Naona hili ni tatizo kubwa sana kwa watangazaji wetu wa vituo vyote vya redio kuanzia redio ya taifa mpaka vituo vidogo vya redio linapokuja jina lenye asili ya kijerumani matamshi yanakuwa ndivyo sivyo kabisa. Ni kama wewe umsikie mtu akitamka jina Juma kama Jima au Joma. Au jina Ali kama Hali, James kama Jemesi, Mwajuma kama Mijuma n.k. Hii inaleta ukakasi masikioni. Nitaanza na majina machache na kama yeyote anahitaji usaidizi wa matamshi ya majina mengine au hata maneno ya kijerumani dondosha kwenye uzi huu kwa msaada.
1. Naanza na hili liwasaidie hata walimu na wanafunzi wa fizikia ( physics).
Albert Einstein : Nguli wa fizikia na hisabati - Tamka ALBART AINSHTAIN. Katika sarufi ya kijerumani herufi e na i zikifuatana (ei) hutamkwa kama "ai" na s na t zikifuatana (st) hutamkwa kama "sht"
2. Frank-Walter Steinmeir: Rais wa Ujerumani - Tamka FRANK VALTA SHTAINMAIA. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi W hutamkwa kama tunavyotamka herufi V. herufi "r" ikikaa mwisho wa neno itamke kama "a".
3. Annalena Baebock: Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani - Tamka ANALENA BEEBOK. Kwenye sarufi ya kijerumani herufi a na e zikifuatana (ae) hutamkwa sawa na ule mlio wa mbuzi (meeee!). Mara nyingi badala ya herufi mbili ae huandikwa tu ä.
4. Jens Stoltenberg: Katibu mkuu wa NATO - Tamka YEENS SHTOLTENBERG. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi J hutamkwa kama tunavyotamka herufi Y.
5. Ursula von der Leyen: Raisi wa Kamisheni ya Ulaya ( EU Commission). Huyu sijui kama kuna siku inapita bila kutajwa. Ni watangazaji wa DW tu nimewasikia wakilitamka jina lake kwa usahihi. Tamka URSULA FON DEA LEYEN. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi V hutamkwa kama herufi yetu F.
6. Olaf Scholz: Raisi wa Ujerumani- Tamka OLAF SHOLZ. Kwenye sarufi ya kijerumani "sch" hutamkwa kama "sh" . Mfano: Kijerumani- Schule, Kiswahili- Shule
Natumaini uzi huu uwasaidie hasa watangazaji wetu maana matangazo yanaenda nje ya mipaka ya nchi pia. Kwa msaada zaidi dondosha swali lako hapa.
1. Naanza na hili liwasaidie hata walimu na wanafunzi wa fizikia ( physics).
Albert Einstein : Nguli wa fizikia na hisabati - Tamka ALBART AINSHTAIN. Katika sarufi ya kijerumani herufi e na i zikifuatana (ei) hutamkwa kama "ai" na s na t zikifuatana (st) hutamkwa kama "sht"
2. Frank-Walter Steinmeir: Rais wa Ujerumani - Tamka FRANK VALTA SHTAINMAIA. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi W hutamkwa kama tunavyotamka herufi V. herufi "r" ikikaa mwisho wa neno itamke kama "a".
3. Annalena Baebock: Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani - Tamka ANALENA BEEBOK. Kwenye sarufi ya kijerumani herufi a na e zikifuatana (ae) hutamkwa sawa na ule mlio wa mbuzi (meeee!). Mara nyingi badala ya herufi mbili ae huandikwa tu ä.
4. Jens Stoltenberg: Katibu mkuu wa NATO - Tamka YEENS SHTOLTENBERG. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi J hutamkwa kama tunavyotamka herufi Y.
5. Ursula von der Leyen: Raisi wa Kamisheni ya Ulaya ( EU Commission). Huyu sijui kama kuna siku inapita bila kutajwa. Ni watangazaji wa DW tu nimewasikia wakilitamka jina lake kwa usahihi. Tamka URSULA FON DEA LEYEN. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi V hutamkwa kama herufi yetu F.
6. Olaf Scholz: Raisi wa Ujerumani- Tamka OLAF SHOLZ. Kwenye sarufi ya kijerumani "sch" hutamkwa kama "sh" . Mfano: Kijerumani- Schule, Kiswahili- Shule
Natumaini uzi huu uwasaidie hasa watangazaji wetu maana matangazo yanaenda nje ya mipaka ya nchi pia. Kwa msaada zaidi dondosha swali lako hapa.