Nani aligharamia ukarabati wa kifahari wa ofisi ya Mkuu wa mkoa DSM?

Ukimjua aliyegharamia halafu wewe itakusaidia nini? Kwa mfano akiamua kutumia sehemu ya mshahara wake kwa ajili ya kununua computer au mapambo kuna shida? Acheni hizo.
Imegharimiwa na Ghalib Said Mohamed na ofisi yake, yaani GSM foundation, GSM- Msasani Mall, GSm pikipiki, GSM Magororo you name it. Na ndio hao waliogharamia lile zoezi lake la kupima afya mnazo mmoja lililoishia kuwa kituko, ndio waliolipia safari zake za marekani, Dubai nk na ndio waliogarimia safari yake ya hivi sasa ya South Afrika. Wanapata nini? kwanza wanapata mtu wa kushikilia iliyokuwa nafasi ya Ridhiwana katika kusimamia maslahi ya kifedhuli ya hii Yemen Group mfano, swala zima la Silent Ocean clearing agency iliyo wahi ku paralize port yetu, pamoja na makelele yote hawa mabwana wanaendelea na ile biashara kama ilivyokuwa hapo mwanzo. Kwa kupitia makonda tender zote za halmashauri zote za DSM kwa sasa ziko mikononi mwa hawa GSM. kwa wale mapumba wanaodai eti hakuna tatizo ni waganga njaa wasio na shule wanaoshindwa kujua madhara ya muingiliano wa serikali na matapeli hawa wakimataifa wanaosafisha pesa chafu. Kuna watu bado ndani ya CCM walioshikwa pabaya na huyu bwana kiasi kwamba wanalazimika kuwasimamia waendelee kuhujumu uchumi wetu. Kama hamuamini Usalama wa taifa watupe macho, lakini wawe watu wenye integrity wataona maana ukweli uko machoni kabisa. Kumbukeni wamepewa ardhi iliyokuwa na Tanu na kujenga just next to CCM lumumba. Hizo ofisi zao ni kama sebule ya viongozi wa chama, kunywa chai, kupewa posho n,k ni aibu kabisa na hii scope nawapa mwanahalisi na Jamhuri, maana ndio wanaume wa investigative reporting na hawana woga. Hawa ni kama bomba la ulaji la hao jamaa walio next to them.
 
Kwan ukarabati na uendeshwaji wa ofis upo chin ya nani,
Kitu kingine ni ulimbukeni ile sio ofis ya makonda ni ofis ya mkuu wa mkoa wa dar hata wewe ukiteuliwa utaitumia tu,aaaaaaaa 虛幻燈片頭曲子女兒園小區物業交付出國語翻倍晉寧澤犬吠影吠聲明顯瘦會員登錄界面陷阱電荷花人一下那小子彈琴日志文件旅行團體育課件事情不同了解決方案
 
Serikali ya Nyerere ndiyo ilitufungia kila kitu, hata chakula madukani ilikuwa mpaka uletewe na serikali, sijuwi ulikuwepo? Mwinyi akaja kubadili hayo na yote yakawa "ruksa". Kuanzia hapo umasikini wako ni wa kichwani mwako kwani baada ya Mwinyi tumeona mabilionea wa Kitanzania wakiibuka.

Wewe kimekushinda nini wenzako wameweza? Fikiri.
Kwahiyo Nyerere alikuwa TLP au aliwahi kuongoza serikali kupitia CHADEMA.?
Unaulizwa sufuria unajibu karai.

Kwa kuwa umeruka swali sasa labda tufanye hivi 50-2o = 30.
Kwahiyo miaka 30 ya uongozi "msafi" tena chini ya serikali hiyo hiyo ya CCM(kama unavyotaka tuamini) na uliofungulia kila kitu, Je Tanzania ni Masikini au sio masikini?
Kama bado ni masikini ni kwa nini?

Na Ashukuriwe Mungu, laiti kama Mwalimu Nyerere, angelithubutu kuanza kuchimba kila aina ya Madini yanayopatikana hapa nadhani kila lawama na jiwe angelirushiwa yeye.
Mwisho conclude na ule msemo wako pendwa................ Ujinga?
 
Picha zimekuwa zikisambaa kwenye mitandao kuonyesha ufahari wa hali ya juu wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa dar es salaam.

Ofisi hiyo imekuwa tofauti kabisa na ile ya Mkuu wa mkoa aliyepita bwana Sadick, ofisi ya Makonda ina kompyuta kadhaa za apple,mapambo mengi ya kila aina yanayoashiria ufahari na utukufu wa hali ya juu kuliko hata ofisi ya rais.

Nani aligharamia ufahari huu wakati hata ikulu haijabadili muonekano? Kulikuwa na umuhimu wa kuweka ufahari huo katika kipindi hiki cha kubana matumizi?
Nini kilipungua katika ofisi ya aliyekuwa Mkuu wa mkoa mpaka ufahari uongezwe katika jiji ambalo limezungukwa na wananchi wenye hali ngumu na maisha yasiyoridhisha.picha zaidi za ukarabati huu ziko instagram page ya. QUALITY HOMES

View attachment 348618
Ni GSM waligharamia kimya kimya kwa ahadi ya kuwatetea kwa mkulu wasidaiwe kodi za huko nyuma walizokwepa.
 
Hahahahahaaaaa. Yaani mmemtafuta Makonda mmemkosa. Sasa mnaanza kuwa na wivu na ofisi yake. Imewauma sana kuona Ofisi yake inakuwa na hadhi nzuri kuliko Ofisi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Mtaa wa Ufipa licha ya kupokea mamilioni ya fedha za ruzuku
Acha ujinga hakuna mwenye wivu na hiyo Ofisi bali watu wanataka kujua GSM alipata nini baada ya kuigharamia? je? Taratibu za kutangaza tenda zilifuatwa? Ofisi za chadema na Ofisi za makonda vina uhusiano gani? Kaa ukijua kuwa Wapinzani wa makonda kwa sasa ni CCM wengi kwani familia ya marehemu kabwe ni CCM wote, akina Manji na wengineo kibao wanataka kujua Ukweli wa Daud Albert kwa kila jambo hata Umtetee vipi safari hii hachomoki kamwe.
 
utadhani ataishi kwenye hiyo ofisi milele.
Katua jana South Africa kazuga zuga kidogo, Leo anapanda ndege kuelekea Gambia kwa Sangoma marufuku Duniani ambaye anaishi Msituni pembezoni mwa mto Gambia huko atakaa week kadhaa akifanya matambiko na kafara za kila Aina kwa sasa Daud Albert ni kigagula amepagawa anafanya vitu vya ajabu ajabu, jumapili alisali makanisa matatu tofauti huku BAKWATA wakishinda na kukesha kwake na sasa anaelekea kwa waganga sugu wa kienyeji ni hatari sana.
 
Kwahiyo Nyerere alikuwa TLP au aliwahi kuongoza serikali kupitia CHADEMA.?
Unaulizwa sufuria unajibu karai.

Kwa kuwa umeruka swali sasa labda tufanye hivi 50-2o = 30.
Kwahiyo miaka 30 ya uongozi "msafi" tena chini ya serikali hiyo hiyo ya CCM(kama unavyotaka tuamini) na uliofungulia kila kitu, Je Tanzania ni Masikini au sio masikini?
Kama bado ni masikini ni kwa nini?

Na Ashukuriwe Mungu, laiti kama Mwalimu Nyerere, angelithubutu kuanza kuchimba kila aina ya Madini yanayopatikana hapa nadhani kila lawama na jiwe angelirushiwa yeye.
Mwisho conclude na ule msemo wako pendwa................ Ujinga?

Nyerere alipokuwepo madarakani alifuta vyama vyote vya upinzani na kubakisha chama kimoja tu, TANU. Kilichoasisiwa na wazee waliompokea Dar (siku hizo walikuwa vijana) akina Abdul Wahid Sykes, Dossa, na wengine wengi.

Kwa hiyo kuuliza kama wakati wa utawala wa Nyerere kulikuwa na TLP ni ujinga huo.

Swali sijaruka, nimekujibu uhalisia wa umasikini ulipoanzia. Wakati wa Nyerere Tanzania ilikuwa ni nchi masikini zaidi duniani kuliko zote. Leo hatuko huko.

Leo hii ukiwa kijana na hauna tatizo lolote la kiafya na unalialia kuwa u masikini basi utakuwa na tatizo kichwani mwako au ni mvivu wa kutupwa.
 
Namuunga mkono Makonda kunadorisha office...office nyingi za umma zinatia aibu chafu na kila kitu cha kizamani...hazina hata motisha wa kufanyia kazi humo
.
Ni wenye akili za aina yako pekee watakuunga mkono, ila tambua ofisi za srikali zina fungu maalumu la ukarabati ,swali iweje iwe ya mkuu wa mkoa pekee wakati kuna za wilaya ndani bado zikiwa kuu kuu na je! Kwanini iwe moja tu kati ya mikoa na majiji yote nchini? Huo ndio mzizi hasa wa swali, maana serikali iko kwenye kuondoa matumizi yote yasiyo lazima ili kubana matumizi sasa kulikuwa na ulazima wowote wa msingi kufanya marekebisho hayo na kwa kiasi hicho na kwa wakati huu wa kauli mbiu ya kubana matumizi??
 
