Naibu waziri wa Afya: Tuhamasishe matumizi ya P2

Mjanja M1

JF-Expert Member
Oct 7, 2018
3,660
12,305
Akijibu swali la Mbunge Thea Ntara ambae aliuliza,

"Hili suala sasa hivi linatisha, mabinti wanatumia hizo P2 kama unavyotumia panadol yaani hakuna utaratibu, tutafika wakati mabinti hawa hawataweza kupata watoto, je serikali ina mpango gani wa kutoa elimu kwa hao mabinti ili wajue matumizi ya P2 pamoja na hizo 'Energy drink'," - Mbunge Dkt Thea Ntara

Naibu Waziri wa Afya Dkt Godwin Molle amejibu swali hilo kwa kusema,

"Ni kweli matumizi ovyo ya P2 yanaleta madhara mengi, inasababisha akina mama kupata hedhi ambayo haina mpangilio na wakati mwingine kupata matatizo ya mifupa, sisi wote kwa pamoja tushirikiane kuhamasisha matumizi mazuri ya P2 yanayozingatia ushauri wa kitaalamu," - Naibu Waziri wa Afya

Mollel amesema P2 ni njia ya dharura ya vidonge vya uzazi wa mpango ambayo hutumika kuzuia mimba kwa Mwanamke aliyefanya tendo la kujamiiana bila kinga kwa mfano aliyebakwa au ametumia condom ikapasuka na anadhani anaweza kupata mimba asiyoitarajia wakati Sayana Press ni njia ya kuzuia kupata ujauzito kwa muda mrefu, hivyo matumizi ya kuzuia mimba kwa Sayana Press na P2 ni tofauti.

Nini maoni yako?

#Bungeni
Written by Mjanja M1 ✍️
 
"Ni kweli matumizi ovyo ya P2 yanaleta madhara mengi, inasababisha akina mama kupata hedhi ambayo haina mpangilio na wakati mwingine kupata matatizo ya mifupa, sisi wote kwa pamoja tushirikiane kuhamasisha matumizi mazuri ya P2 yanayozingatia ushauri wa kitaalamu," - Naibu Waziri wa Afya
Hao wataalamu wamejificha wapi maana mimba zisizotarajiwa ni nyingi, vyombo vya habari havishirikiani na hao wataalam kuhamasisha jamii
 
Mimi nafikiri ni muda muafaka serikali ifanye utowaji mimba kuwa ni jambo halali, sheria iruhusu tu kutoa mimba liwe jambo la Kawaida kama vile walivyoruhusu wanafunzi wa kike kupata mimba kuzaa kisha kurudi kuendelea na masomo
 
Kuna watu bado mnakunywa tu ma p2!?
Madhara huwa ni makubwa mno kwa mabinti, madhara makubwa kwa watumiaji wa mara kwa mara wa dawa hizo husababisha kizazi kulegea na mwisho kusababisha mimba kutoka pindi akinasa ujauzito (Miscarrage)

Hivyo, ni muhimu kupinga matumizi holela ya dawa hizo maana wahanga wakubwa wa dawa hizo ni mabinti waliopo shuleni na vyuoni.
 
Na matangazo yote haya bado wanawaagiza? Mbadala ni safe days na ujifunze kuwithdraw 😋
Withdraw iko more safe lakni inahitaji utalaamu wa hali juu kuuchomoa uume na utamu wote ule...

Njia nzuri tumia mpira maana itakulinda na magonjwa mengine pia nje na mimba zisizotarajiwa.
 
Back
Top Bottom