Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,634
- 697,845
Kwa miaka mingi tulikuwa tunasikia midundo ya ngoma kuashiria kuanza kwa taarifa ya habari kwenye redio ya Taifa/serikali RTD na baadae TBC! ilikuwa ni midundo maarufu sana na yeyote aliyeisikia hata kwa mbali alijua wazi huu ni wakati wa taarifa ya habari....kwa majonzi makubwa midundo hii haipo tena huko TBC
Midundo hii ni ufundi wa Mzee Morris Nyunyusa mlemavu wa macho aliyekuwa na kipaji cha ajabu cha kupiga ngoma 17 kwa wakati mmoja, na midundo hii ilihusisha ngoma zote hizi
Umahiri wake huu ulimfanya ajulikane ndani na nje ya nchi huku akipata mialiko mingi tu...! Mzee huyu alikuwa ni tunu ya Taifa kwenye sanaa. Ni miaka mingi imepita hakumbukwi popote hata pengine kwenye vyuo vyetu vya sanaa
INAUMA SANA lakini historia itamkumbuka celebrity huyu wa kipindi hicho Mzee Morris Nyunyusa na pengine kuna siku kazi zake zitatakumbukwa na kutengenezewa hakimiliki ili wale aliowaacha wafaidike nako