Namkumbuka Marehemu Mwivano Kupaza aliyeuwawa na kaka yake Peter Kupaza

Ukwaju

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
13,370
11,090
Jamani samahanini sana wale wa miaka ya nyuma kuna jamaa km sikosei anatokea Mkoa wa Tanga alikuwa USA Wiscosin akamuagiza dada yake aende huko, akatembea naye (akambaka) walipoitoa mimba, Binti Mwivano akafariki (sijui aliuawa) Kaka mtu akamtenganisha na kwenda kumtupa mtoni, wapelelezi wa huko wakagundua tukio zima na kumhukumu. Alikata rufaa (Bw Kupaza) kuwa sio yeye je alitoka na yupo wapi siku hizi?
 
Lushoto-Tanga, ile kesi ilikua full utata kwani baadhi ya ndg zake walichukuliwa kwenda kutoa ushahidi na wote walikiri kuwa enzi za utoto wake jamaa hakuweza hata kuchinja kuku, so kusema alimcharanga dadake ilikua haingii akilini, ila jamaa alioa mwanamke wa kizungu ambaye hakua radhi jamaa kua na huyu dadaake!! ndio ninayokumbuka! labda uingie kwenye google
 
Sakata zima liliwekwa kwenye channel ya Crime and Investigation. Yaani yule jamaa alikuwa anafanya kazi butchery na vile alivyomcharanga, suspicion ya kwanza ilikwenda kwa watu wa aina hiyo kwani jinsi alivyocharangwa ilikuwa very clean ambayo kwa mtu wa kawaida asingeweza kufanya hivyo.

Yule binti alimweleza wifi yake issue ya 'kaka' kumtamani, na kulikuwa na misunderstanding. Baadae yule wife alihama nyumbani na ndiyo hayo mauaji yalitokea baada ya muda fulani. Kwa vile uso ulikuwa umeharibika walitumia sculptors (nadhani ndiyo jina lao) kutengeneza aina ya uso ambao marehemu angekuwa nao. Walipotangaza tu kwenye tv yule exwife alikisia kwamba ni wifi yake na alikwenda kuripoti polisi.

Polisi walifuatilia hiyo kesi na yule jamaa alipoulizwa alisema Mwivano amerudi nyumbani Tanzania, ndipo walipofuatilia hadi kwa wazee wake Tz na kuona kwamba wazee hawana habari na walidhania bado mtoto wao yuko marekani.

Kesi iliendelea na mwisho yule jamaa nadhani alihukumiwa kifungo cha maisha.

Niliiona hiyo kwenye channel hiyo na nilikuwa interested kuangalia kwa vile ilihusu Tz.
 
Aisee kesi ya zamani hii,sikumbuki gazeti lipi la hapa nyumbani lakini nakumbuka picha yake huyo msichana ilishika kurasa za mbele za gazeti hilo.
 
Mwivano aliuwawa mwaka 1999. Story yake ilisikitisa na bado inasikitisha. she was only 25. Peter Kupaza alimuua huyu dada yake na ilichukua muda wa miezi sita kujulikana kwamba mabaki yalikuwa ya Mwivano maana kwa jinsi alivyomchuna ngozi kwa ustadi mkubwa ilikuwa ngumu kujulikana mpaka walipopeleka kwa mtu wa ku-reconstruct sura. Miguu yake haikuwahi kupatikana.

Yawezekana hata huyu Peter alitumia cutting board kuchuna kichwa chake maana sniffer dog ali-detect damu ya mwanadamu kwa visu vya jikoni cutting board na bafuni.

Story inasikitisha kwa kweli. Lakini ki ufupi Peter Kupaza kafungwa maisha. waweza ku google murdered Mwivano of Tanzania itakuletea mengi mno ya tukio zima.
 
Sakata zima liliwekwa kwenye channel ya Crime and Investigation. Yaani yule jamaa alikuwa anafanya kazi butchery na vile alivyomcharanga, suspicion ya kwanza ilikwenda kwa watu wa aina hiyo kwani jinsi alivyocharangwa ilikuwa very clean ambayo kwa mtu wa kawaida asingeweza kufanya hivyo.

