Napinga Kiswahili kutumika kama lugha ya kufundishia

Naomba unijibu swali hili: kwa nini karibu nchi zote zilizoendelea kuna kozi elimu ya juu zinafundishwa kwa kiingereza? Majuzi chuo kikuu kikongwe kabisa mjini Milan Italia kimeamua kufundisha kozi zake zote kwa Kiingereza, unadhani ni kasumba?

Acha utumwa wa kifikra sio kila kinachofanywa na watu wa Italia au taifa lolote kubwa duniani kiko sahihi kuigwa, kumbuka formula na nadharia nyingi za masomo ziligunduliwa na Wagiriki pamoja na Warumi sasa kama English people waliweza kuzitranslate kwenda kwenye lugha zao kwann sisi tusiweze kuzileta kwny kisw??.. Enzi utamaduni wako kwa manufaa yako na ya vizazi vijavyo.. Mbona Wachina kwa kiasi kikubwa wameweza!
 
Tumepambana hasi Kiswahili kimekuwa miongoni mwa Lugha rasmi katika EAC na AU, sioni kama tutashindwa kukifanya kiswahili kuwa Lugha ya kufundishia. Pia kumbuka hakuna Taifa lililo pata maendeleo ya juu kwa kutumia lugha ya kigeni.
 
Mkuu inawezekana hoja yako ni ya msingi, lakini unaijenga vibaya. Kuna ubaya gani kutumia kiswahili kama lugha ya kufundishia? Unatakiwa kujua kuwa lugha sio lengo, lugha ni njia ya kufikia malengo.

Lakini pia unatakiwa ujue kuwa kuna tatizo kwenye kufikia lengo. Ukiangalia kiwango cha kiswahili cha watanzania wengi kiko chini sana hata huwezi kuamini. angalia hata hapa JF, jinsi watu wanavyojaribu kutumia kiswahili, kuna makosa kwenye sarufi, herufi na hata mantiki yote sifuri. FaizaFoxy huwa anajitahidi kuwarekebisha watu.

Lakini vilevile hatuwezi kuiga nchi nyingine kwa kuwa kila nchi ina mazingira yake. Huwezi kuiga Rwanda kwa sababu Kagame na wenzake hawajui kifaransa wamechagua Kiingereza, sisi ni Tanzania tuna Kiswahili na Kiingereza, vyote tunaudhaifu. lakini udhaifu upo hata kwenye lugha za kikabila. Kwa hiyo tatizo ni kubwa kuliko unavyodhani.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom