Naomba niwasaidie watangazaji wa vituo vyote vya redio namna ya kutamka majina ya Kijerumani

raslimali

JF-Expert Member
Nov 4, 2014
1,344
1,012
Naona hili ni tatizo kubwa sana kwa watangazaji wetu wa vituo vyote vya redio kuanzia redio ya taifa mpaka vituo vidogo vya redio linapokuja jina lenye asili ya kijerumani matamshi yanakuwa ndivyo sivyo kabisa. Ni kama wewe umsikie mtu akitamka jina Juma kama Jima au Joma. Au jina Ali kama Hali, James kama Jemesi, Mwajuma kama Mijuma n.k. Hii inaleta ukakasi masikioni. Nitaanza na majina machache na kama yeyote anahitaji usaidizi wa matamshi ya majina mengine au hata maneno ya kijerumani dondosha kwenye uzi huu kwa msaada.

1. Naanza na hili liwasaidie hata walimu na wanafunzi wa fizikia ( physics).

Albert Einstein : Nguli wa fizikia na hisabati - Tamka ALBART AINSHTAIN. Katika sarufi ya kijerumani herufi e na i zikifuatana (ei) hutamkwa kama "ai" na s na t zikifuatana (st) hutamkwa kama "sht"

2. Frank-Walter Steinmeir: Rais wa Ujerumani - Tamka FRANK VALTA SHTAINMAIA. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi W hutamkwa kama tunavyotamka herufi V. herufi "r" ikikaa mwisho wa neno itamke kama "a".

3. Annalena Baebock: Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani - Tamka ANALENA BEEBOK. Kwenye sarufi ya kijerumani herufi a na e zikifuatana (ae) hutamkwa sawa na ule mlio wa mbuzi (meeee!). Mara nyingi badala ya herufi mbili ae huandikwa tu ä.

4. Jens Stoltenberg: Katibu mkuu wa NATO - Tamka YEENS SHTOLTENBERG. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi J hutamkwa kama tunavyotamka herufi Y.

5. Ursula von der Leyen: Raisi wa Kamisheni ya Ulaya ( EU Commission). Huyu sijui kama kuna siku inapita bila kutajwa. Ni watangazaji wa DW tu nimewasikia wakilitamka jina lake kwa usahihi. Tamka URSULA FON DEA LEYEN. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi V hutamkwa kama herufi yetu F.

6. Olaf Scholz: Raisi wa Ujerumani- Tamka OLAF SHOLZ. Kwenye sarufi ya kijerumani "sch" hutamkwa kama "sh" . Mfano: Kijerumani- Schule, Kiswahili- Shule

Natumaini uzi huu uwasaidie hasa watangazaji wetu maana matangazo yanaenda nje ya mipaka ya nchi pia. Kwa msaada zaidi dondosha swali lako hapa.
 
Naona hili ni tatizo kubwa sana kwa watangazaji wetu wa vituo vyote vya redio kuanzia redio ya taifa mpaka vituo vidogo vya redio linapokuja jina lenye asili ya kijerumani matamshi yanakuwa ndivyo sivyo kabisa. Ni kama wewe umsikie mtu akitamka jina Juma kama Jima au Joma. Au jina Ali kama Hali, James kama Jemesi, Mwajuma kama Mijuma n.k. Hii inaleta ukakasi masikioni. Nitaanza na majina machache na kama yeyote anahitaji usaidizi wa matamshi ya majina mengine au hata maneno ya kijerumani dondosha kwenye uzi huu kwa msaada.

1. Naanza na hili liwasaidie hata walimu na wanafunzi wa fizikia ( physics).

Albert Einstein : Nguli wa fizikia na hisabati - Tamka ALBART AINSHTAIN. Katika sarufi ya kijerumani herufi e na i zikifuatana (ei) hutamkwa kama "ai" na s na t zikifuatana (st) hutamkwa kama "sht"

2. Frank-Walter Steinmeir: Rais wa Ujerumani - Tamka FRANK VALTA SHTAINMAIA. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi W hutamkwa kama tunavyotamka herufi V. herufi "r" ikikaa mwisho wa neno itamke kama "a".

3. Annalena Baebock: Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani - Tamka ANALENA BEEBOK. Kwenye sarufi ya kijerumani herufi a na e zikifuatana (ae) hutamkwa sawa na ule mlio wa mbuzi (meeee!). Mara nyingi badala ya herufi mbili ae huandikwa tu ä.

4. Jens Stoltenberg: Katibu mkuu wa NATO - Tamka YEENS SHTOLTENBERG. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi J hutamkwa kama tunavyotamka herufi Y.

5. Ursula von der Leyen: Raisi wa Kamisheni ya Ulaya ( EU Commission). Huyu sijui kama kuna siku inapita bila kutajwa. Ni watangazaji wa DW tu nimewasikia wakilitamka jina lake kwa usahihi. Tamka URSULA FON DEA LEYEN. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi V hutamkwa kama herufi yetu F.

6. Olaf Scholz: Raisi wa Ujerumani- Tamka OLAF SHOLZ. Kwenye sarufi ya kijerumani "sch" hutamkwa kama "sh" . Mfano: Kijerumani- Schule, Kiswahili- Shule

Natumaini uzi huu uwasaidie hasa watangazaji wetu maana matangazo yanaenda nje ya mipaka ya nchi pia. Kwa msaada zaidi dondosha swali lako hapa.
.
 
Naona hili ni tatizo kubwa sana kwa watangazaji wetu wa vituo vyote vya redio kuanzia redio ya taifa mpaka vituo vidogo vya redio linapokuja jina lenye asili ya kijerumani matamshi yanakuwa ndivyo sivyo kabisa. Ni kama wewe umsikie mtu akitamka jina Juma kama Jima au Joma. Au jina Ali kama Hali, James kama Jemesi, Mwajuma kama Mijuma n.k. Hii inaleta ukakasi masikioni. Nitaanza na majina machache na kama yeyote anahitaji usaidizi wa matamshi ya majina mengine au hata maneno ya kijerumani dondosha kwenye uzi huu kwa msaada.

1. Naanza na hili liwasaidie hata walimu na wanafunzi wa fizikia ( physics).

Albert Einstein : Nguli wa fizikia na hisabati - Tamka ALBART AINSHTAIN. Katika sarufi ya kijerumani herufi e na i zikifuatana (ei) hutamkwa kama "ai" na s na t zikifuatana (st) hutamkwa kama "sht"

2. Frank-Walter Steinmeir: Rais wa Ujerumani - Tamka FRANK VALTA SHTAINMAIA. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi W hutamkwa kama tunavyotamka herufi V. herufi "r" ikikaa mwisho wa neno itamke kama "a".

3. Annalena Baebock: Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani - Tamka ANALENA BEEBOK. Kwenye sarufi ya kijerumani herufi a na e zikifuatana (ae) hutamkwa sawa na ule mlio wa mbuzi (meeee!). Mara nyingi badala ya herufi mbili ae huandikwa tu ä.

4. Jens Stoltenberg: Katibu mkuu wa NATO - Tamka YEENS SHTOLTENBERG. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi J hutamkwa kama tunavyotamka herufi Y.

5. Ursula von der Leyen: Raisi wa Kamisheni ya Ulaya ( EU Commission). Huyu sijui kama kuna siku inapita bila kutajwa. Ni watangazaji wa DW tu nimewasikia wakilitamka jina lake kwa usahihi. Tamka URSULA FON DEA LEYEN. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi V hutamkwa kama herufi yetu F.

6. Olaf Scholz: Raisi wa Ujerumani- Tamka OLAF SHOLZ. Kwenye sarufi ya kijerumani "sch" hutamkwa kama "sh" . Mfano: Kijerumani- Schule, Kiswahili- Shule

Natumaini uzi huu uwasaidie hasa watangazaji wetu maana matangazo yanaenda nje ya mipaka ya nchi pia. Kwa msaada zaidi dondosha swali lako hapa.
Guten morgen Bruder
 
Kuna kile kikundi cha hilter cha SS sijui kukiandika wala kukisoma, nisaidie hapa
 
Naona hili ni tatizo kubwa sana kwa watangazaji wetu wa vituo vyote vya redio kuanzia redio ya taifa mpaka vituo vidogo vya redio linapokuja jina lenye asili ya kijerumani matamshi yanakuwa ndivyo sivyo kabisa. Ni kama wewe umsikie mtu akitamka jina Juma kama Jima au Joma. Au jina Ali kama Hali, James kama Jemesi, Mwajuma kama Mijuma n.k. Hii inaleta ukakasi masikioni. Nitaanza na majina machache na kama yeyote anahitaji usaidizi wa matamshi ya majina mengine au hata maneno ya kijerumani dondosha kwenye uzi huu kwa msaada.

1. Naanza na hili liwasaidie hata walimu na wanafunzi wa fizikia ( physics).

Albert Einstein : Nguli wa fizikia na hisabati - Tamka ALBART AINSHTAIN. Katika sarufi ya kijerumani herufi e na i zikifuatana (ei) hutamkwa kama "ai" na s na t zikifuatana (st) hutamkwa kama "sht"

2. Frank-Walter Steinmeir: Rais wa Ujerumani - Tamka FRANK VALTA SHTAINMAIA. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi W hutamkwa kama tunavyotamka herufi V. herufi "r" ikikaa mwisho wa neno itamke kama "a".

3. Annalena Baebock: Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani - Tamka ANALENA BEEBOK. Kwenye sarufi ya kijerumani herufi a na e zikifuatana (ae) hutamkwa sawa na ule mlio wa mbuzi (meeee!). Mara nyingi badala ya herufi mbili ae huandikwa tu ä.

4. Jens Stoltenberg: Katibu mkuu wa NATO - Tamka YEENS SHTOLTENBERG. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi J hutamkwa kama tunavyotamka herufi Y.

5. Ursula von der Leyen: Raisi wa Kamisheni ya Ulaya ( EU Commission). Huyu sijui kama kuna siku inapita bila kutajwa. Ni watangazaji wa DW tu nimewasikia wakilitamka jina lake kwa usahihi. Tamka URSULA FON DEA LEYEN. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi V hutamkwa kama herufi yetu F.

6. Olaf Scholz: Raisi wa Ujerumani- Tamka OLAF SHOLZ. Kwenye sarufi ya kijerumani "sch" hutamkwa kama "sh" . Mfano: Kijerumani- Schule, Kiswahili- Shule

Natumaini uzi huu uwasaidie hasa watangazaji wetu maana matangazo yanaenda nje ya mipaka ya nchi pia. Kwa msaada zaidi dondosha swali lako hapa.
Olaf ni waziri mkuu bruder, ansonsten umesomeka mkuu!
 
Namba 3 inatamkwa Beabok acha mambo yako hata huyo Ursula inatamkwa Urzula sio kama unavyotuambia
 
Kutamka na kuandika ni mambo mawili tofauti Mkuu.

Kama alivyoshauri mdau hapo juu. Ni vyema useme Audio au video ya namna inavyoandikwa na jinsi inavyotamkwa.

Ni sehemu nzuri ya kujitangaza
 
Una patikana jimbo gani ujerumani?

Una mpango wa kufungua darasa mtandaonii?
CCM inatamkwa schicem
KINANA inatamkwa chinerner
Chongolo inatamkwa tshonglo.
Jifunzeni kiswahili nyie nzi wa kijani msiwe kama wenzenu nyumbu kila kitu ni kupinga tuu....bahati mbaya wa mizambarauni hata hawajui zzk wao anataka Nini.
 
Uwasaidie pia na hawa wachambuzi wetu uchwara wa mpira wa miguu na ambao hawajui kutamka kwa ufasaha majina ya baadhi ya vilabu vya mpira wa miguu vya Ujerumani; Schalke 04, nk.
 
Back
Top Bottom