Gift mzalendo
JF-Expert Member
- Dec 13, 2019
- 1,147
- 1,339
Habari wakuu
Nikiri Mimi ni muumini wa demokrasia ya vyama vingi na siasa za hoja za ushindani kwani naamini ushindani wowote huletea wananchi maendeleo
Ni moja ya watu tunatamani kuona tunakuwa na vyama vya siasa imara vinavyoweza kubadilishana madaraka Kila wakati pale kilichopo kinaposhindwa kufikia matarajio ya wananchi
Pia nikiri wananchi wanatamani Sana mabadiliko kwenye maeneo mengi hata ikibidi chama kilichopo kiwekwe pembeni kwanza na waone
Lakini Naomba niandike kwa masikitiko makubwa kwamba Mfumo wa Chama kikuu Cha upinzani Chadema Hauna uwezo wa kubeba uongozi wa nchi na taifa kwa ujumla
Yako madhaifu mengi kwenye mfumo wa Chadema, Kwa Leo aomba nielezee udhaifu wa chadema kwenye
Demokrasia ya NDANI
Chadema inaonyesha udhaifu mkubwa haswa kwenye nafasi ya juu ya chama
MFumo wa Chadema unaruhusu nafasi ya juu ya uongozi, MTU mmoja kuweza kugombea mara nyingi atakavyo hata maisha
Hii inaonyesha hata wakipewa nchi wanaweza wakabadili Mfumo wa nchi kuwa hivyo na Pengine kuwa madikteta haswa,
maana kile wanachofanya Sasa ndo picha ya kile watachofanya wakipewa serikali
Pia hapa tuona tatizo kubwa lingine la Chadema kutegemea MTU badala ya Mfumo na Hili ni hatari Sana Kama tulivyoona kwa awamu Fulani waliacha kuimarisha Mifumo wakategemea Mtu ,
Nafikiri tuliona hatari yake pale yule mtu anapoondoka pasipo kutarajiwa
lazima Chadema kabla ya kupewa Serikali washughulikie hili.
Mbaya zaidi hili tatizo liko Hadi kwenye viongozi waandamizi wa juu kabisa wa Cdm kuamini MTU mmoja
Kwamba MTU Fulani akishachukua fomu ya nafasi Fulani Basi mwingine anakiri kutokuchukua hiyo fomu
Alafu mnataka mpewe nchi Muongoze kidemokrasia kweli
Pili Mfumo wa Chadema umeonyesha udhaifu mkubwa wa kubeba watu smart au maarufu wanajiunga na chama chao
Hiii inaweza kuchangiwa pia na udhaifu wa demokrasia ya Ndani
Tatu ni Mfumo wa Chadema kushindwa kubeba au kuhandle watu wenye mawazo tofauti na wale wanaokihama chama hicho
Neno usaliti limetumika kuwa kashifu na kuwatuhumu wale wanatofautiana na baadhi ya viongozi wa chama hicho au msimamo bila kujali hoja zao
Kama kuhama chama kwa kutofoutiana hoja au msimamo ni usaliti kwa chadema
Inakuwaje wanawapokea waliohama chama lingine kwa hoja zile zile na wengine wanakuja kwa kutaka kugombea tu nafasi Tena za Cdm
Je Cdm ikipewa serikali Leo itawachukuliaje wale wanaotofautiana na serikali yao ?
Kama watawachukulia Kama wasaliti Kama wanavyofanya kwa sasa
je wapinzani wao watakuwa salama ?
