Mi nahisi ujio wa Mwigamba jimbo la Ubungo ni kama kumpeleka Mbele Mnyika.......
Hii ni kwa sababu mwigamba ni mtu dhaifu sana na kura za Mnyika zimekaa. Hivyo ujio wake utapunguza japo kiduchu kura za CCM na sio za Mnyika.
==============================
Hii ni kwa sababu mwigamba ni mtu dhaifu sana na kura za Mnyika zimekaa. Hivyo ujio wake utapunguza japo kiduchu kura za CCM na sio za Mnyika.
==============================
KILE kinachoonekana ni kama Chama Kipya cha Siasa nchini cha ACT-Wazalendo wamejipanga kumwondosha Mbunge wa Jimbo la Ubungo CHADEMA John Mnyika kwenye Ramani ya kisiasa nchini baada ya Uchaguzi Mkuu hapo baadae mwaka huu zimebainika, Anaripoti KAROLI VINSENT.
Baada ya hivi sasa Katibu mkuu Taifa wa ACT-Wazalendo Samsoni Mwigamba kutangaza rasmi kuwania Ubunge kwenye Jimbo la Ubungo ambalo linashikiliwa kwa sasa na Naibu huyo Katibu Mkuu Chadema bara.
Mwigamba ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa Mtandao huu ambapo Mwigamba hakusita kuzungumzia safari yake ya kisiasa katika Uchaguzi mkuu ujao kwa kusema atagombea Rasmi Ubunge kwenye Jimbo la Ubungo.
Kwa Mujibu wa Mwigamba anasema Sababu ya kwenda kwenye Jimbo hilo inatokana na Mbunge wa sasa aliyopo kushindwa kuwatendea haki wananchi wajimbo hilo ikiwemo kuwatimizia mahitaji muhimu.
"Nakuhakishia Mwandishi nawania Ubunge kwenye Jimbo la Ubunge maana Mnyika ameshindwa kutimizia Mahitaji muhimu wananchi wa Ubungo,mimi mwenyewe ni Mkazi wa Ubungo tunapata tabu, leo Mbunge wetu yupo kwenye Kazi ya kukijenga chama chake cha Chadema kuliko wananchi tuliomchagua sasa mimi najitosa rasmi nakuhakishia namtoa mnyika" amesema Mwigamba.
Mwigamba ambaye kabla ya kuhamia ACT-Wazalendo alikuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Arusha na alifukuzwa kwenye Chama hicho kikubwa cha Upinzania nchini kwa madai ya kuandaa Mipango ya kumpindua Mwenyekiti wa Chadema Taifa Freeman Mbowe kwa kushirikiana na wenzake ambaye ni Zitto Kabwe pamoja na Profesa Kitila Mkumbo ambapo Mwigamba alizitaja ahadi ambazo Mbunge Mnyika alizihaidi mwaka 2010 kwa mujibu wa Mwigama anadai ameshindwa kuzitimiza, ni mahitajia ya Maji safi na salama ambayo anadai limekuwa Tatizo kubwa kwa wananchi wa Jimbo hilo pamoja na tatizo la usafiri ambalo anasema ataweza kuliondoa kwa mda mfupi tu pindi atakapopata Ubunge huo.
Chanzo; FullHabari Blog