sifongo
JF-Expert Member
- Jun 5, 2011
- 4,896
- 5,302
Habari wanajamvi na wapenzi wa filamu, nina nia ya kutengeneza filamu ya kipelelezi ila kuna vitu nahitaji kuvijua hasa vitengo vya usalama ndani Serikali, mfano ninajua kwamba kuna kitengo kinahusika na ufuatiliaji wa pesa haramu nadhani kipo BOT au WIZARA YA FEDHA kwa anayefahamu anisaidie na jina lake pia, na katika vikosi vya usalama wa Taifa nafahamu TISS peke yake, na je ndani ya TISS kuna vitengo vingine au la? Na kutokana na ugumu wa kupata mavazi ya polisi hapa Nchini katika moja ya Scene zangu kuna sehemu mauaji yametokea na nia yangu ni kufanya watu wa usalama wa Taifa (ambao sijajua ni Division gani) wanaiwahi ile maiti na kutaka polisi wasijue kitu kama vile wafanyavyo CIA, MI6 na vikosi vingine vya kijasusi kwenye Movie au Novel za mbele sasa tatizo langu sijajua je vikosi kama hivyo vipo hapa Nchini na je vinafanya kazi chini ya order kutoka mamlaka gani?
Kingine ni jina la kitengo cha kuzuia dawa za kulevya ndani ya jeshi la polisi (sio tume).
Natanguliza shukrani zangu na mwenye kufahamu anisaidie hayo, na baada ya kukamilisha story na kupanga script naahidi kuiweka hapa baadhi ya Scene wadau mnisaidie tuweze kuisogeza tasnia ya filamu Nchini.
Kingine ni jina la kitengo cha kuzuia dawa za kulevya ndani ya jeshi la polisi (sio tume).
Natanguliza shukrani zangu na mwenye kufahamu anisaidie hayo, na baada ya kukamilisha story na kupanga script naahidi kuiweka hapa baadhi ya Scene wadau mnisaidie tuweze kuisogeza tasnia ya filamu Nchini.