Yule binti alimweleza wifi yake issue ya 'kaka' kumtamani, na kulikuwa na misunderstanding. Baadae yule wife alihama nyumbani na ndiyo hayo mauaji yalitokea baada ya muda fulani. Kwa vile uso ulikuwa umeharibika walitumia sculptors (nadhani ndiyo jina lao) kutengeneza aina ya uso ambao marehemu angekuwa nao. Walipotangaza tu kwenye tv yule exwife alikisia kwamba ni wifi yake na alikwenda kuripoti polisi.

Polisi walifuatilia hiyo kesi na yule jamaa alipoulizwa alisema Mwivano amerudi nyumbani Tanzania, ndipo walipofuatilia hadi kwa wazee wake Tz na kuona kwamba wazee hawana habari na walidhania bado mtoto wao yuko marekani.

Kesi iliendelea na mwisho yule jamaa nadhani alihukumiwa kifungo cha maisha.

Niliiona hiyo kwenye channel hiyo na nilikuwa interested kuangalia kwa vile ilihusu Tz.


Hicho kipindi kimerusdiwa tena leo! Sad!
 
Duuu kipindi hicho tulikuwa Sekondari nakumbuka kuna jamaa yetu tulikuwa tulimpa jina la utani Kupaza kutokana na hii kesi
 
Alipatikana na hatia na alihukumiwa kifo alichomwa sindano ili onyeshwa kwenye luninga nakumbuka nika ma. Mwaka 1998
 
Lol,tunawezaje pata documentary ya hyo mambo,duh tulikuwa tumetia aibu kwakweli....
 
...Kwa nini tunaamini kuwa Kupaza ndio alifanya Unyama huo?? Kwa nini tusidhani kuwa labda mke wake baada ya kusikia kuwa Kupaza anamnyemelea pia mdogo wao akaamua kufanya 'Action' ya 'kuuwa' ndege wawili kwa jiwqe moja????
 
...Kwa nini tunaamini kuwa Kupaza ndio alifanya Unyama huo?? Kwa nini tusidhani kuwa labda mke wake baada ya kusikia kuwa Kupaza anamnyemelea pia mdogo wao akaamua kufanya 'Action' ya 'kuuwa' ndege wawili kwa jiwqe moja????

Kutokana na alivyocharangwa very neatly ndiyo wahusika wa kwanza walikuwa ni wale wenye ujuzi wa kukata nyama butchery. Na Kupaza alikuwa na ujuzi huo.

Muuaji wa kawaida ambaye siyo mzoefu yeye atacharanga vyo vyote tu.
 
Nimejaribu kuseach nikakutana na uzi huu watu walisha udiscuss sana hapa [https://www.jamiiforums.com/mahusiano-mapenzi-urafiki/237174-je-ni-kupaza-aliyemuua-mwivano-upande-wa-pili-wa-shilingi-4.html] [/url]

Usikuwa wa leo mke wangu hakupata usingizi mzuri iliopofika saa 11 asubihi akawa anapitia JF akakutana na thead kama hii baada ya kuiona tu akaniambia kuwa JF leo wameweka tread ya Peter ana Mwivano kisa ambacho kilitokea miaka iliyopita ikawa guzo sana kwenye vyombo vya habari vya hapa nchini na marekani kulipotokea kisa hicho.

Nakumbuka awali 2009 mke wangu aliwahinionyesha picha ya Peter na Mwivano ( Kwani wanaundugu) kabla ya kwenda marekani pia alinionyesha picha za mazishi ya Mwaivano huko Marekani, pia alinisimulia kisa hicho kilivyokuwa lakini sikuwapata muda wa kulichukulia sana kwa uzito kwani pindi hiyo nilikuwa na mambo mengi sana ya kikazi hivyo sikupata muda sana wa kuhoji zaidi ya kumwambia kisa hiki nilikifuatilia kwenye magazeti muda sasa lakini sikuweza kuunganisha dots vizuri.

