Onambali
Member
- Mar 11, 2011
- 67
- 10
- Thread starter
- #41
Wana JF,
Nawasalimu.
Kwa wale mnaokumbuka kwamba nimetangaza nia yangu ya dhati ya kuomba ridhaa ya wananchi ili kuwa rais (mtumishi) wa Tz mwaka 2030. Nashukuru kwa kuwa wengi hasa wa hapa jamvini wameunga mkono nia yangu hiyo na wametoa ushauri makini. Nawashukuru sana.
Ndugu wana JF,
Baadhi ya watu wamehoji kwamba 2030 ni mbali sana na kwa nini nitangaze nia yangu sasa. Jibu langu ni hili hapa.
Kupata kiongozi mzuri si jambo la mzaha na halihitaji kukurupuka. Rais wa kwanza wa TZ hayati JK Nyerere aliwahi kusema 'ikulu ni pa kuogopwa kama ukoma...., pia alisema..kwa mtu msafi kabisa, ikulu sio mahali pa kukimbilia'. Inawezekana alitoa kauli hizi baada ya kuona dhuluma na ukiukaji wa taratibu unaoendelea katika eneo la uongozi katika Tz. Hivyo kama rais mtarajiwa niwezaye kuona ugumu na gharama ya uamuzi nitakaouchukua, lazima nianze mapema kujiandaa ili nitakapoingia ikulu ni pafanye mahali huru ambapo 'ukoma' haupo tena, badala yake ikulu pawe nyumbani pa kila mtanzania na sio pa wachache yaani mafisadi.
Ndugu zangu, nchi ikiwa na viongozi wabovu huendelea kuwa maskini. Mfano, kilichosababisha Mexico iwe maskini ingawa ina rasilimali kadhaa iko karibu eneo moja kijiografia na Marekani (ambayo inahesabika kuwa nchi tajiri duniani) ni tofauti ya kimisingi, mitazamo na mipango ambayo huwa miongoni mwa mambo ya msingi yanayotofautisha 'viongozi kutoka kwa watawala'. Kuna uwezekano mkubwa kiongozi akawa mtawala pia, ila sio kila mtawala huwa kiongozi.
Wana Jf,
Nimetangaza nia yangu hii mapema sio kwa mzaha ili kwa nia ya dhati ambayo nimeamua sio tu kwa sababu ni haki yangu kama raia wa Tz, ila kwa sababu naamini nina uwezo (kwa msaada wa Mungu) wa kujenga Tz yenye watu wazalendo, wanaoheshimiana, wasiodhulumiana, wanaotenda haki, wanaochukia rushwa, wanaopenda kufanya kazi, waliokombolewa kifikra na watakaojivunia utaifa wao usiku na mchana hivyo kulinda heshima ya nchi yao na kutumia rasilimali za nchi yao katika njia endelevu kwa manufaa ya nchi vizazi hata vizazi. Kazi hii sio lelemama, inahitaji vitendo badala ya maneno matupu ambayo wahenga wanasema 'hayavunji mfupa'. Kazi hii pia inahitaji mtu msafi aliyeanza kufahamu jambo hilo kabla ya kunajisika ili ajijenge katika usafi huo na hatimaye atumie usafi wake huo kurekebisha na kuondoa uchafu ndani na kwenye kingo za uongozi nchini TZ.
Wana JF,
Leo naishia hapa, maoni yenu yana thamani kubwa sana, karibuni kwa maoni zaidi.
Nawasalimu.
Kwa wale mnaokumbuka kwamba nimetangaza nia yangu ya dhati ya kuomba ridhaa ya wananchi ili kuwa rais (mtumishi) wa Tz mwaka 2030. Nashukuru kwa kuwa wengi hasa wa hapa jamvini wameunga mkono nia yangu hiyo na wametoa ushauri makini. Nawashukuru sana.
Ndugu wana JF,
Baadhi ya watu wamehoji kwamba 2030 ni mbali sana na kwa nini nitangaze nia yangu sasa. Jibu langu ni hili hapa.
Kupata kiongozi mzuri si jambo la mzaha na halihitaji kukurupuka. Rais wa kwanza wa TZ hayati JK Nyerere aliwahi kusema 'ikulu ni pa kuogopwa kama ukoma...., pia alisema..kwa mtu msafi kabisa, ikulu sio mahali pa kukimbilia'. Inawezekana alitoa kauli hizi baada ya kuona dhuluma na ukiukaji wa taratibu unaoendelea katika eneo la uongozi katika Tz. Hivyo kama rais mtarajiwa niwezaye kuona ugumu na gharama ya uamuzi nitakaouchukua, lazima nianze mapema kujiandaa ili nitakapoingia ikulu ni pafanye mahali huru ambapo 'ukoma' haupo tena, badala yake ikulu pawe nyumbani pa kila mtanzania na sio pa wachache yaani mafisadi.
Ndugu zangu, nchi ikiwa na viongozi wabovu huendelea kuwa maskini. Mfano, kilichosababisha Mexico iwe maskini ingawa ina rasilimali kadhaa iko karibu eneo moja kijiografia na Marekani (ambayo inahesabika kuwa nchi tajiri duniani) ni tofauti ya kimisingi, mitazamo na mipango ambayo huwa miongoni mwa mambo ya msingi yanayotofautisha 'viongozi kutoka kwa watawala'. Kuna uwezekano mkubwa kiongozi akawa mtawala pia, ila sio kila mtawala huwa kiongozi.
Wana Jf,
Nimetangaza nia yangu hii mapema sio kwa mzaha ili kwa nia ya dhati ambayo nimeamua sio tu kwa sababu ni haki yangu kama raia wa Tz, ila kwa sababu naamini nina uwezo (kwa msaada wa Mungu) wa kujenga Tz yenye watu wazalendo, wanaoheshimiana, wasiodhulumiana, wanaotenda haki, wanaochukia rushwa, wanaopenda kufanya kazi, waliokombolewa kifikra na watakaojivunia utaifa wao usiku na mchana hivyo kulinda heshima ya nchi yao na kutumia rasilimali za nchi yao katika njia endelevu kwa manufaa ya nchi vizazi hata vizazi. Kazi hii sio lelemama, inahitaji vitendo badala ya maneno matupu ambayo wahenga wanasema 'hayavunji mfupa'. Kazi hii pia inahitaji mtu msafi aliyeanza kufahamu jambo hilo kabla ya kunajisika ili ajijenge katika usafi huo na hatimaye atumie usafi wake huo kurekebisha na kuondoa uchafu ndani na kwenye kingo za uongozi nchini TZ.
Wana JF,
Leo naishia hapa, maoni yenu yana thamani kubwa sana, karibuni kwa maoni zaidi.