Mwitikio wa Serikali na Wengine juu ya Mengi kutaja mafisadi!

Jamani, nahisi sifa moja kubwa ya kuwa mwanasiasa Tanzania ni uwezo uliopitiliza wa kuwa mnafiki. Sishangai serikali ikimgeuka Mengi. Ila katiba si inaruhusu mtu kutoa maoni yake na kama inaonekana kuna waliokosewa wampeleke mahakamani. Serikali kuwatetea hawa wafanyabiashara ambao wengi tunajua wanatudhulumu, ndio watakuwa wamechemsha

Serikali yetu inashangaza; Waziri Simba na Mkuchika wameiabisha serikali sana katika sakata hili kwa wanaonekana kuwasemea na kuwatetea Watuhumiwa.

Kinachoshangaza ni jinsi wanavyomchulia Mengi, labda sikufuatilia vizuri lakini ni vema Mawaziri hao wajiulize Mengi alitoa tuhuma hizo kwa kuvialika vyombo vyake pekee au alialika vyombo vyote vya habari (vikiwamo vya Rostam)? Kama Mengi alizungumza na vyombo vyote vya habari na vyombo vyote viliripoti habari hii, iweje leo Mawaziri wetu waseme ati Mengi anatumia vyombo vyake vya habari vibaya? Hao T/Daima, Mtanzania, Majira nk walioripoti habari hiyo nao watachukuliwa hatua gani? Nijuavyo mimi Mengi aliongea na Waandishi na Vyombo malimbali vya Habari na si vyombo vya IPP!

Waziri wa Utawala Bora Sofia Simba ni vema angesea kuwa Serikali itafuatailia na kuchunguza tuhuma dhidi ya "raia wema" (Watuhimiwa wa Ufisadi) kuliko kumshukia Mengi moja kwa moja, hii inaonyesha kuwa ama wameshegemea upande mmoja au wana chuki binafsi na Mengi.

Mawaziri wetu wanachemsha! They don't qualify kuwa Mawaziri, WAJIUZULU!
 
Kitu gani kizuri hapo?. Kwani wewe HUKUFIKIRI KUWA HAO WATU WANAWEZA KUMSHITAKI MENGI??

duh!

Wabongo zaidi ya uwajuavyo!

FP,
Sina hakika kama umejaribu kuelewa nilichomaanisha kwenye post yangu. Na pia sikuona sababu kwa nini usiniulieze (kama hukunielewa) badala ya kuamua kutoa conclusion yenye kuonesha dharau kwa maoni yangu ambayo hayakuhusu wewe na si lazima uyakubali.

Kwa kuwa tumekuwa tukisema kuwa tunahitaji siku moja hili suala lifike mahakamani, na Mengi mwenyewe alisema hivyo kwamba kama wanaona wameonewa waende mahakamani, huoni kuwa kwa maelezo hayo ya Waziri Simba jamaa wakienda mahakamni tutaipata ile fursa tuliyokuwa tunaitafuta siku nyingi? Kama huoni hiyo basi eleza jinsi unavyoona wewe na siyo kujaribu kushusha hadhi ya wenzio kwa kuwapandia mgongoni!
 
Mshikaji fikiria nje ya BOX. Aliyeibiwa nguo ni wananchi wa Tanzania. hao wananchi wanakuwa represented na POLISI (au kwa upana SERIKALI).

Sio kazi ya mwananchi kumfungulia mwananchi mwingine kosa la JINAI. Ni Polisi au ofisi ya DPP ndo ina mamlaka hayo.

Mengi hana mamlaka ya kuwapeleka mahakamani hao mafisadi kwa CRIMINAL CASE.

Jamani muwe mnauliza kwanza!

Umejibu hili swali ambalo nilikuwa ninataka Tom atafakari.

Hata hivyo ni vema ungeangalia 'key word' kwenye swali langu ambalo ni 'malalamiko' as a result umetoka nje ya swali.

Ninachoweza kukusaidia ni kwamba soma tena swali.
 
FP,
Sina hakika kama umejaribu kuelewa nilichomaanisha kwenye post yangu. Na pia sikuona sababu kwa nini usiniulieze (kama hukunielewa) badala ya kuamua kutoa conclusion yenye kuonesha dharau kwa maoni yangu ambayo hayakuhusu wewe na si lazima uyakubali.