Cha kushangaza kabisa leo nikaamua kugoogle kikamilivu ndiyo nikakutana na hii story hapa JF kwa undani what exactly happened, Ni meazimia kukutana na familia za wahusika wa pande mbili kama itakuwa baraka upande wao huenda nikaweka hapa kujua updates zaidi.

Aksante sana wan JF kwani hapa ni zaidi ya mtandao wa kijamii.
 
...Kwa nini tunaamini kuwa Kupaza ndio alifanya Unyama huo?? Kwa nini tusidhani kuwa labda mke wake baada ya kusikia kuwa Kupaza anamnyemelea pia mdogo wao akaamua kufanya 'Action' ya 'kuuwa' ndege wawili kwa jiwqe moja????

Hata mimi nimepata mawazo kama hayo yako. Kulingana na maelezo ya hii kesi aliyeripoti kwamba Peter ndie anaweza kuwa ameua ni huyo xwife wa Peter. Halafu, kama hawa watu (Peter na nduguye) walikua wapenzi (waliokubaliana) tofauti na maelezo kwamba alikua anambaka, na hata kwenye form ya abortion iliyopatikana hospitalini aliisaini marehemu. Kwa nini Peter amuue?
Huyu mwanamke alijua kazi ya Peter alokua anafanya (kwa maelezo yake amesema hata Peter ashawahi kumweleza jinsi ya kukata nyama na kuchuna ngozi kwa ustadi), na aliujua huu uhusiano, hakuna uwezekano wa yeye kuzunguka hapa na kuwakomoa wote? Kinachonipa wasiwasi zaidi ni roho ya kukata rufaa aliyo nayo Peter, kama kweli yeye ndiye muuaji basi ana roho kama jiwe.
 
Alipatikana na hatia na alihukumiwa kifo alichomwa sindano ili onyeshwa kwenye luninga nakumbuka nika ma. Mwaka 1998

Hapa alihukumiwa kifungo cha maisha ila itapata parole baada ya kutumikia miaka 31 kama akiontesha tabia njema, jua kuwa alihukumiwa akiwa na miaka 40 hivi huvyo akipata parole atakuwa na miaka 71 hivi.
 
Kwa wale ambao wanawajua wanawake wa kimarekani huenda wakawa na mtazamo tofauti kidogo.

Napata hisia Ross ndiye alikuwa muhusika na aliapnga tukio hili kwa ustadi mkubwa akijua tabia ya mtalaka wake na ross alijua mahusiano na dada yake yainaweza kumpoint Kupaza moja kwa moja na yule jamaa mwanaume wa kizungu ayeuona kwanza mfuko wenye mwili huku akisikitika kwenye mto wa wascosin na kumwambia yule mama alikuwa na familia na marafiki piknic ndiye alitekeleza mpango huo
 
Lol,tunawezaje pata documentary ya hyo mambo,duh tulikuwa tumetia aibu kwakweli....
Angalia Zuku kuna channel inayohusu makala za uharifu,na wahalifu wanavyofuatiliwa hadi kudakwa
 
Kwa wale ambao wanawajua wanawake wa kimarekani huenda wakawa na mtazamo tofauti kidogo.

Napata hisia Ross ndiye alikuwa muhusika na aliapnga tukio hili kwa ustadi mkubwa akijua tabia ya mtalaka wake na ross alijua mahusiano na dada yake yainaweza kumpoint Kupaza moja kwa moja na yule jamaa mwanaume wa kizungu ayeuona kwanza mfuko wenye mwili huku akisikitika kwenye mto wa wascosin na kumwambia yule mama alikuwa na familia na marafiki piknic ndiye alitekeleza mpango huo
Wabeba box kaeni chonjo na hao wanawake wenu wa kufikia ,wengine hujisahau kabisa ,na hatimaye wanaporudishwa hubaki kulaumu ndugu kuwa hawawajali wanapokabiliwa na msongo wa mawazo na maisha
 
123.PNG 456.PNG 789.PNG
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom