Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,987
Mtuhumiwa alikamatwa Januari 25, 2024 eneo la Retco Jijini katika msako wa pamoja uliofanywa na Jeshi la Polisi na Maafisa wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii na kufanikiwa kumtia mbaroni kinara wa kuandaa nyaraka na mihuri bandia na kuwapa wanachama wa NSSF ili wapate mafao kinyume na sheria inayosimamia ulipwaji wa mafao.
Siku za hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la vishoka/matapeli ambao wamekuwa wakiandaa nyaraka (barua za kuachishwa kazi) za kughushi ambazo hutengeneza na kuwapa wanachama wa mfuko kwenda kufungua madai kinyume na taratibu ambazo ziko wazi kuwa ili mwanachama apate mafao ni lazima awe ameachishwa kazi na anakidhi vigezo vilivyopo kwa mujibi wa sheria.