Kwa kuwa tumekuwa tukisema kuwa tunahitaji siku moja hili suala lifike mahakamani, na Mengi mwenyewe alisema hivyo kwamba kama wanaona wameonewa waende mahakamani, huoni kuwa kwa maelezo hayo ya Waziri Simba jamaa wakienda mahakamni tutaipata ile fursa tuliyokuwa tunaitafuta siku nyingi? Kama huoni hiyo basi eleza jinsi unavyoona wewe na siyo kujaribu kushusha hadhi ya wenzio kwa kuwapandia mgongoni!

Hii approac ya hawa watuhumia kwenda mahakamani sijui inatoka wapi, kama kweli ni wezi wataenda mahakamani??

Naomba mtu anisaidie hivi mwananchi wa kawaida anawezi kumshtaki fisadi kama ana vithibitisho??
 
Jamani, kilio cha uporaji unaofanywa na mapapa ya ufisadi ni cha watanzania wote wenye mapenzi mema na nchi yetu. Mtu yeyote anaeonekana anawatetea waporaji hao mimi namwona kama mmoja kati ya maadui wakubwa wa nchi yetu. Hivyo basi, waziri Sophia, Mkuchika na wengine wenye tabia hizo ni vibaraka wa mafisadi na adui wakubwa wa watanzaia.
 
Hii approac ya hawa watuhumia kwenda mahakamani sijui inatoka wapi, kama kweli ni wezi wataenda mahakamani??

Naomba mtu anisaidie hivi mwananchi wa kawaida anawezi kumshtaki fisadi kama ana vithibitisho??

You very right. Hata kama wakienda mahakamani shauri litakuwa ni kukashifiwa na wala si kesi ya ufisadi. Labda tuseme Mengi atapeleka vielelezo kwamba nilivyoongea ni sawa na vielelezo ninavyo bado atawajibika kuvifikisha mahali husika na itakuwa ni shauri jingine. Kazi ambayo mimi ninamtaka Mengi aifanye sasa, anangoja nini?
 
"Simba alisema Mengi hana mamlaka hayo ya kutaja watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi."


I need to be educated. Hivi zile kura za siri kwa ajili ya kuwataja watu tunaowashuku katika jamii kua ni wauaji wa maalbino, siyo kwamba tunawashutumu? I mean, if we are allowed to 'make' allegations in secret, why souldn't we be allowed to do that in public if I am not afraid??
 
Hili suala ni gumu kwani kila mtu anamrushia mwenzie mpira. Nani amfunge paka kengere?
serikali ndiyo hiyo inaruka viuzi, Mengi anaishia kutaja eti kama wanabisha wamshitaki! na hao mafisadi hawawezi kumshtaki!!!! then?????? what next
 
Tatizo Mengi bado anaonekana kama ana ajenda ya kisiasa, sidhani kama Serikali imejiridhisha na utetezi wake alioutoa siku za nyuma kuwa hana nia ya kugombea urais. Hadi hapo watawala watakapo amini kuwa Mengi ni Raia mwema, hata afanye jambo jema kiasi gani bado litapokelewa na wakubwa kuwa linalengo la kisiasa. I hope wananchi wengi wanamuelewa anachokipigania.
kwa hiyo tuamini kuwa ni jinai kwa mwananchi yeyote mwenye sifa kugombea uraisi??
uhuni kweli huu
 
"Simba alisema Mengi hana mamlaka hayo ya kutaja watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi."


I need to be educated. Hivi zile kura za siri kwa ajili ya kuwataja watu tunaowashuku katika jamii kua ni wauaji wa maalbino, siyo kwamba tunawashutumu? I mean, if we are allowed to 'make' allegations in secret, why souldn't we be allowed to do that in public if I am not afraid??

Nakumbuka waziri alisema kuwa hizo kura zitatumika pamoja na ushahidi mwingine katika mchakato wa kuwatambua wauaji.
 
kwa hiyo tuamini kuwa ni jinai kwa mwananchi yeyote mwenye sifa kugombea uraisi??
uhuni kweli huu

nadhani Si jinai kugombea cheo bali ni jinai kumnyang'anya mtu tonge mdomoni, tumeona ya TLP juzi, kwikwikwi na CCM ni hivyo. kazi ipo
 
Ninapongeza kauli za serikali kwani watanzania wote tuna haki sawa na hakuna wa kumuhukumu mwengine pasi na mamlaka halali yaani mahakama. Kama Mengi ana ushahidi wa madai yake na ana vielelezo kwanini hakuviwasilisha katika mamlaka husika ili anaowatuhumu wachukuliwe hatua zipasazo? Hivi leo hii kila mtu anayemtuhumu mwenzie atinge maelezo amchafue kwa nia ya aliyechafuliwa aende mahakamani? Hakuna mantiki hata kidogo, watu wote wafuate sheria na utaratibu uliopo na si kutumia nafasi maalum kupindisha mambo.

Endapo serikali ingekaa kimya maana yake ina kubaliana na uendeshaji wa nchi bila ya kuzingatia utawala bora.

Serikali haipo kwa ajili ya wanyonge tu bali hata akina Mengi na Rostam. Ni vema basi ni lazima ikemee yale yote mabaya ikiwa ni pamoja na kauli za uchochezi, kuchukua sheria mikononi, ufisadi nk.
Serikali yetu iko imara wakati wote na iendelee kufanya kazi kwa faida ya wananchi wote bila ya kuwaonea aibu watu wachache kama Mengi wanaotaka kutimiza matakwa yao binafsi kwa mgongo wa mafisadi nk.

Tuziachie mamlaka husika zifanye kazi ya kutoa hukumu na si vinginevyo.

Kusema mtu ni fisadi kwa vitu ambavyo viko wazi sioni kama nitatizo. Kwani Mengi si mjinga wakutoka kichwa kichwa kwenda kwenye vyombo vya habari. Anajua kwani si mliona wakati anashitakiwa na Manji! Je manji aliendelea na kesi? Si alikacha kesi ikatupwa? Wakati mzee wa watu anaudhulia mahakamani kila siku.

Mbona hizi sheria zitumike kwa mengi je wakati wana mtandao wanajipamba kwa kuwachafua wenzao Salim mwarabu si mtanzania, Sumaye mwizi, Kikwete safi na Lowassa wake je mbona hamkusema? Sasa hivi sheria zifuate mkondo siyo?

Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo maadili yalishaondolewa na hao hao ambao leo hii wamegeukwa walisahau nao kuwa wana uvundo. Alivyofanya ni sawa kama anatishwa asiseme? Kama akiona watu wanaiba na hakuna linalofanyika asiseme eti kwakuwa kuna sheria? Kwanini sheria ziliwekwa? Ili zifunjwa otherwise hakukuwa na haja ya kuwa nazo.
 
Nazani tunahitaji kuandaa maandamano ya kumuunga mkono alichokisema mengi, tulitarajia serikali wangemuunga mkono mengi na kumpa support au
wangetumia maneno ya mengi kama sababu ya kufuatilia ufisadi.
Vyombo vya habari vya mengi tunavihitaji kwa ajili ya vita hii na mafisadi,
kwa kweli isingekua vyombo vya habari vya mengi, mambo mengi sana tusingeyajua, tunaomba mungu amjalie katika biashara zae, ili aendelee kutuhabarisha,
.usife moyo mengi wewe songa mbele.
wananchi wa taifa hili wako nyuma yako.
 
Hii ni kwa Pundamilia,

Wizi ni kosa la jinai (criminal). Mwenye uwezo wa kumfikisha mwizi mahakamani na kumsomea mashtaka ni Jamhuri. Raia ukishuhudia wizi, kama anaibiwa mwenzako, au jamii au mwenyewe, huna uwezo wa kwenda kumshitaki mwizi mahakamani.

Kazi yako ni kutoa ushirikiano kwa Jamhuri (kupitia jeshi la polisi), kwa kuiambia au kutoa taarifa na kuwa tayari kutoa ushahidi mahakamni utakapoitwa kama shahidi.

Mengi ameiambia serikali, si kwa kwenda polisi. Kwa kuwa ananguvu ya vyombo vya habari ametumia nguvu hiyo kuiarifu Jamhuri kuwa kuna mwizi ameonekana ameiba na ushahidi anao.

Sasa sioni tatizo hapo ndugu pundamilia. Kuiambia polisi au kuiambia jamhuri mpaka uende mwenyewe kituo cha polisi na makaratasi? Hivi mtu huwezi kupiga simu polisi ukasema Mimi fulani niko mahali fulani nashuhudia au nimeshuhudia tukio la wizi??

Sijaona kosa la raia kusema kuwa mali ya umma imefujwa na yeye anao ushahidi!! Vyombo husika vichukue hatua na baada ya kufanya uchunguzi vije mbele na viseme ushahidi hautoshi kuwafikisha mahakamani. Halafu walituhumiwa ni juu yao kufungua kesi ya madai.

Pundamilia unaposema Mengi ilitakiwa afuate taratibu; naomba uwe wazi ni taratibu zipi hizo?
 
Sirikali makini haiachi kushughulikia ktk style iijuayo yenyewe aili muradi truth ina onekana, sidhani mama Sophy amekosea, maana kuikubali njia ya Mengi ni ku givein cheaply kwa sirikali kwa bwana Mengi na ndicho ambacho pengine alikitarajia, mimi naamini tayari sirikali iko kazini juu ya hao mapapa aliowataja Mengi, na wengine wako mahakamani tayari kabla Mengi kutoka na single yake.

Mama Simba yuko sahihi, acha dola ifanye kazi yake kama dola na kuweka miongozo kwa jamii ambamo ndugu Mengi anatokea, Mungu ibariki Tanzania, Hongera mama Simba kwa Job well done- tuachie home yetu ya Mengi vs Mapapa
 
Kusema mtu ni fisadi kwa vitu ambavyo viko wazi sioni kama nitatizo. Kwani Mengi si mjinga wakutoka kichwa kichwa kwenda kwenye vyombo vya habari. Anajua kwani si mliona wakati anashitakiwa na Manji! Je manji aliendelea na kesi? Si alikacha kesi ikatupwa? Wakati mzee wa watu anaudhulia mahakamani kila siku.

Mbona hizi sheria zitumike kwa mengi je wakati wana mtandao wanajipamba kwa kuwachafua wenzao Salim mwarabu si mtanzania, Sumaye mwizi, Kikwete safi na Lowassa wake je mbona hamkusema? Sasa hivi sheria zifuate mkondo siyo?

Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo maadili yalishaondolewa na hao hao ambao leo hii wamegeukwa walisahau nao kuwa wana uvundo. Alivyofanya ni sawa kama anatishwa asiseme? Kama akiona watu wanaiba na hakuna linalofanyika asiseme eti kwakuwa kuna sheria? Kwanini sheria ziliwekwa? Ili zifunjwa otherwise hakukuwa na haja ya kuwa nazo.

Ndugu yangu Mugerezi,

Baada ya kusoma posting yako nimeona kweli iko haja kupitia katika thread hii ni kuelimishe kwani ni moja ya sehemu ya faida za hapa JF.
Kimsingi sheria moja inapovunjwa haihalalishi kuvunjwa kwa nyingine. Unapuvunja sheria kwa kigezo kuwa tayari ilivunjwa sheria nyingine hapo awali hutasamehewa hata kidogo. Kwa mfano, labda umemkamata mwizi aliyekuibia, pamoja na kwamba yule mwizi amefanya kosa lakini ukichukua hatua yeyote ile ya kumwadhibu kwa namna yeyote, tayari na wewe unakuwa ni sehemu ya wavunja sheria na mamlaka husika zitakuadhibu kwa kosa hilo.

Ninachotaka kukueleza hapa ni kuwa si sahihi kufanya mambo bila ya kufuata taratubu na sheria zilizopo kama kweli nia yetu ni kuikomboa jamii ya kitanzania. Endapo tutafumbia macho na kuamua kufanya mambo bila ya utaratibu basi tujue tunazidi kuiangamiza demokrasia na utawala bora. Demokrasia na utawala bora vinahitaji kila mtanzania abadilishe mind set yake na tuwe wakweli na waungwana katika matendo yetu viinginevyo tutazidi kupoteza muda kwa kupiga kelele zisizokwisha.

Endapo kama nina ushahidi wa kutosha dhidi ya uovu unaofanywa na mtu au kundi fulani basi ni wajibu wangu kuufikisha katika sehemu husika ili sheria iweze kuchukua nafasi yake.
 
