Natafuta kazi yoyote ya kupata angalau 15,000/= Tsh per day

Kuna wale rafiki zangu hawachagui Kazi hawana Mishe yoyote ukiwapa direction wapi Kazi ilipo wanakwenda kufanya mladi Tu iwe ya Halali

Nna ujumbe wenu hapa

Kama uko dar fika mpaka Gongo la mboto mwisho opposite na chuo cha Kampala ukifika hapo uliza mtu akuelekeze kilipo kiwanda kinaitwa NAMELA

Hiki ni kiwanda cha nguo ndio hatua ya Kwanza kabisa ya uandaaji nguo kama mashuka..khanga..vitenge maduvet n.k ufanyika na Kisha baada ya hapo mzigo upelekwa NIDA pale bara bara ya Mandera kwa ajili ya ukamilishaji kuwa nguo kamili

Kwaiyo kijana yoyoye aliepo around Gongo la mboto Majohe au maeneo anayoweza kufika hapo NAMELA naomba kuanzia kesho asubuhi avae vizuri kwa heshima aweke nywele zake smart ata ukisimama mbele za watu unaonekana mwenye tabia njema sio unaenda kuomba Kazi umevaa modo uko nusu uchi au umenyoa viduku na unanuka sigara

Ukifika getini muulizie mtu mmoja anaitwa chifu na umwambie umekuja kuomba Kazi yoyote atakae taja jina Hili pale getini huyu mtu atajua Moja kwa Moja umetoka Kwangu so utapewa maelekezo kwa haraka

Kumbuka kubeba kitambulisho cha kupigia Kura au namba ya Nida

Cha kuzingatia unadhifu wako maana mwingine akifika getini anaambiwa hakuna kazi kutokana na alivyokwenda kumbuka kupendeza unapokwenda kuomba Kazi maana wewe ni masikini tuu sio kichaa
Samahani mkuu,huu mchongo bado upo?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom