‘Mwombeeni JK aepuke mapepo yanayomfuata Ikulu’ - Siamini kama kauli hii anaitoa waziri nchini!

Kiukweli kanisa la Gwajima lipo pale kinyume cha sheria' lile eneo matumizi yake siyo kwa kanisa.Nadhani waziri angeanza na hilo kwanza.!
 
sishangai kwani lukuvi alitetea sana KIKOMBE CHA BABU WA LOLIONDO.
Ni waziri anayeabudu ulozi ulozi sana.

Mkuu huwa tunatofautiana sana kwenye maswala mengi ila kwa hili hata mimi binafsi siamini kama kuna waziri anaweza amini ujinga wa akina Mwingira na watu kama hao
 
Kristo ni kwa Wakristo -bila shaka hatujamuelewa wazir labda ametoa wito kwa Mheshimiwa kubadili dini kwani maombezi ya kutoa mapepo kwa JINA LA YESU hufanya kazi kwa mtu mwenye imani TU
 
kumbe ndo maana jamaa kila siku anapiga misere anaogopa mapepo ikulu, dah hii kali.
 
hapo jamaa amemsitili mkulu nadhani hayo mapepo hayamfuati ikulu ila ameingia nayo mwenyewe, ni ya kwake!!! Kumbuka huyu ni waziri anajua mengi ambayo raia wa kawaida hatujui. Sijui itakuwaje siku upangaji wake utakapoisha, namshauri mrithi wake aende moja kwa moja chamwino na hapo magogoni pawe ni sehemu ya makumbusho ya taifa, alternately watu nchi nzima wafunge na kuomba kwa sana kuyafukuza
 
lukuvi ni kiongozi kihiyo, nawaonea huruma hao wanaomwamini maana hana uwezo wowote katika jambo lolote isipokuwa fitina, ana vitina sana, lakini siku jk akakapomjua kuwa ni mfitini nadhani atamumwaga maana hana tija kwa taifa kama tanzania hebu angalieni ana faida gani,amefanya nini. naturn off
 
Lukuvi ni mmoja mawaziri waliokunywa kikombe, Labda ugonjwa uliompeleke kunywa kikombe umemrudia hivyo kachanganyikiwa
 
Ukiona hivyou ujue kwisha kaaaaz, nawasihi viongozi wa
CCM woote waanze mchakato wa kupita majimboni kuanzia sasa na kuwaaga watanzania tena kwa kilio cha kwikwi maana ndio kwisha kaaaaz. 2015 hakika hawatarudi tena, tutawafuta rasmi. Angeanza mkuu mwenyewe ingekuwa dili mno. Au vipi wadau?
 
Saa ya wokovu ni sasa!!!
Mola ndiye mlinzi wa dhati kwa kila binadamu aaminiye. Huhitaji kuombewa, unahitaji kuomba na kuamini kwenye maombi.
 
Tetesi za mabadiliko baraza la mawaziri zimeanza kuwatesa baadhi ya mawaziri; eti kuna mapepo/majini yanamtembelea rais ikulu, unapigwa chini tu kama kazi zako ni umbea umbea tu na ahadi za abunwasi eti hizi karibuni uchumi utakuwa mzuri kwa mkakati upi Lukuvi?.
 
mzee yahaya ndiye aliyaleta hayo majini na mapepo hapo ikulu

kazi kwao sasa -- babu mwenyewe alishajifia siku nyingi!
 
Back
Top Bottom