...Ametoa neno kwenye kanisa la ufufuo na uzima leo kuhusu rushwa na kusema kuwa viongozi wamekosa huruma kwa wananchi na wamekosa Mungu ndani yao.Amedai yeye sio mgeni kwenye kanisa hili la Gwajima na ameonyeshwa kukerwa na rushwa.
...Naona siasa na kanisa zinaendelea kupamba moto,ungemuona Nape ungesema kuwa ameanza kuwa mchungaji,alikuwa anaongea mpaka povu linamtoka mdomoni.
Source : TBC 1
Mbona thread hii ni ya kijinga? Nape ni Mkristo, mlitaka aende msikiti gani au aende jamatini? Hivi tumefikia mahali ambapo viongozi hawatakiwi kwenda kusali? Kila kanisa linajisikia fahari kiongozi akiwepo na mara zote hutoa nafasi kwa viongozi ya kusalimia. Mnataka viongozi wakatae kuongea ili waonekane viongozi wazuri?
Tunachokipinga ni huu utaratibu wa Edward Lowassa kutembeza ufalme makanisani wa kumwaga fedha alizotuibia alipokuwa Waziri na baadaye Waziri Mkuu. Lengo lake kuu ni kujisafisha aonekane mtu safi wakati ni mwizi, tena mwizi mkubwa.