Naomba kupewa elimu juu ya Mbao za kuezekea Nyumba

Chakula Kibaya

JF-Expert Member
Sep 19, 2022
482
1,037
Habari ya usiku ndugu wanajamvi, natumai sote tuko salama na tunaendelea vizuri ujenzi wa taifa. Niende kwenye mada Moja kwa moja.

Mimi ni mjasiriamali ambaye kwa kudra za Mwenyezi Mungu nimebahatika kujenga kaboma na Sasa nimefikia hatua ya kupaua. Kuna mambo mawili naomba kufahamishwa kutoka kwenu kwani naamin humu Kuna wazoefu na wataalamu. Mambo yangu ni haya;

1. Aina zipi za mbao ambazo ni nzuri kuezekea: Kama mnavyojua Kuna aina nyingi za mbao ambazo hutumika kuezekea hivyo naomba kuelimishwa ni aina gani ya mbao ambayo ukiitumia huwa inadumu Sana bila ya kuliwa na wadudu.

Mfano Mimi Niko Mwanza mjini na nasikia wauzaji wengi wanasema Kuna mbao za BUHINDI na mbao za IRINGA. Hii kitu inanichaganya sijui wanamaanisha nini na sijui Kati ya hizo mbao zipi ni nzuri.

2. Dawa ya kutibu mbao na ufanisi wake; Hapa pia naomba kupewa elimu na ushauri juuu ya dawa zinazotumika katika hatua ya awali ya kutibu mbao kabla haijaenda site. Huwa naona Kuna baadhi ya dawa hazina rangi na Kuna dawa nyingine inabadilisha rangi ya mbao Hadi kuwa ya kijani. Swali je Kuna tija ya kutibu mbao na ni dawa ipi nzuri ya kutibu mbao?

Nitashukuru sana endapo nitapewa msaada katika hili. Nawasilisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari ya usiku ndugu wanajamvi, natumai sote tuko salama na tunaendelea vizuri ujenzi wa taifa. Niende kwenye mada Moja kwa moja.

Mimi ni mjasiriamali ambaye kwa kudra za Mwenyezi Mungu nimebahatika kujenga kaboma na Sasa nimefikia hatua ya kupaua. Kuna mambo mawili naomba kufahamishwa kutoka kwenu kwani naamin humu Kuna wazoefu na wataalamu. Mambo yangu ni haya;

1. Aina zipi za mbao ambazo ni nzuri kuezekea: Kama mnavyojua Kuna aina nyingi za mbao ambazo hutumika kuezekea hivyo naomba kuelimishwa ni aina gani ya mbao ambayo ukiitumia huwa inadumu Sana bila ya kuliwa na wadudu.

Mfano Mimi Niko Mwanza mjini na nasikia wauzaji wengi wanasema Kuna mbao za BUHINDI na mbao za IRINGA. Hii kitu inanichaganya sijui wanamaanisha nini na sijui Kati ya hizo mbao zipi ni nzuri.

2. Dawa ya kutibu mbao na ufanisi wake; Hapa pia naomba kupewa elimu na ushauri juuu ya dawa zinazotumika katika hatua ya awali ya kutibu mbao kabla haijaenda site. Huwa naona Kuna baadhi ya dawa hazina rangi na Kuna dawa nyingine inabadilisha rangi ya mbao Hadi kuwa ya kijani. Swali je Kuna tija ya kutibu mbao na ni dawa ipi nzuri ya kutibu mbao?

Nitashukuru sana endapo nitapewa msaada katika hili. Nawasilisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mbao nzuri ni za SAOHILL, ila bei yake kidogo imechangamka
 
Hivi wakuu ipi bora kusubiri fundi amalize kupaua ndio nipake mchanganyiko wa oil chafu na petrol au nipake kabla ya kupiga kenchi
 
Hivi wakuu ipi bora kusubiri fundi amalize kupaua ndio nipake mchanganyiko wa oil chafu na petrol au nipake kabla ya kupiga kenchi
Ukipakia juu wanatoza fedha nyingi kutokana na risk ya kuteleza na kuanguka, japo ni nzuri zaidi maana unapaka surface zote 6 za ubao. Ukipakia chini ni gharama nafuu japo mafundi wa kupiga nao hawapendi kwasababu wanachafuka sana pia wanakuwa kwenye risk ya kuteleza
 
Niko mwanza mkuu,Huko sao hill ni wap?

Sent using Jamii Forums mobile app
Na mimi nilishauriwa ninunue mbao za Buhindi zinatokea maeneo ya Sengerema na baadhi ya visiwa huko ziwani. Inasemekana kua zinatokana na miti iliyo komaa na unaweza kuzitumia bila kuzipaka dawa (ila mimi nilizipaka). Zinapatikana Kenyatta Road nyuma ya makaburi ya wahindi opposite na stand ya Igombe.
 
Lakini si ghali sana kama wasemavyo watu.
Wao hupika kabisa mbao na sio wengine wanaozipaka tu
Ishu kubwa haipo.kwenye kupika mbao , tatizo la mbao kwa sasa lipo kwenye ukomavu wa mti uliokatwa hizo mbao!
Sao hill wanakata miti iliyokomaa sana na ndio mbao nzuri kwa ujenzi hasa kupaua .na ndio mbao ghali.
Mbao iliyokatwa kwenye mti usiokomaa huwa zinapinda muda zikikauka na kama ulipaua ndo ile unakuta mabati yaanaacha mwanya baada ya muda fulani.
Mbao isiyokomaa ni hasara hata kqa wenye hardwares wanaoziuza maana zikikaa muda bila kuuzwa zitapinda na kukosa soko huku unaziona , ndo maana huuzwa kwenye masoko ambayo ni bize kama buguruni ili zitoke kabla hazijakauka
 
Nje ya mada ,Kwa wajuzi bei ya mbao ilivyochangamka na changamoto za kuliwa na wadudu sio wakati muafaka wa kutumia chuma badala ya mbao kwenye kupaua?
 
Na mimi nilishauriwa ninunue mbao za Buhindi zinatokea maeneo ya Sengerema na baadhi ya visiwa huko ziwani. Inasemekana kua zinatokana na miti iliyo komaa na unaweza kuzitumia bila kuzipaka dawa (ila mimi nilizipaka). Zinapatikana Kenyatta Road nyuma ya makaburi ya wahindi opposite na stand ya Igombe.
Nashukuru sana,lakini hata kule sokoni sabasaba si zinapatikana pia???
Nipe uzoefu wako ilikuwa lini ulipozinunua , ulinunua kwa sh ngapi na ulitumia dawa gani kuzitibu!??
Ingawa naona huu ushauri wa kupaka oil chafu mixer petrol ni wa kuzingatiwa.


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom