Nataka kubadilisha kioo display ya simu ya samsung A30

mtume wawatu

JF-Expert Member
Oct 30, 2016
1,000
1,080
Ndugu zangu habari za muda huu?

Naomba niende moja kwa moja kweenye mada. simu yangu ya sammsung a30 imeanguka na kuharibika kioo yaani display.

Kwa sasa simu imevujia wino na kioo ni cheusi hakioneshi kitu. hivyo, nalazimika kutaka kuibadili display ili simu yangu ipate kurudi katika ubora wake.

Naomba kupata msaada wa wapi ninaweza kubadili hii display na gharama zake kwa hapa dar es salaam.

Nitashukuru kwa msaada wenu.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
ndugu zangu habari za muda huu? naomba niende moja kwa moja kweenye mada. simu yangu ya sammsung...
Nenda kkoo, aggrey mafundi kibao.

Garama inategemea watakuangaliaje tu ila inaweza range 20 hadi 40 hapo.

Ama tena nenda machinga complex kule.

Ila ujue wanaweka cha kichina. Vinakuwa kama vina kimpauko kwa mbali screen haiwi dark kama kioo original.

Samsung OG ni zaidi ya 70k hadi 100k na kama unataka OG inakulazimu kwenda duka la samsung.
 
Nenda kkoo, aggrey mafundi kibao. Garama inategemea watakuangaliaje tu ila inaweza range 20 hadi 40 hapo. Ama tena nenda machinga complex kule.

Ila ujue wanaweka cha kichina. Vinakuwa kama vina kimpauko kwa mbali screen haiwi dark kama kioo original.

Samsung OG ni zaidi ya 70k hadi 100k na kama unataka OG inakulazimu kwenda duka la samsung.
Hata za kichina hawezi pata kwa 20 au 40 mkuu Samsung sio sawa na techno
 
Mmoja huyu hapa

 
Hata za kichina hawezi pata kwa 20 au 40 mkuu Samsung sio sawa na techno
Hii unaona hapo nimeshabadilisha mara tatu, ya kwanza jamaa alikula 40, ya pili akala 30 ya tatu akala 20. Imepasuka tena nimeamua kuwaachia watoto wahangaike nayo.

Niliipataga kama bahati inakaa na charge sana (simu unaiwasha hotspot siku nzima na ikifika jioni inasoma 65% kama muujiza vile) na ipo faster mno ila kioo chake hakinaga bahati ya kudumu.
20230320_194829.jpg
 
A30 ni Amoles tena Full HD kioo bei yake itakua hela ndefu, pengine ikafika laki 2 hadi 3 Genuine.

Otherwise zipo lcd ambazo watu wanachakachua around 30k, unaweza cheki Aliexpress ama Kkoo.
 
A30 ni A305 hii ni A30s A307 simu mbili tofauti. Pia waweza ukawekewa bei kubwa wakakupiga vile vile, Amoled mpaka uitest mwenyewe
Nina swali nje ya mada kama betri 4000mAmp imekufa, je nikitaka kubadilisha battery naweza weka battery ya 5000mAmp kwenye simu hiyo hiyo?
 
Nina swali nje ya mada kama betri 4000mAmp imekufa, je nikitaka kubadilisha battery naweza weka battery ya 5000mAmp kwenye simu hiyo hiyo?
Unaweza ila nyingi feki so zina heat ila ukipata original inakaa poa japo inachukua muda zaid kuicharge mpaka ijae. Pia watengeneza simu wengi hawashauri kufanya jambo hilo.
 
Nina swali nje ya mada kama betri 4000mAmp imekufa, je nikitaka kubadilisha battery naweza weka battery ya 5000mAmp kwenye simu hiyo hiyo?
Unaweza ila sio simu zote. Pia zipo battery fake wanaweza kukuambia 5000mah kumbe uhalisia ni 3000mah ikawa ukaaji chaji mbaya kuliko 4000mah ya mwanzo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom