gfsonwin
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 18,274
- 20,673
Wewe ni mama ama binti ambaye umeolewa ma una mchumba, katika kuish kwenu najua kabisa kuna kukoseana kwa hapa na pale. Je wewe unapokosea wajua jinsi ya kukiri kosa na kuomba msamaha? je watanguliza ubabae na mdomo wa kama chiriku ama unayaona na unakubali makosa yako? Je panapo kuyaona na kuyakubali je wachukua hatua gani zaid?
soma hapa:
1)Ona kosa lako kabisa kisha jiweke kwenye nafasi ya mwenzako iwe kama wewe ndo umetendewa.
2)Ona na dadavua athari za kosa lenyewe kabla hata hajakuambia ili uweze kufikiri njia sahihi ya kupata suluhu.
3) kwa upole kabisa unapoambiwa kwamba umekosea usikasirike wala kupandisha hasira, tulia msikilize hadi amalize, wala usianze kulia kama njia ya kujihami ama kuropoka maneno makali( hili linawahusu akina dada)
4)Onyesha kwamba umeyatambua makosa yako kihisia na hata kwa kusema kisha taja suluhu kwako wataka iwe ni nini.
5)wakati wa kutoa suluhu jiweke kwenye nafasi ya mwenzi wako isiwe kitu ambacho kitamuumiza mwenzio bali kiwe ni kile ambacho kitawanufaisha.
6)umesha tambua kosa, umelielezea, ukasema wataka suluhu ya jambo iwe nini, basi omba msamaha hata kama atasema hasamei kwa wakati huo wewe omba.
7) usiyaweke maneno ambayo mwenzi wako anaweza kuwa anayasema moyoni kwa wakati huo manake mengine yawezekana yakawa yanamtoka kwa hasira tu. Ila weweuwe mpole wala usimbughudhi kwa lolote lile hadi moyo wake utulie.
8)silaha kubwa sana kwa mama wakati wa kkukiri na kuomba msamaha hasa panapo makosa makubwa basi iwe ni upole na unyenyekevu wala isiwe maneno ya kuropoka na jeuri ama kashfa.
9) kwa kujua upendo wa mwenzi wako kwako basi ni busara kabisa ukampa muda wa yeye kusahau hapa waweza kumuomba akupe ruhusa uende kwenu kidogo ili aone kama bado anaweza kukuhitaj.
10) mwombe Mungu sana wala usitangaze kwa watu manake Mungu anasema katika zab 62:1-2 kwamba umngoje bwana kwa kimya na yeye atakuwa mwamba wako hutatikisika sana.
hitimisho njia hii siyo lazima ikafanya kazi kwa kila mtu ila kwa wewe mwanamke mwenzangu najua itakusaidia.
kwaharini bana niko fungateni nitarudi tena kujibu hoja zenu. ila nikimaliza funngate nakuja na bandiko kali la wababa manake nimejifunza mengi nilipo huku.
soma hapa:
1)Ona kosa lako kabisa kisha jiweke kwenye nafasi ya mwenzako iwe kama wewe ndo umetendewa.
2)Ona na dadavua athari za kosa lenyewe kabla hata hajakuambia ili uweze kufikiri njia sahihi ya kupata suluhu.
3) kwa upole kabisa unapoambiwa kwamba umekosea usikasirike wala kupandisha hasira, tulia msikilize hadi amalize, wala usianze kulia kama njia ya kujihami ama kuropoka maneno makali( hili linawahusu akina dada)
4)Onyesha kwamba umeyatambua makosa yako kihisia na hata kwa kusema kisha taja suluhu kwako wataka iwe ni nini.
5)wakati wa kutoa suluhu jiweke kwenye nafasi ya mwenzi wako isiwe kitu ambacho kitamuumiza mwenzio bali kiwe ni kile ambacho kitawanufaisha.
6)umesha tambua kosa, umelielezea, ukasema wataka suluhu ya jambo iwe nini, basi omba msamaha hata kama atasema hasamei kwa wakati huo wewe omba.
7) usiyaweke maneno ambayo mwenzi wako anaweza kuwa anayasema moyoni kwa wakati huo manake mengine yawezekana yakawa yanamtoka kwa hasira tu. Ila weweuwe mpole wala usimbughudhi kwa lolote lile hadi moyo wake utulie.
8)silaha kubwa sana kwa mama wakati wa kkukiri na kuomba msamaha hasa panapo makosa makubwa basi iwe ni upole na unyenyekevu wala isiwe maneno ya kuropoka na jeuri ama kashfa.
9) kwa kujua upendo wa mwenzi wako kwako basi ni busara kabisa ukampa muda wa yeye kusahau hapa waweza kumuomba akupe ruhusa uende kwenu kidogo ili aone kama bado anaweza kukuhitaj.
10) mwombe Mungu sana wala usitangaze kwa watu manake Mungu anasema katika zab 62:1-2 kwamba umngoje bwana kwa kimya na yeye atakuwa mwamba wako hutatikisika sana.
hitimisho njia hii siyo lazima ikafanya kazi kwa kila mtu ila kwa wewe mwanamke mwenzangu najua itakusaidia.
kwaharini bana niko fungateni nitarudi tena kujibu hoja zenu. ila nikimaliza funngate nakuja na bandiko kali la wababa manake nimejifunza mengi nilipo huku.