Nape: Nchi hii ina wenyewe na wenyewe ni CCM!

Haya maneno wanasiasa, waliolewa madaraka, wanayoyatumia, waangalie, yasije kuwatokea kwa haja ndogo kama si puani, ulimi ulikiponza kichwa ati!, hizi mbwembwe zao zilizozidi, zitawapeleka pabaya.
 
Angemalizia tu na ccm ina wenyewe na wenyewe ni mafisadi papa.

Unafikiri wao hawajijui kama ni mafisadi, wanajijua, sema watu wakisema, wanakuwa wakali, kwa mfano unafikiri mwizi hajijui kama yeye ni mwizi, anajijua, ila mtu mwingine akisema, akimsema kuwa yeye ni mwizi, anakuwa mkali, hata kahaba pia.
 
Kulikuwa hakuna umuhimu wa kuweka hii stori hapa JF maana kila anachoongea Nape ni MTOKOTO. Huyu kijana mtokotaji imeshakuwa kawaida yake kuongea bila kukumbuka kuwa siasa ya chama kimoja hazipo tena. Hilo suala halihitaji hata kwenda shule ya chekechea kujifunza, this guy needs help.
 
hivi hicho chama kina members wangapi? hii itasaidia kujua idadi ya wasio wananchi lakini tunaishi Tanzania..
Kati ya matamshi yanayokera, hili linaongoza..na ni tamko hatarishi
 
Unafikiri wao hawajijui kama ni mafisadi, wanajijua, sema watu wakisema, wanakuwa wakali, kwa mfano unafikiri mwizi hajijui kama yeye ni mwizi, anajijua, ila mtu mwingine akisema, akimsema kuwa yeye ni mwizi, anakuwa mkali, hata kahaba pia.

Cha ajabu mtu muovu ukimpa sifa nzuri ambayo hana, na anajijua kabisa hana sifa hiyo, atajipongeza kwa kukushukuru na kuchekelea, wala hataikataa, kumbe si ajabu, we unamkejeli, inahitaji moyo kukataa sifa nzuri ambayo huna au kukataa pongezi za kejeli ambazo hustahili kwa sababu, kiukweli haujafanya tukio au maendeleo unayosifika kuyafanya kwa kiwango kinachofaa na cha kukufanya ustahili pongezi.
 
Je mawaziri kama akina Wasira, akina Magufuli, wao si watumishi waserikali? sasa hapa Nchemba anataka kutuambia aliona walimu tu, ila mawaziri waliotumia kuahidi vitu ambavyo walihitaji kuvitenda kama kazi yao yakawaida wakawadanganya wanaigunga kama sehemu ya kampeni. CCM walevi wamadaraka.

Akasisitiza wao wapo tayari kusema tuandamane hadi ikulu kuindoa serikali na hawaoni aibu amani endapo itapotea!

Akasema serikali haiwezi kulikubali hilo, naye Nchemba akasema walimu wanaposimamia
uchaguzi wakumbuke kuwa wao ni watumishi wa serikali na endapo CDM isingesaidiwa na walimu basi CDM ingepata kura 1000!
 
Mkuu ushaenda kusoma hiki kitabu? Ni vitu vya kawaida kwa vyama vinavyoongoza kwa muda mrefu kusema hivyo. Until you prove them otherwise!
Naomba usinipe BAN, and this is not thinking outside of the box, this shows that THERE'S NO BOX!!

!
1478815_1296045936.jpg


Chegg does not guarantee CDs, access codes, or lab manuals with this book.


ISBN: 0253285917

ISBN-13: 9780253285911



PUBLISHER: Indiana University Press
AUTHORS: Francis Meli
South Africa Belongs to Us: "... Meli combines the insights of an insider with sound scholarship." -- Patrick O'Meara"Meli's book is a welcome addition to the literature on South Africa." -- L. E. Meyer, Choice"... the book is written in a sober, matter-of-fact style with a minimum of invective and rhetoric. Packed with quotations and thoroughly annotated, it appeals to reason more than the emotions and deserves to be taken seriously as history rather than dismissed as propaganda or myth making." -- The New York Review of Books"This book is clearly the most important one written on South Africa during the last decade." -- Nature, Society, and Thought"... made the case for the ANC's central role as South Africa's historic movement for economic justice as well as racial and political democracy." -- Journal of African HistoryIn this history of the African National Congress, Francis Meli demonstrates that the party is central to the future of South Africa. British, American, and other Western governments have finally recognized that no South African settlement is possible without dealing with the ANC. «Show less
South Africa Belongs to Us: "... Meli combines the insights of an insider with sound scholarship." -- Patrick O'Meara"Meli's book is a welcome addition to the literature on South Africa." -- L. E. Meyer, Choice"... the book is written in a sober, matter-of-fact... Show more»
Rent South Africa Belongs to Us today, or search our site for other Meli africa textbooks. Every textbook comes with a 21 day "Any Reason" guarantee.

Context ni tofauti kabisa.

