Power G
JF-Expert Member
- Apr 20, 2011
- 3,886
- 1,194
Wapenzi wa JF, ni miezi sita kamili tangu Mamsapu wangu apate ajira katika kampuni moja ya umma hapa jijini Dar. Siku tu ya kwanza amekwenda kuripoti aliporudi home aliniambia kwamba hajaona kampuni ambayo ina wakaware wengi kama hiyo. Katika miezi mitatu ya kwanza akiwa hapo kila aliyetaka kumletea mazoea mabaya alinipa taarifa. Hata wale waliomkonyeza, waliompa offer za lunch akazitolea nje, waliomtekenya kwenye kiganja wakati wakisalimia kwa mkono, waliojipitisha pitisha ofisini kwake kumtaka mazungumzo yasiyo na kichwa wala miguu, wote hao nilipewa taarifa zao. Mamsapu muda wa kufika nyumbani toka kazini katika hiyo miezi 3 ya mwanzo ilikuwa kabla ya saa 12 jioni.
Baada ya miezi mitatu kumalizika, mambo naona yamebadilika kabisa. Zile taarifa za wakware sipati hata moja (siuji kama wale wakware wote walishaacha kazi ama la!) na wife "amekuwa na kazi nyingi sana" kiasi kwamba muda wa kufika nyumbani ni saa 3 hadi saa 4 usiku, Kazini anakwenda hadi week end na kwenye pay slip sijawahi kuona amepata malipo ya overtime!
Hiki kimya kinanipa wasi wasi kwamba labda sipati taarifa kwa kuwa sasa tayari kuna maridhiano tofauti na hapo mwanzoni. Je ninyi mnafikiriaje juu ya hili???
Baada ya miezi mitatu kumalizika, mambo naona yamebadilika kabisa. Zile taarifa za wakware sipati hata moja (siuji kama wale wakware wote walishaacha kazi ama la!) na wife "amekuwa na kazi nyingi sana" kiasi kwamba muda wa kufika nyumbani ni saa 3 hadi saa 4 usiku, Kazini anakwenda hadi week end na kwenye pay slip sijawahi kuona amepata malipo ya overtime!
Hiki kimya kinanipa wasi wasi kwamba labda sipati taarifa kwa kuwa sasa tayari kuna maridhiano tofauti na hapo mwanzoni. Je ninyi mnafikiriaje juu ya hili???