TUNTEMEKE
JF-Expert Member
- Jun 15, 2009
- 4,587
- 579
Katika kuhakikisha anapambana na kufunika hoja ya wanachama wanaotaka James Mbatia ajieleze kuhusu kukidhoofisha chama na kuwa kibaraka wa CCM tayari Mbatia amemvua Kafulila Ukatibu mwenezi wa NCCR Taifa na Mwenyekiti wa kina Mama Taifa, Bi Amina pia kavuliwa waadhifa huo.
Kwakuwa Mbatia anaona Kafulila na wenzake 28 waliosaini waraka wa kutaka ajieleze na apigiwe kura za kutokuwa na imani nae ndipo amechukua jitihada za kuwapunguza wanaoweza kupunguzika, hivyo kwa sasa wamebaki 26, anapanga kupunguza wengine wanne ili apate idadi anayoweza kuishinda, wajumbe hao ni wale wanaoteuliwa na Mwenyekiti ili kuwa wajumbe katika halmashauri kuu..
tayari kikao cha halmashauri kuu kimeitishwa jumamosi ijayo huku wajumbe wasiomtaka wakiwa hawajajulishwa ili wasihudhurie na hatimaye amvue Kafulila uanachama ili kujilinda, anaona hiyo ndio njia pekee maana hana namna nyingine ya kujinusuru, na baada ya kujibu hoja ameanza kufukuza wauliza hoja kwani hana majibu kwa mujibu wa waraka na ushahidi uliotolewa.
Kwakuwa Mbatia anaona Kafulila na wenzake 28 waliosaini waraka wa kutaka ajieleze na apigiwe kura za kutokuwa na imani nae ndipo amechukua jitihada za kuwapunguza wanaoweza kupunguzika, hivyo kwa sasa wamebaki 26, anapanga kupunguza wengine wanne ili apate idadi anayoweza kuishinda, wajumbe hao ni wale wanaoteuliwa na Mwenyekiti ili kuwa wajumbe katika halmashauri kuu..
tayari kikao cha halmashauri kuu kimeitishwa jumamosi ijayo huku wajumbe wasiomtaka wakiwa hawajajulishwa ili wasihudhurie na hatimaye amvue Kafulila uanachama ili kujilinda, anaona hiyo ndio njia pekee maana hana namna nyingine ya kujinusuru, na baada ya kujibu hoja ameanza kufukuza wauliza hoja kwani hana majibu kwa mujibu wa waraka na ushahidi uliotolewa.