Asha Abdala
JF-Expert Member
- Mar 21, 2007
- 1,130
- 44
Baada ya Kafulila kuondoka chamani kwenda kwenye NCCR Mageuzi ambayo Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe aliwahi kukitaja humu kwamba kilipewa fedha za EPA kuhujumu majimbo ambayo CHADEMA ilikuwa na nguvu mwaka 2005, nimejikuta nakumbukia uchaguzi wa mwaka 2005.
Nakumbuka mwaka huo palikuwa na mgombea mdogo kuliko wote alitoka mara moja tu katika gazeti moja la kila wiki, na baada ya uchaguzi sijamsikia tena mara kwa mara. Huyu kijana picha yake niliyoiona gazetini ilikuwa handsome sana, natamani nimuone uso kwa uso!.
Hivi karibuni nilisoma akitajwa kwenye gazeti la Hoja takribani mwezi mmoja kabla ya Kafulila kutimka mwenywe CHADEMA. Gazeti hilo lilimnukuu Kafulila akisema kwamba kuna makundi ndani ya CHADEMA ambayo yamesababisha chama kugawanyika hata kwenye kuteua wagombea. Habari hiyo ilimnukuu Kafulila akisema kwamba hali hiyo imedhihirika katika jimbo la Kigoma Kusini. Alisema kwamba kuna Kambi ya Zitto, ambayo inamtaka yeye awe mgombea, kambi ambayo ni ya vijana wengi nchi nzima na inawakilisha kundi la watanzania wa kawaida.
Kafulila alinukuliwa akisema kwamba kundi la pili ni kambi ya Mbowe na Dr Slaa ambayo ni ya wazee na matajiri ambayo ina mtaka mjumbe wa bodi ya wadhamini wa chama hicho kijana Muslim Hassanal ndio awe mbunge wa jimbo hilo.
Kafulila aliendelea kusema kundi hilo, ndio limemfadhili Muslim kwenda Kigoma kutimiza moja ya ahadi zake za mwaka 2005 aliyoitoa kwamba atahakikisha kila zahanati inapata magodoro, achaguliwe au asichaguliwe. Inadaiwa kwamba Muslim ambaye ni mmoja wa wafanyabiashara vijana alitoa ahadi katika sekta mbalimbali ambazo zote alisema hata akishindwa ubunge angezitimiza kabla ya uchaguzi ujao.
Madai hayo yalijitokeza kabla ya uchaguzi wa serikali za mitaa, na Kafulila akadai pia kuwa Muslim anafanya hivyo ili CHADEMA ikishinda Vijiji vya Kigoma Kusini ionekane yeye ndio amechangia.
Nisaidieni jamani, namtafuta "Mbunge" Muslim Hassanal. Nimejaribu ku-google search habari pekee ambayo naona imemtaja ni http://www.habaritanzania.com/new/articles/3113/1/-Mawaziri-wa-Mkapa-wapeta-majimboni
Niliposoma habari hii nikakumbuka jina la Kiffu aliyekuwa NCCR Mageuzi ambaye chama kule kilikuwa ni yeye na yeye ndio chama, matokeo yake uamuzi wake wa kuhama kwenda CCM mara baada ya uchaguzi ukakigawa chama hicho vipande vitatu. Kipande kimoja akaenda nacho CCM, kipande kingine kikaenda CHADEMA, kipande kimoja kilibaki NCCR; ndio hiki alichonacho Kafulila hivi sasa.
Matokeo yake ni NCCR ambayo ilipata vijji vingi kuliko CHADEMA mwaka 2004, na kura nyingi kiasi kuliko CHADEMA mwaka 2005; kupata viti vichache na kura chache kuliko CHADEMA mwaka 2009. Hali ambayo imefanya rasmi CHADEMA kuwa chama mbadala wa CCM Kigoma Kusini badala ya aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo kupitia NCCR kurejea CCM.
'Mbunge' Muslim Hassan ni vizuri akajitokeza wakati huu kwa kuwa gazeti la Mwananchi ambalo awali lilikuwa linaipa nafasi CHADEMA kushinda Kigoma Kusini kupitia kwa Kafulila sasa limebadili Kauli yake na kuandika habari za kiuchambuzi kuwa NCCR Mageuzi ndio itayoshinda baada ya Kafulila kuhamia chama hicho.
