Habari zenu wanajamii.
Jamani maisha ni safari ndefu na inahitaji uvumilivu na ujasiri. Nimetumia ujasiri wangu kwa kujitokeza katika jukwaa hili ili kuweza kupata mwenza ambae atakuwa mume kama Muumba akibariki. Kwa aliye na nia ya dhati haswa naomba tuwasiliane kwa private message.
Sifa zangu
Umri: Miaka 30
Umbo:Ni wa kawaida sana, na kwa wale wanopenda makalio makubwa, mimi sina jamani, ni bora kuwa mkweli!
Urefu: Centimeter158
Rangi: Maji ya maharage
Elimu: Degree mbili
Kazi: Muajiriwa wa serikali
Dini:Islam
Sifa za Mtarajiwa
Umbo: asiwe na kitambi kwa kweli
Urefu: itakuwa vyema kama akinizidi maana isije leta zahma
Rangi: yeyote
Elimu: Degree
Kazi: Ni muhim maana maisha ni magumu sana
Dini: Islam, ila uwe hujaoa!
Najua kunawatakoleta mzaha, ni kawaida sana kwenye jamii. Nipo tayari kwa maswali mtakayoyauliza. Karibuni!
Awe hajaoa kabisa, au awe hajaoa kabla ya kukuoa wewe?...Dini: Islam, ila uwe hujaoa!
Hapana Vin Diesel, sipo tayari kuwa mke wa pili!
Mi ninazo zooote kasoro moja tu.......So i guess am ineligible
Daah! sifa zoote ninazo isipokuwa hapo kwenye kitambi! hebu nipe muda ntarekebisha hii ila ntabakiza cha kuvalia mayenu! Kama pouwa twende kazi.
Vipi kuhusu afya yako iko vizuri?
ishu ya dini bana inafanya nikukose. Can't u think otherwise kuhusu hiyo ishu ya dini?
Hizo degree mbili ni za nini, I mean specialization i.e sociology, education, economics...
Nasreem, mimi nimefurahishwa na namna unavyojibu maswali, nimevutiwa na nina sifa zote kasoro nimeoa. Ila ningeomba tuwe marafiki tu.. kwani nimevutiwa kuwa na rafiki kama wewe.Kama huna tatizo na hili ni PM.