binti ashura
Senior Member
- Jan 14, 2011
- 118
- 19
Ndugu zangu mie ni ni mfanyakazi kama siyo kibarua, nalipwa 500,000 kwa mwezi lakini kila nikijitahidi kupanga bajeti nashindwa. Najikuta nikipewa mshahara tarehe 24 kufika tarehe 10 ya mwezi unaofuata ni shughuri nzito. Mie sinywi pombe, sivuti sigara, kwa sasa nimeacha na soda lakini bado hali si shwari.
Nina mpango wa kuacha chai ingawa sijui kama itasaidia, najikuta siku zinapopita madeni yanaongezeka mpaka imefikia kiasi cha kukopa kwa watu wapya ili niwalipe wale walionikopesha mwanzo.
Naomba msaada wa mawazo.
Nina mpango wa kuacha chai ingawa sijui kama itasaidia, najikuta siku zinapopita madeni yanaongezeka mpaka imefikia kiasi cha kukopa kwa watu wapya ili niwalipe wale walionikopesha mwanzo.
Naomba msaada wa mawazo.