SA ilitolewa kwenye Apartheid na ANC ambapo wazungu wachache walidhani kuwa ndio wenye nchi.

ANC ni chama cha Weusi walio wengi na waliokuwa hawana lao kwa muda mrefu, hivyo context yao ya kutamka hivyo ni tofauti na ya chama kinachong'ang'ania madarakani kwa michezo michafu, kisichoheshimu wananchi wa kawaida, na kinachosimamia maslahi ya kichama zaidi.
 
Nape mbona ni mpumbav tu. Mkapa alishasema kuwa ccm haina hatimiliki ya Tanzania.Na tutamdhihirishia nape hilo jambo 2015.
 
Taarifa ITV muda huu namwona Nape anadai nchi hii ina wenyewe na wenyewe ni chama cha mapinduzi!

Hivi huyu mtu ana akili kweli? Ina maana wote wasio katika CCM hawana haki na hii nchi?

wanachama wa ccm wanaoilpa michango na hivyo kuwa hai hawafiki laki tano........................kwa nchi yenye raia wapatao milioni 50...................sijui ni kwa mantiki ipi ccm nchi hii ni yao...........................labda kwa misingi ya kupora haki yetu kujichagulia viongozi tuwapendao.......
 
Taarifa ITV muda huu namwona Nape anadai nchi hii ina wenyewe na wenyewe ni chama cha mapinduzi!

Hivi huyu mtu ana akili kweli? Ina maana wote wasio katika CCM hawana haki na hii nchi?

yani kauli zingine Mungu saidia tu. Ngoja tuombe uhai ili kushuhudia yeye mwenyewe akiitenda hii kauli
 
Wale magamba 3 mbona ameshindwa kuwaondoa? Nasikia igunga alikimbizwa na baunsa mmoja akatoka mbio, kwani anaishi sehemu gani huyu nape?, mi nacheka tu, nasikia alikuwa miongoni mwa ccj sasa ccm anatafuta nini? Njaa tu, bali atuombe radhi haraka iwezekanavyo, hii ni nchi yetu na si ya ccm, ashindwe na alegee
 
Nilimwona akiongea jana and my conclusion was, "kama huyu bwana havuti bhange bac hana siku nyingi ameacha"
 
Angesema, nchi hii ina wajinga, na wajinga wenyewe ndio wao. Lakini huyu kijana hajui kuongea ndio maana ilifukuzwa Igunga. Nimsaidie, ccm ni yao na nchi ni yetu waTZ.
 
Regia,

Think outside the box.

Kumbuka, JK alishatwambia kuwa "Anachoongea Nape ndio msimamo wa chama" na hivyo napenda kujiaminisha kuwa NDIVYO alivyotumwa na chama na kupewa baraka na mwenyekiti wa chama aongee kwa watanzania kwa ujumla wao.

SASA, watanzania tutaendelea kudharauliwa kiasi hiki mpaka lini? Hivi kweli sisi tusio na vyama hatuna chetu Tanzania hii? Na CHADEMA mkija kuingia madarakani (endapo itatokea) mtatufanyia dharau za namna hii?

Hivi wanasiasa mnajua tumewavumilia sana? Mnajua mnaanza kututia vidole machoni sasa?

Nape, tutake radhi watanzania. Waweza kudai hukumaanisha inavyoonekana au ilivyoelezwa na watu lakini nikiri kuwa kauli hii INAKERA hasa kwa sisi tusio na vyama vya siasa; wachilia mbali wapinzani wenu kisiasa. Labda kama umeongopewa si wewe uliyeongea haya.

Hakika naona Nape sasa ANANITATIZA NA KAULI YAKE YA JANA.Ni kauli INAYOKERA,CHEFUA NA KULETA CHUKI ZAIDI HATA KAMA MTU ALIKUA HANA NIA YA KUICHUKIA CCM ATAICHUKIA KUPITIA KAURI KAMA YA NAPE YA JANA.

Mimi ni kijana wa kizazi kipya ambae sina sura ya kichama bali SURA YANGU NI TANZANIA MBELE.Kwa kauli ya NAPE hakika kuna jambo tata sana kupitia kijana huyu na chama cha Mapinduzi.Nimekuwa najaribu sana kusema zile picha na muonekanao ambao wazee wetu walizokuwa nazo kuwa ili uwe MTANZANIA WA KWELI NI LAZIMA UWE MFUASI WA CCM kuwa kwa sasa zimepitwa na wakati.Sikutegemea kusikia kauri toka kwa kijana Nape ambae nilikua naamini kuwa ATAIBUKA KAMA CHANZO CHA KIZAZI KIPYA NDANI YA CCM KITAKACHO LETA MAPINDUZI YA KIFIKRA YA WAZEE WETU NDANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI,kuwatoa kwenye mtizamo wa kuamini kuwa pasipo CCM hakuna Tanzania.

Hakika siasa ni ULEVI [Opium] kama mhusika ajitambui basi ni hatari sana kwa TAIFA.Kwa picha hii ya Jana ya NAPE ni hakika CCM kuna HATARI kubwa sana uko mbele ya safari.