Hayo ni machache kwa Leo kwenye mfumo wa Chadema
Naamini bado Wana nafasi ya kufanya madabiliko ya mfumo wao kuweza kubeba dhamana ya juu zaidi katika nchi yetu na sio tu kuwa chama kikuu Cha upinzani
Wao ndo wataamua ni muda Gani kwa haraka au miaka kumi na 15 nayoiona mimi baada ya kuingiza uongozi wenye fikra mpya au waliopo wakubali madhaifu wabadilishe
Hakuna Haja ya kubomoa nyumba ya nyasi Kama huna uhakika wa kujenga au kupata nyumba Bora zaidi ya tofali na mabati au zaidi ya hapo
Nikiri Mimi ni muumini wa demokrasia ya vyama vingi na siasa za hoja za ushindani kwani naamini ushindani wowote huletea wananchi maendeleo
Ni moja ya watu tunatamani kuona tunakuwa na vyama vya siasa imara vinavyoweza kubadilishana madaraka Kila wakati pale kilichopo kinaposhindwa kufikia matarajio ya wananchi
Pia nikiri wananchi wanatamani Sana mabadiliko kwenye maeneo mengi hata ikibidi chama kilichopo kiwekwe pembeni kwanza na waone
Lakini Naomba niandike kwa masikitiko makubwa kwamba Mfumo wa Chama kikuu Cha upinzani Chadema Hauna uwezo wa kubeba uongozi wa nchi na taifa kwa ujumla
Yako madhaifu mengi kwenye mfumo wa Chadema, Kwa Leo aomba nielezee udhaifu wa chadema kwenye
Demokrasia ya NDANI
Chadema inaonyesha udhaifu mkubwa haswa kwenye nafasi ya juu ya chama
MFumo wa Chadema unaruhusu nafasi ya juu ya uongozi, MTU mmoja kuweza kugombea mara nyingi atakavyo hata maisha
Hii inaonyesha hata wakipewa nchi wanaweza wakabadili Mfumo wa nchi kuwa hivyo na Pengine kuwa madikteta haswa,
maana kile wanachofanya Sasa ndo picha ya kile watachofanya wakipewa serikali
Pia hapa tuona tatizo kubwa lingine la Chadema kutegemea MTU badala ya Mfumo na Hili ni hatari Sana Kama tulivyoona kwa awamu Fulani waliacha kuimarisha Mifumo wakategemea Mtu ,
Nafikiri tuliona hatari yake pale yule mtu anapoondoka pasipo kutarajiwa
lazima Chadema kabla ya kupewa Serikali washughulikie hili.
Mbaya zaidi hili tatizo liko Hadi kwenye viongozi waandamizi wa juu kabisa wa Cdm kuamini MTU mmoja
Kwamba MTU Fulani akishachukua fomu ya nafasi Fulani Basi mwingine anakiri kutokuchukua hiyo fomu
Alafu mnataka mpewe nchi Muongoze kidemokrasia kweli
Pili Mfumo wa Chadema umeonyesha udhaifu mkubwa wa kubeba watu smart au maarufu wanajiunga na chama chao
Hiii inaweza kuchangiwa pia na udhaifu wa demokrasia ya Ndani
Tatu ni Mfumo wa Chadema kushindwa kubeba au kuhandle watu wenye mawazo tofauti na wale wanaokihama chama hicho
Neno usaliti limetumika kuwa kashifu na kuwatuhumu wale wanatofautiana na baadhi ya viongozi wa chama hicho au msimamo bila kujali hoja zao
Kama kuhama chama kwa kutofoutiana hoja au msimamo ni usaliti kwa chadema
Inakuwaje wanawapokea waliohama chama lingine kwa hoja zile zile na wengine wanakuja kwa kutaka kugombea tu nafasi Tena za Cdm
Je Cdm ikipewa serikali Leo itawachukuliaje wale wanaotofautiana na serikali yao ?
Kama watawachukulia Kama wasaliti Kama wanavyofanya kwa sasa
je wapinzani wao watakuwa salama ?
Hayo ni machache kwa Leo kwenye mfumo wa Chadema
Naamini bado Wana nafasi ya kufanya madabiliko ya mfumo wao kuweza kubeba dhamana ya juu zaidi katika nchi yetu na sio tu kuwa chama kikuu Cha upinzani
Wao ndo wataamua ni muda Gani kwa haraka au miaka kumi na 15 nayoiona mimi baada ya kuingiza uongozi wenye fikra mpya au waliopo wakubali madhaifu wabadilishe
Hakuna Haja ya kubomoa nyumba ya nyasi Kama huna uhakika wa kujenga au kupata nyumba Bora zaidi ya tofali na mabati au zaidi ya hapo