Tukiweza kumpata Muslim Hassanal, tutaweza kuwafanya Mwananchi wakawapambanisha na Kafulila; CHADEMA na NCCR ili watanzania tujue yupi hasa ni mbadala wa kweli wa CCM Kigoma Kusini na kote nchini.
Asha
Nakumbuka mwaka huo palikuwa na mgombea mdogo kuliko wote alitoka mara moja tu katika gazeti moja la kila wiki, na baada ya uchaguzi sijamsikia tena mara kwa mara. Huyu kijana picha yake niliyoiona gazetini ilikuwa handsome sana, natamani nimuone uso kwa uso!.
Hivi karibuni nilisoma akitajwa kwenye gazeti la Hoja takribani mwezi mmoja kabla ya Kafulila kutimka mwenywe CHADEMA. Gazeti hilo lilimnukuu Kafulila akisema kwamba kuna makundi ndani ya CHADEMA ambayo yamesababisha chama kugawanyika hata kwenye kuteua wagombea. Habari hiyo ilimnukuu Kafulila akisema kwamba hali hiyo imedhihirika katika jimbo la Kigoma Kusini. Alisema kwamba kuna Kambi ya Zitto, ambayo inamtaka yeye awe mgombea, kambi ambayo ni ya vijana wengi nchi nzima na inawakilisha kundi la watanzania wa kawaida.
Kafulila alinukuliwa akisema kwamba kundi la pili ni kambi ya Mbowe na Dr Slaa ambayo ni ya wazee na matajiri ambayo ina mtaka mjumbe wa bodi ya wadhamini wa chama hicho kijana Muslim Hassanal ndio awe mbunge wa jimbo hilo.
Kafulila aliendelea kusema kundi hilo, ndio limemfadhili Muslim kwenda Kigoma kutimiza moja ya ahadi zake za mwaka 2005 aliyoitoa kwamba atahakikisha kila zahanati inapata magodoro, achaguliwe au asichaguliwe. Inadaiwa kwamba Muslim ambaye ni mmoja wa wafanyabiashara vijana alitoa ahadi katika sekta mbalimbali ambazo zote alisema hata akishindwa ubunge angezitimiza kabla ya uchaguzi ujao.
Madai hayo yalijitokeza kabla ya uchaguzi wa serikali za mitaa, na Kafulila akadai pia kuwa Muslim anafanya hivyo ili CHADEMA ikishinda Vijiji vya Kigoma Kusini ionekane yeye ndio amechangia.
Nisaidieni jamani, namtafuta "Mbunge" Muslim Hassanal. Nimejaribu ku-google search habari pekee ambayo naona imemtaja ni http://www.habaritanzania.com/new/articles/3113/1/-Mawaziri-wa-Mkapa-wapeta-majimboni
Niliposoma habari hii nikakumbuka jina la Kiffu aliyekuwa NCCR Mageuzi ambaye chama kule kilikuwa ni yeye na yeye ndio chama, matokeo yake uamuzi wake wa kuhama kwenda CCM mara baada ya uchaguzi ukakigawa chama hicho vipande vitatu. Kipande kimoja akaenda nacho CCM, kipande kingine kikaenda CHADEMA, kipande kimoja kilibaki NCCR; ndio hiki alichonacho Kafulila hivi sasa.
Matokeo yake ni NCCR ambayo ilipata vijji vingi kuliko CHADEMA mwaka 2004, na kura nyingi kiasi kuliko CHADEMA mwaka 2005; kupata viti vichache na kura chache kuliko CHADEMA mwaka 2009. Hali ambayo imefanya rasmi CHADEMA kuwa chama mbadala wa CCM Kigoma Kusini badala ya aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo kupitia NCCR kurejea CCM.
'Mbunge' Muslim Hassan ni vizuri akajitokeza wakati huu kwa kuwa gazeti la Mwananchi ambalo awali lilikuwa linaipa nafasi CHADEMA kushinda Kigoma Kusini kupitia kwa Kafulila sasa limebadili Kauli yake na kuandika habari za kiuchambuzi kuwa NCCR Mageuzi ndio itayoshinda baada ya Kafulila kuhamia chama hicho.
Tukiweza kumpata Muslim Hassanal, tutaweza kuwafanya Mwananchi wakawapambanisha na Kafulila; CHADEMA na NCCR ili watanzania tujue yupi hasa ni mbadala wa kweli wa CCM Kigoma Kusini na kote nchini.
Asha