Ni kweli mfumo ambao wazee wetu waliujenga wakati wa Mwalimu baada ya uhuru ulizingatia chama kwanza kwa kuzingatia nyakati na muda wa kipindi hicho na siasa za dunia kwa ujumla wake ilikuwa sawa kwao kwa wakti huo na elimu yao ya wakati huo.Leo hii TAIFA linalokwenda kwenye UTANDAWAZI kuliweka TAIFA mikononi mwa CCM kuwa ndio wanauchungu na wenye haki na ustawi wa TANZANIA ni kuliweka TAIFA kwenye rehani na hati hati kama tunazo ziona sasa.

TAIFA ni dhamana ya Watanzania wote bila kujali CHAMA,DINI AU KABILA bali UTAIFA.Kauri ya NAPE ni dalili za matusi na kuibua hisia za chuki dhidi ya vyama vingine na hivyo kuhatarisha usalama wa TAIFA.Tulipofika NAPE kwa lugha yake hiyo kunaibua hisia za uchonganishi wa kiitikadi kati yake na wale wote wenye kuipenda Tanzania ambao hawako CCM lakini wana mapenzi mema na TAIFA lao.Na chuki hiyo ndiyo inayotengeneza hayo ambayo kwa kiwango fulani bado ni jinamizi la CCM.

Dhamila yangu ya ndani katika haya tunayoyaona kila siku yakisemwa na wengi kuwa CCM IMEFIKA WAKATI IFE,mimi binafsi SIKUWA NAPENDA ILI LITOKEE KWA KUWA NI KWELI VYAMA VINGI VYA UKOMBOZI VYA AFRICA HATA UGHAIBUNI VINGI VIMEKUFA.Nilitaka CCM kibaki kiendelee kuishi katika Taifa kama au chama cha Upinzania au chama Tawala na kuleta HIstoria ya kidunia katika siasa za kidunia na Africa kwa ujumla wake.

Kwa picha hii,ambayo niliamini kwa kijana kama Nape kuwa ni matunda kizazi kipya yatakayo leta mwamko mpya wa kisiasa ndani ya CCM na kuwafanya Wazee wa CCM watambue wajibu wao wa kutoka ndani ya fikra zao za kuingangania Tanzania kumilikiwa na CCM,na kuiachia Tanzania ndani ya Watanzania bali CCM kubaki kuwa chama kinachoomba ridhaa ya Watanzania kupata nafasi ya kutwala na kumilikishwa dhamana ya utawala kwa kipindi cha miaka Mitano.

Lakini cha ajabu imani yangu ya kuamini ndoto zangu uenda Nape akawa tunda la kizazi kipya lenye kusudio la kuwapa hisia Wazee wetu walio ndani ya CCM kuwa hizi ni nyakati mpya na kila zama na vitabu vyake [Mzee Mwinyi],Nape kashindwa hilo na hakika CCM anaitajika kijna mwingine Mpya atakae kuwa na maono [vision] ya Mheshimiwa Pombe John Magufuri lakini katika umri wa miaka therasini [30s]na hivyo kuwafanya wazee hao kuliona TAIFA kupitia kijana wao huyo hivyo kuliepusha TAIFA katika hatari inayolinyemelea ya kusambalatika.

Nape picha aliyoionyesha ni kufikisha salamu kwa Wapenda amani na wanaolitakia TAIFA nia njema kuwa TANZANIA ni MALI YA CCM na YEYE NAPE KAKUBALI MANENO YA WAZEE WA CCM KUWA TANZANIA NI MALI YA CCM NA SI MALI YA WATANZANIA ambao wengine ni wanachama wa CCM,CUF,CDM,TLP,na vyama vingine na wasio na vyama vya kisiasa.

CCM hakika its too late to catch the train,nilitamani kuiona CCM ikipita mabonde na kuendelea kushiriki kuijenga Tanzania kama chama cha UPINZANI AU CHAMA TAWALA hivyo kuleta changamoto kama tunazoziona katika Taifa kama la USA kati ya chama cha DEMOCRATIC NA REPBULICAN, au vyama viwili vya UK, lakini naona maneno mengi ya UMMA yanayoumba kuhusu kifo cha CCM hakika YANAUMBA KIFO CHAKE KWELI.

Kwenye nyekundu hakika ndio ukweli wenyewe.
 
Mshezi sana, huwezi kusema nchi hii ni yenu na familia zenu, kumbe ndo maana hawaishi kutusingiza sisi maskini kuwa sio raia wa nchi hii,
 
I said before, Nape is a hopeless opportunist... Mropokaji tu! Msishangae kesho akipinga kuwa hajasema hilo.
 
Nape akili timamu hana awaambie wanachama wenzie yalomtokea katika kampeni za madiwani kule mara(serengeti na Rorya) ilikuwa ni kuzomewa tu.Huyu dogo njaa inamsumbua hana hata msimamo maana hata leo unaweza ukamwona jukwaani akimkampenia RA.
 
Back
Top Bottom