niachiemimi
JF-Expert Member
- Feb 18, 2015
- 3,497
- 4,924
Samahani mkuu. Unamaanisha lile jani la aloe vera nilikate kisha yale maji yake yanayotoka kwenye jani ndio nitumie kupigia mswaki kila asubuhi na jioni?.Nyongeza:
Epuka soda zote na pipi, au biskuits, achana na dawa za kisasa, tumia aloe vera gel ya kukamua mwenyewe, tena tafuta miche yake uoteshe hapo kwako hata kwenye makopo kama maua, ili uwe unatumia kama dawa ya meno.
Mimi nimetumia dawa nyingi za meno, kuanzia colgate original, sensodyne aina zote, Al to Killer lakini tatizo limeendelea,
Nimeshang'oa mawili na kuziba meno kadhaa lakini naona yanaendelea kupukutika Hadi nikaamua nihame kwenda asili. Sasa yametulia baada ya kuanza kufuata kanuni za afya, kwa kuwa ninapoishi ni karibu na porini natumia aloe vera original toka porini napiga asubuhi na jioni, yaani fresh, upukutikaji na sensitivity ya meno imeisha au kupungua.
Pole sana, fuata principle tu za afya, meno yetu tunayaharibu wenyewe kwa vyakula, vinywaji na dawa za neno za kisasa.
Jiulize kwa nini matangazo ya dawa za meno yanavyoongezeka na magonjwa ya meno yanazidi?
Hizi dawa hazitibu meno zaidi ya ku brush hard layer ya jino na kuifikia enamel.
Nawashauri wale ambao hamjaanza kupata matatizo ya meno kuchukua pre caution mapema. Mimi nilijiona nina meno magumu nikawa najilia na kujinywea hovyo hadi tatizo likaniingia.
Sirudii tena narudi kwa vitu vya asili tu.