Nani yuko nyuma ya Mkataba wa TFF na GSM, kwanini TFF wanazuia usijadiliwe wala kuhojiwa?

1, Azam sports federation cup inadhaminiwa na Azam, na huyohuyo Azam anamiliki timu inayoshiriki hiyo michuano

2. Ligi kuu NBC moja ya mdhamini wake ni Azam.. na Azam haohao wanamiliki timu, mbona hatuskii malalamiko yoyote..??

Sidhani kama kudhamini teams kuna shida, shida ni kumiliki team zaidi ya moja
 
Azam inadhamini timu zote na Yanga inatumia uwanja wa Azam na kipigo Kiko palepale Tu wanakandwa.

Wewe ni daktari wa nini?
Azam haidhamini Timu zote inadhamini Ligi na mkataba wa Udhamini wake ni Kwenye Kuonyesha Ligi..
Na kuhusu Uwanja hawapewi kwa Hisani wanalipia Uwanja, Kwa hyo wakilipia huwezi sema wanapewa Bure..

Swala ni kwamba Kwanini Vipengele vya Udhamini kati ya TFF na GSM visiwekwe wazi...

Vipengele vya NBC na TFF viko wazi
Vipengele vya Azam na TFF viko wazi..
Kwanini GSM na TFF Vifichwe
 
Hujakatazwa kuhoji, ila kawaulize TFF au GSM hao ndiyo wanaweza kutoa ufafanuzi.
Mmeambiwa hivyo tangu 2021. Sportpesa kadhamini Simba, Yanga na Namungo kwa wakati mmoja, mliuliza kwanini?
Vipingele vya Udhamini Vilikuwa wazi..
Ila vipengele vya Udhamini Kwa GSM haviko wazi..

Soma Tena barua ilivyoandikwa
 
1, Azam sports federation cup inadhaminiwa na Azam, na huyohuyo Azam anamiliki timu inayoshiriki hiyo michuano

2. Ligi kuu NBC moja ya mdhamini wake ni Azam.. na Azam haohao wanamiliki timu, mbona hatuskii malalamiko yoyote..??

Sidhani kama kudhamini teams kuna shida, shida ni kumiliki team zaidi ya moja
Tatizo siyo mkataba, Bali tatizo ni 5G.

Simba kila wakifanya tathimini wanaona mechi ya round ya Pili mnara unakwenda kusimama palepale kwenye 5G.
 
1, Azam sports federation cup inadhaminiwa na Azam, na huyohuyo Azam anamiliki timu inayoshiriki hiyo michuano

2. Ligi kuu NBC moja ya mdhamini wake ni Azam.. na Azam haohao wanamiliki timu, mbona hatuskii malalamiko yoyote..??

Sidhani kama kudhamini teams kuna shida, shida ni kumiliki team zaidi ya moja
Ndyo..
Lakini Tatizo linakuja pale ambao Wanufaika wa Udhamini hawajui vipengele vya Mkataba bata kipengele kimoja kwanni?
Nini kinafichwa humo..

Yaani unidhamini mimi halafu huniambii Umeandika nini kwenye mkataba?
 
Kwanini viwe wazi?
Umekosea Swali..
Swali la kujiuliza ni kwanini Vifungwe..
Wote tunajua kuwa Mkataba huwa wazi kwa Wanufaika wa mkataba huo Sasa kwanini Vifungu vya mkataba vifichwe kwa Wanafaika hao??
 
Baada ya Malalamiko mengi ya Wadau kuhusu GSM kuwa na Udhamini wa Timu zaidi ya Sita kwenye Ligi ya NBC,na kufanya Mpira wetu kuwa na sintofahamu kwa sababu GSM pia ndiyo mdhamini wa timu ya Yanga..

baada ya Viongozi sa Simba kuhoji hilo Kwa TFF, TFF imekuja na Jibu kwamba hakuna anayeruhusiwa kuhoji kuhusu Mkataba huo.

Je, hii ni sahihi kwa mustakabali wa Ufanisi wa Soka letu.

Inawezekanaje Mdhamini wa Ligi awe ndo Mdhamini wa Timu Ndani ya Ligi na adhamini timu zaidi ya Mbili na ukihoji unatisihiwa kuchukuliwa hatua.

wananchi tushtuke.

PIa soma.


View attachment 2932503
huu mkataba ulishakufa zamani, simba tuliukataa. mabango yote ya gsm kila mechi yalikuwa yanaondolewa wanapoteza simba. iwe ugenini au nyumbani
 
Tatizo sio tff, Bali ni viongozi vilaza wa Simba . Hawajui nguvu na ukubwa wa Simba. Wameshindwa hata na Babra aliyehoji na kupinga waziwazi.
Wanashindwa kutambua wanaopaswa kuingia mkataba na wadhamini ni Bodi ya ligi, wanachaguliwa watu wa kuongoza Bodi ya ligi.
Bodi ya ligi ikiingia mkataba tff anatakiwa kupata asilimia 10 tu ya mapato lakini tff anachukua asilimia 20 lakini wamekata kimya. Waziri wa Sasa wa michezo aliwahi kuwapigania akaishia kufungiwa lakini huu ulikuwa wakati sahihi wa kudai haki zao.
 
Baada ya Malalamiko mengi ya Wadau kuhusu GSM kuwa na Udhamini wa Timu zaidi ya Sita kwenye Ligi ya NBC,na kufanya Mpira wetu kuwa na sintofahamu kwa sababu GSM pia ndiyo mdhamini wa timu ya Yanga..

baada ya Viongozi sa Simba kuhoji hilo Kwa TFF, TFF imekuja na Jibu kwamba hakuna anayeruhusiwa kuhoji kuhusu Mkataba huo.

Je, hii ni sahihi kwa mustakabali wa Ufanisi wa Soka letu.

Inawezekanaje Mdhamini wa Ligi awe ndo Mdhamini wa Timu Ndani ya Ligi na adhamini timu zaidi ya Mbili na ukihoji unatisihiwa kuchukuliwa hatua.

wananchi tushtuke.

PIa soma.


View attachment 2932503
Unataka tujadili mkataba wa 2021?
 
Back
Top Bottom