaji yao, jinsi ya kufanya biashara na nchi maskini za Afrika na Amareka ya Kusini, jinsi ya kutengeneza ajira kwa watu wao na jinsi ya mabilionea wao kuingia katika kushamirisha huduma za jamii kama elimu, afya na mahitaji kama umeme na gesi na mafuta.
Sasa hebu linganisha na makongamano ya kwetu. Ya wenzetu ni ya akili tupu, ubongo unatumika na suluhu zitakuwa zenye mapato ya kweli na ya kudumu. Kinyume chake, sisi tunaishia kudumazana na kulialia kama watoto wanywa uji wa chekechea. Je, hapo tupo sawa nao kweli? Mwogope Mungu, useme ukweli!
Sababu za Matatizo Yetu
Chanzo cha makongamano yetu ni ya aibu. Ni sababu za matatizo yetu tulizokosea. Eti sisi tumejiaminisha kwamba sababu ya matatizo yetu ni kurogwa, laana, mikosi, mapepo, majini na kadhalika. Jamani hizi ni sababu za kitoto, za kitaahira, za kujidumaza, za mtu kuwa chini ya viwango vya kuwa sura na mfano wa Mungu. Yaani ni sababu za chini ya mtu. Kinyume chetu ni wenzetu. Wenzetu huishi kwa utafiti na kujijali na kujihesabu kama wenye uwezo wa kufikiri na kufanya maamuzi hata magumu kabisa. Wenzetu wanajisikia kuwa “makamu wa Mungu” wakati sisi tunajiona kama hayawani fulani tu (Zab 8:3-8). Kutokana na kujitambua kwao, wenzetu wamekataa sababu za matatizo yao kuwa kurogwa, laana, mikosi, mapepo, majini na kadhalika. Katika kuyasoma mazingira na kutafiti wenzetu wameona sababu za matatizo yao ni pamoja na kutindikiwa rasilimali, mabadiliko ya tabia nchi, elimu isiyotosheleza mahitaji ya kisasa, teknolojia ndogo na magonjwa tandavu kama saratani na COVID -19. Kinyume chao, sisi ndiyo hizo sababu za kijinga.
Tunadai Tunajua hata Pasipo Utafiti
Kwa bahati mbaya, Waafrika hatufanyi utafiti kujua sababu halisi ya matatizo yetu isipokuwa tunarukia majawabu kumbakumba: kurogwa, laana, mikosi, mapepo, majini na kadhalika. Kwa huruma, hapo mwaka 2009, Baba Mtakatifu Benedikto XVI alitusaidia kutufahamisha moja ya sababu ya uduni wetu na akatupendekezea suluhu baada ya Sinodi II ya Afrika. Ajabu lakini, pamoja na msaada huo, hatutilii maanani alichosema na wengi sana wala hatuna habari na alituambia. Ni hivi, katika jukumu lake la kutuchunga hata Waafrika Baba Mtakatifu Benedikto XVI alituandikia akidokeza imani katika uchawi kati ya sababu zinazotudumaza akisema:
“Uchawi, ambao msingi wake ni dini za jadi, kwa hivi karibuni hutiwa tena nguvu. Woga wa zamani unaibuka tena na unatengeneza pingu poozeshi za kutojiamni. Wasiwasi kuhusu afya, ustawi, watoto, hali ya hewa, na kujikinga na pepo wabaya mara nyingine husababisha watu kukimbilia kwenye mazoezi fulani ya dini za jadi za Kiafrika ambayo hayapatani na mafundisho ya Kikristo. Tatizo la ‘kujisajili kuwili’ – kwenye Ukristo na kwenye dini za jadi za Kiafrika – linabaki ni changamoto. Kwa njia ya katekesi na utamadunisho wa kina, Kanisa huko Afrika linahitaji kuwasaidia watu kugundua ukamilifu wa tunu za Injili. Ni muhimu kuweka wazi maana ya kina ya mazoezi haya ya ushirikina kwa kuainisha mambo mengi ya kiteolojia, kijamii na kiuchungaji yanayohusu janga hili” (Africae Munus 93).
Mzigo wa Suluhu za Ovyo
Wataalamu wanasema, “Wrong diagnosis, wrong prescription”, yaani “Ubainishaji ugonjwa uliokosewa, utoaji dawa uliokosewa.” Tunavyong’ang’ania sisi ni suluhu za ovyo tu. Kwa kuwa tulishakosea sababu ya matatizo yetu, tunachong’ang’ania kama suluhu ni bure: eti kwenda kwa waganga wa kienyeji, kwenda kwa wachungji na manabii, kufanya makongamano ya Roho Mtakatifu, maombi kwa Mungu na kwenda kuomba nchi za nje.
Tunakwenda kwa waganga wa kienyeji watusaidie kupata mali, kupata ajira na kuponywa maradhi yetu. Wao, kama wajinga wenzetu, wanatupatia hirizi na kututoza mbuzi, kuku, ng’ombe na pesa taslimu. Wanatufilisi ndiyo maana sisi tunabaki pale pale. Hawajui chochote hao ndiyo maana hawana tofauti na sisi wenyewe. Sisi maskini na wagonjwa kama wao pia. Hayupo aliyempita mwenzake hasa, hali yetu moja tu.
Tukitoka kwa waganga wa kienyeji, tunakwenda kwa wachungaji, manabii na mitume watuombee. Tunaombewa kwa sauti za kupasua anga, tunapigwa mateke ya upako, tunanyweshwa maji waliyooga wao, tunanunulishwa chumvi za upako, maji ya upako, chupi za upako, kunyonywa matiti, “kujambiwa ushuzi” na kadhalika eti tupate utajiri na matatizo yetu yakome. Wajinga sisi!
Tukitoka hapo, kila mwaka tunatengeneza “Makongamano eti ya Roho Mtakatifu” eti tumwombe Mungu tupate ajira, majumba, pesa, visa za kwenda Marekani au Ulaya na kadhalika. Hapo napo tunafanyiana mambo ya kitoto kutoana pepo, kuwingana majini, kukata mizizi ya laana na kadhalika. Papo hapo tunamtania Mungu, tukisali, kufunga na kukesha, kukemea, kupayuka payuka na kadhalika. Jamani, haya tunayong’ang’ania ni mambo ya kitoto ndiyo kisa hayatutatulii lolote; maradhi yapo pale pale, kukosa ajira kuko pale pale, ufukara upo pale pale. Ndiyo kisa wagonjwa wetu wapo pale pale. Ukosefu wa ajira unaendelea. Umaskini unaendelea na kadhalika. Mkinibisha niambieni kwa takwimu tangu shughuli za makongamano ya Wapentekoste, Walokole na Karismatiki zianze ni ajira ngapi zilizopatikana nchini? Mbona maelfu wanatafuta ajira bado? Au tuseme, kwa mfano, je, Karismatiki wetu wote wana ajira? “Wanaowabomu” pesa watu si wao pia? Wagonjwa wangapi waliopona, Karismatiki wenyewe hawaumwi? Hivi hawapo pamoja nasi katika foleni za hospitalini? Viwete wangapi wanaotembea? Bubu wangapi wanaosema? Viziwi wangapi wanaosikia? Wakoma wangapi waliotakaswa? Wafu wangapi waliofufuliwa? Bila shaka hakuna. Kama wapo, ni wa kuwasingizia kwa usanii tu. Ni aibu! Ndiyo maana hata “wajanja na mabingwa wa miujiza” waliokuwa wanatudanganya wenzao kwamba wana uwezo wa kutufanyia miujiza wengine wamekufa, wamezikwa na wameoza makaburini mwao. Wenzao wala hawakuwaponya wasife na hata walipokufa hawakuwafufua. Je, niwataje kwa majina? Orodha yao ninayo hapa mezani pangu.
Kulia ndiyo kutia uchafu wa kunuka sebuleni kwetu Waafrika. Ni aibu kubwa. Wanaume wazima wanatumaini kulia kutatulia matatizo yetu! Akina mama wetu wazima wanatumaini kulia kutatulia matatizo yetu. Vijana wazima wanatumaini kulia kutatulia matatizo yetu. Ndipo basi watoto wetu watakuwa malofa hivyo hivyo maana mtoto wa kakakuona ni kakakuona. Hii ni aibu kubwa kabisa kwa bara letu. Hivi bara gani lingine duniani ambalo watu wazima wanalia ili kutatua matatizo yao, kama si Afrika peke yake? Hivi ni watu wa ngozi gani nyingine duniani ambao watu wazima wake wanalia ili kutatua matatizo yao kama si watu weusi na machotara wetu? Hivi watu gani wengine wanaomtwisha Mungu kazi ya kuwatunza na kuwalisha kama ndege kama si watu weusi na machotara wetu? Ndipo aibu hii ni ya hapa Afrika, Kusini mwa Sahara, na Amerika ya Kaskazini na Kusini walipo jamaa zetu weusi na vizalia vyetu. Ni aibu kweli kweli. Ndiyo maana wasiotutakia mema wanatuona sisi nusu masokwe au chimpanzee. Unadhani wanatuonea? Hapana. Tunayayoyatenda kwenye makongamano yetu ndiyo yanayotustahilisha kutukanwa huko. Hebu tuamkeni jamani!
Mzee wetu Pd. Titus Amigu