pole sana mkuu. lingekua li nivea lisingepata pole yangu sana sana ningeliombea mabaya. Mungu wangu akuponye na kukulinda pia.
Pole Zinduna ....tunakuombea upone upesi uje uendelee na show!
Oh! Pole sana Zinduna.... mi nakumisije sasa? Pona haraka bana!! Bishanga anaumisi msuto wako.Habari zenu wana JF wapendwa.Ni wiki ya pili sasa niko hoi kitandani baada ya kufanyiwa operesheni .....No, sorry nilikuwa namaanisha upasuaji wa kidole tumbo. Unajua kuna maradhi mengine ukiyatamka kwa kiingereza yanavutia tofauti na kuyatamka kwa kiswahili. kwa mfano ni vyema kusema nina Appendex badala ya kusema nina kidole tumbo, au ni vizuri ukisema una diarrhea badala ya tumbo la kuhara, au kusema nina typhoid badala ya kusema nina homa ya matumbo.
Vile vile ni vyema kusema unaumwa tonsils badaya ya kusema unaumwa mafindofindo, au kusema unaumwa AIDS badala ya kusema una UKIMWI.Si mmeona majina ya maradhi yakitamkwa kwa kiingereza yanavyovutia.
Ndio sababu na mie nikasema nimefanyiwa operesheni ya appendex badala ya kusema nimefanyiwa upasuaji wa kidole tumbo.
Hapo full kunyonya kama sina akili nzuri