Ni vizuri Mengi ameanza kurekebisha makosa yake. Laiti kama sio yeye kutumia vibaya vyombo vyake vya habari mwaka 1995 Tanzania ingekuwa na oposition nzuri sana hasa bungeni lakini akakubali kushirikiana na CCM kuwaonyesha watanzania wote picha za mauaji ya Rwanda. Intention ya hizo picha ilikuwa kuwafunza watanzania kuogopa vyama vya upinzani visije kuleata hali kama hiyo. kwa hilo alikwa ni kibaraka mkubwa.

Aliponyimwa kuuziwa hoteli ya Kilimanjaro ndio akaanzisha mtindo wa kushitaki kwa umma. Sijui alitegemea umma alioshiriki kuamputate uchukue hatua gani. Hivi sasa kazi anayofanya single hande ilitakiwa kufanywa na wabunge kutoka vyama mbali mbali waliochaguliwa na watanzania. kwa bahati mbaya sana mengi anahangaiki symptoms badala ya kiini cha maradhi waliyo nayo watanzania.

Ili kuweza kusafisha makosa aliyowatendea watanania Mengi anatakiwa kuhakikisha vyombo vyake vya habari vinatoa elimu ya uraia ili kila Mtanzania aweze kutambua namna ya kutumia ballot box kurekebisha matatizo yaliyopo. Therefore badala ya kuinvest milions kwenye vikoba kujaribu kuwatetea baadhi ya wabunge resources hizo azielekeze kwenye elimu ya uraia, hapo atakuwa ametoa mchango mkubwa kurekebisha matatizo yaliyopo.

Hata hivyo nampongeza kwa kutambua makosa yake mapema kwa kuwa bado ana nafasi ya kuyarekebisha for the benefit of the nation. Sera alizoanzisha za "kutajana" kwa majina ni safi sana kwa kuwa zitasaidia kuvunja Conspiracy of silence tuliyo nayo watanzania.

Ikiwa mwaka 1995 muasisi wa TANu na CCM hayati Mwalimu Nyerer alitamka wazi wazo kumuunga mkono mgombea wa NCCR Balzi Paul Ndobo kugombea ubunge jimbo la Musoma Vijijini kwa kuwa mgombe aliyesimamishwa na CCM alikua na tuhuma za kufilisi ushirika kuna tatizo gani watanzania wakachagua wagombea kutoka vyama vya upinzania kwa wingi zaidi kuingia bungeni ili kuimarisha accountability of the government. Thats your role Mr Mengi badala ya kujipendekeza kwa JK
 
Sirikali makini haiachi kushughulikia ktk style iijuayo yenyewe aili muradi truth ina onekana, sidhani mama Sophy amekosea, maana kuikubali njia ya Mengi ni ku givein cheaply kwa sirikali kwa bwana Mengi na ndicho ambacho pengine alikitarajia, mimi naamini tayari sirikali iko kazini juu ya hao mapapa aliowataja Mengi, na wengine wako mahakamani tayari kabla Mengi kutoka na single yake.

Mama Simba yuko sahihi, acha dola ifanye kazi yake kama dola na kuweka miongozo kwa jamii ambamo ndugu Mengi anatokea, Mungu ibariki Tanzania, Hongera mama Simba kwa Job well done- tuachie home yetu ya Mengi vs Mapapa

Mimi shida yangu, ni utaratibu ambao mtu mwenye ushahidi wa jinai anatakiwa autumie kuifahamisha serikali (utaratibu wa kisheria). Au tunakereka kwa mengi kutumia vyombo vya habari? Lakini si ndiyo kazi ya vyombo vya habari?

Jinai inatakiwa ishughulikiwe na serikali. Sasa mtu ukishuhudia jinai huruhusiwi kutumia vyombo vya habari kuifahamisha serikali? Kosa hasa hapa ni nini?
 
Hebu tujikumbushe kidogo hii makala ya zamani kidogo ili tumfahamu huyu Manyerere na hapo itakuwa rahisi kumjadili:-


Huyu Manyerere anasema mengi amekuwa mahakama!!! Je naye amekuwa amekuwa Dr. wa vichaa kusema kuwa huyu mzee kachanganyikiwa?
 
Back
Top Bottom