Naomba kujua ABCs za biashara ya vyombo vya nyumbani(jikoni)

Habari Wana jamvi muhimu kwa vijana.

Natanguliza salamu za dhati kwenu...
Suala naloleta mezani ni kwa wenye uzoefu wa biashara ya vyombo vya ndani.

Nikimaanisha
Bakuli, vikombe
Mabeseni
Majaba
Na KADHALKA

Kwa wenye uzoefu tafadhali nina mambo naomba kuyajua na kama kuna mambo ya
Umuhimu mtaya analyse.
Kwa kuanzia nina capital ya 1m
Vyombo vya plastics mfano vikombe vyupa
Vya chai bakul na kadhalka naweza pata wapi kwa bei nzuri kariakoo pia kuna
Vijana wenzetu wanaofanya hii biashara utakuta wamevimwaga wanauza 200 kila kitu au 500 pia wao wananunua kwa bei ipi
Mpaka wanaeza fanya vile au pia mpangilio upi unawawezesha kupanga katika price zile na profit inakuaje kwa wale ( to which ukiwauliza hawasemagi, wengine watakuambia tu nimeshikiza ya mtu ).

Angalizo: kama hufaham kaa tusubiri mawazo pengine nawe utafaidika au mtag unaejua anafaham wote tufaidike.

Ahsanteni.
"business is life"
Mimi sifahamu kuhusu hii bishara lakini bado ninaweza kukupa ushauri na sitasubiri tu kama unavyotaka. Kama uko Dar tenga siku nenda Kariakoo. Kwanza chunguza vyombo wanavyouza watu wengi vikoje na bei yake ikoje (rejareja). Hili ni rahisi sana kwani utajifanya mnunuzi. Ukimaliza hili zoezi basi ndenda kwenye maduka ya vyombo (kama huyajui unaweza kuulizia kwa ujanja). Nenda na listi yako ulizia bei ya jumla ya kila chombo unachotaka.

Zamani maduka mengi ya vyombo yalikuwa around soko la Kariakoo ila sijui mpangilio wa sasa. All ni all, kujua maduka yalipo ni rahisi sana. Fanya utafiti wako mpaka ujiridhishe ndipo ubebe fedha za manunuzi. Wakati wa kuulizia usiende umevaa vizuri na uonekane una fedha au ubebe fedha. Nenda kimachinga style.
 
Mimi sifahamu kuhusu hii bishara lakini bado ninaweza kukupa ushauri na sitasubiri tu kama unavyotaka. Kama uko Dar tenga siku nenda Kariakoo. Kwanza chunguza vyombo wanavyouza watu wengi vikoje na bei yake ikoje (rejareja). Hili ni rahisi sana kwani utajifanya mnunuzi. Ukimaliza hili zoezi basi ndenda kwenye maduka ya vyombo (kama huyajui unaweza kuulizia kwa ujanja). Nenda na listi yako ulizia bei ya jumla ya kila chombo unachotaka. Zamani maduka mengi ya vyombo yalikuwa around soko la Kariakoo ila sijui mpangilio wa sasa. All ni all, kujua maduka yalipo ni rahisi sana. Fanya utafiti wako mpaka ujiridhishe ndipo ubebe fedha za manunuzi. Wakati wa kuulizia usiende umevaa vizuri na uonekane una fedha au ubebe fedha. Nenda kimachinga style.
Shukurani Sana kaka, ushauri wako unathamani Sana kwangu by kesho nitafika pale kariakoo nianze hivyo maana naplan kufanya hiyo biashara Dodoma so nafikiri umenisaidia na mawazo hayo.
 
Salaam wakuu!

Jamani nahitaji kujulishwa kuhusu biashara ya vyombo vya majumbani hasa ceramic au kwa kiswahili vyombo vya kauli/kuvunjika!

Nahitaji kufanya biashara hii ila sijui hata pa kuanzia, niko Dar.

Kwa anaefahamu wapi naweza kununua kwa jumla anielekeze please! Nilishakwenda kariakoo kufanya utafiti ila nimetoka kapa!

Naombeni mwongozo wenu.

1626087672886.png

 
Kariakoo ule mtaa wa swahili streeet ukatoka kapa? Mbona vimejazana sana...na ungetaka jumla ukiongea na walebwauzaji wangekupa mwongozo.
Hi biashara hata mimi nilitaka sanaa kuifanya sema nikakosa muongozo hivyo kupitia uzi huu nazani naweza kupata Kama atatokea mtu wa kutupa maelezo mazuri.
 
Salaam wakuu!

Jamani nahitaji kujulishwa kuhusu biashara ya vyombo vya majumbani hasa ceramic au kwa kiswahili vyombo vya kauli/kuvunjika!...

Mimi nafanya naagizisha direct China vya kupima kwa Tani ni mchanganyiko, niko navyo vipo njiani vinafika mwezi wa 8 naweza kukuuzia robo tani ukihitaji
 
Ni biashara nzuri ukiwa unavijua vitu na matumizi yake unakuwa unavitangaza na matumizi yake na bei, mfano kitchen gadgets ukiweza kuzitangaza zinatoka sana.
 
Tani 1 ni 1.3 Mil Tsh
Nusu Tani laki 7
Ila bi bei bila usafiri wa kutoka China kwenda Tz
Hapo ni mpaka kampuni ya usafiri ipime mzigo ila kwa mara ya mwisho kutuma Tani 1 ilikuwa USD 550
Asante mkuu kwa kushare...una madini katika nyanja hii naona...
Je ukiuza bei ya kawaida kwa jumla hapa bongo tani moja profit margin ni ngapi? Ukitoa garama zote za mzigo na usafiri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom