Fazul
Member
- Apr 2, 2012
- 82
- 9
Nimekuwa na mpenzi wangu wa mwaka mmoja,siku za hivi karibuni alianza kupuuza simu zangu na nilipochimbua zaidi na kuweza kumuhoji aliniambia ananipenda ila Dini ndio tatizo.mimi ni muislamu naye ni mkristo.na mimi siwezi kubadili dini,na kumuacha ni vigumu sana kwani nampenda zaidi ya sana.wakubwa nisaidieni maana sijui la kufanya.