UKI
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 691
- 172
NAITWA FRANK (sio jina halisi) nimetokea kumpenda binti Jane(sio jina halisi) tulisha do mara moja tu tukapanga kuchumbiana na tukakubaliana sasa jambo moja limejitokeza nilikuwa simjui ni mtoto wa nani ingawa kumbe mama yake ninamjua vizuri na hii kwa kutomjua mama yake ni kwa sababu alikuwa anasoma mwanza na mimi nilikuwa nafanya kazi zangu shinyanga so sikuwahi kwenda kwao pande za dar, ila dar ndiko wazazi wangu wapo na kumbe ninamjua huyo mama anapokaa dar. siku alipokuwa likizo na mimi nilienda dar na nikaenda mpka kwao dah nilipokaribia nilishtuka sana nikamuambia hapa ninapajua sana na mama huyu namjua namuita kama mama basi tukaongea kwa sana kipindi hicho mama yake hakuepo alikuwa ameenda town basi siku ikapita ikabidi suala la kuwashirikisha ndugu na jamaa kuwa mungu akijalia nitaoa kwa fulani story hii nilimueleza baba yangu wa ubatizo kwani baba yangu alifariki siku nyingi, huwezi amini mzee kwanza alianza kunipongeza kwa sana akasema umechagua penyewe alianza kutiririka kuwa huyo mama yake alikuwa ana mapenzi na baba yangu kwa sana tu (ina maana walikuwa wanado kabla hajampata mama yangu) na mimi nilikuwa sijazaliwa dah nilichoka na akasema hata huyo mama anajua hilo na ndio anakuita kama mtoto wake, nilichoka sikuvumilia nikaenda kutiririka kwa mpenzi wangu akaniambia ngoja na yeye ahakikishe hilo akamueleza mama yake kuhusu hilo mama yake alikuwa happy kwa hilo nae akamueleza kila kitu,tupo bado kwenye uchumba bahati mbaya sasa hivi nimepata kazi huku botswana mkataba miaka miwili ndio narudi now namaliza mwaka bado mwaka mmoja ndio nirudi, swali langu kwa wana JF je hapo sio kwamba namuoa dada yangu? na wazee wa waliokuwa kipindi hicho watasemaje?? naombeni mniondoe haya mawazo kwa kweli na sitaki nionekane muaribifu mtoto wa mtoto wa watu bila sababu maana ni sehemu tunayoheshimiana sana naombeni tafadhali kwa hili mnishauri niendelee au nisiendelee