Maswali mengi humu ni ya kuchosha na yana harufu ya chuki binafsi. Huyu bwana tunamtambua kwa uwezo wake mkubwa wa kumobilize resources kwahiyo kuhoji pesa za ukarabati ni aina nyingine ya mawazo finyu
 
Nani asiyependa kufanya kazi ktk mazingira mazuri?? Hlf mtu unakuja kuuliza Nani aliyekarabati? Nani aliyepaoendezesha?? Sasa hizi Ni chuki binafsi... Kitu cha kutambua kuwa hela zote za marekebisho ya utendaji kazi kimkoa zinatoka mkoani hapo hapo... Akili na mbinu (creativity) ndo hutumika zaidi ofisi yako iweje kutoka ktk hizo hizo hela zinazotoka mkoani hapo ndo Maana unaona ofisi km hiyo inakuwa Safi na inapendeza, this is dar es salaam bana, sasa unataka ofisi yake ilingane na wengine za huko mkoani??? Nah. Nafikiri wa mkoani ndo wanatakiwe waige kitu kizuri kutoka Kwa mkuu WA mkoa wa Dar... Km hii ya ofisi yake. Na kuna vitu vingine si vya kumtupia lawama tuuuuu sababu ya maeneo mengine ambayo Watu mnamuhisi vibaya... Big up RC na mkoa WA Dar, ofisi inatakiwa iwe smart Kwa kila kitu, kuanzia watu mpk vitendea kazi. N u will be comfortable. Kwa maoni yangu, natamani ofisi zote za serikalin ziwe nzuri na vitendea kazi vya kisasa km hizo.... Maana sisi wabongo tunapenda kuona vitu vibaya tutoe kasoro na Kuzomea na kikiwa kizuri badala ya kusifia mna-questions kwanza, this is 21th century bn technologia inatu shape, utake usitake Kubadilika lazima
 
Katua jana South Africa kazuga zuga kidogo, Leo anapanda ndege kuelekea Gambia kwa Sangoma marufuku Duniani ambaye anaishi Msituni pembezoni mwa mto Gambia huko atakaa week kadhaa akifanya matambiko na kafara za kila Aina kwa sasa Daud Albert ni kigagula amepagawa anafanya vitu vya ajabu ajabu, jumapili alisali makanisa matatu tofauti huku BAKWATA wakishinda na kukesha kwake na sasa anaelekea kwa waganga sugu wa kienyeji ni hatari sana.

uwii huyu anaenda kujiongeza mikosi.
 
Nyerere alipokuwepo madarakani alifuta vyama vyote vya upinzani na kubakisha chama kimoja tu, TANU. Kilichoasisiwa na wazee waliompokea Dar (siku hizo walikuwa vijana) akina Abdul Wahid Sykes, Dossa, na wengine wengi.

Kwa hiyo kuuliza kama wakati wa utawala wa Nyerere kulikuwa na TLP ni ujinga huo.

Swali sijaruka, nimekujibu uhalisia wa umasikini ulipoanzia. Wakati wa Nyerere Tanzania ilikuwa ni nchi masikini zaidi duniani kuliko zote. Leo hatuko huko.

Leo hii ukiwa kijana na hauna tatizo lolote la kiafya na unalialia kuwa u masikini basi utakuwa na tatizo kichwani mwako au ni mvivu wa kutupwa.

Kwa hiyo wewe hapo ni tajiri??
 
Kwa hiyo wewe hapo ni tajiri??

Neno tajiri linatokana na neno tijara, biashara. Tajiri maana yake ni mfanya biashara, kwa maana hiyo, naam, Mimi ni tajiri sana tena sana kwa kuwa biashara ni jadi yangu na nimejiingiza kwenye biashara nyingi sana, kuanzia majumba ya kupangisha, kilimo, ufugaji na kuwekeza hapa na pale.
 
Neno tajiri linatoka na neno tijara, biashara. Tajiri maana yake ni mfanya biashara, kwa maana hiyo, naam Mimi ni tajiri sana tena sana kwa kuwa biashara ni jadi yangu na nimejiingiza kwenye biashara nyingi sana, kuanzia majumba ya kupangisha, kilimo, ufugaji na kuwekeza hapa na pale.
Bi mkubwa naona uko vizuri sana katika mas-ala ya balagha
 
Back
Top Bottom