Hata ukiitunza vizuri, ikiwa katia mifuko hii ya kilo 50 tuliyoizoea, katika mazingira ya joto na unyevu, sementi huanza kupoteza nguvu taratibu baada ya miezi kama mitatu. Bada ya miezi 6 uwezekano wa kuwa ina nguvu kidogo sana ni mkubwa. Inategemeana sana na hali ya unyevu.
Iwapo unahitaji kuhifadhi sementi kwa muda mrefu jitahidi kutokupanga zaidi ya mifuko nane kwenda juu na pia isiguse kuta wala sakafu.
Dalili inayoonekana wazi ya kuharibika kwa sementi ni kugandamana kama jiwe. Inashauriwa kwamba iwapo kuna vibongebonge unavyoweza kulainisha kwa vidole - bado unaweza kuitumia, lakini ukihitaji nguvu zaidi kuipondaponda- hapo haifai.
Kawaida cement hasa aina ya "Portland cement" na "Portland pozzolana cement" inatakiwa itumike ndani ya miezi mitatu tangu itengenezwe kiwandani. Aina hii ndio inayozalishwa hapa Tanzania.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.