Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,814
- 11,991
Mwenyekiti wa UWT Taifa, Mary Chatanda amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Veronica Vicent kujitafakari juu ya utendakazi wake ndani ya Wilaya hiyo.
Chatanda amesema kuwa amesikitishwa na namna ya utendaji kazi wa Mkurugenzi huyo ambavyo hauko vizuri kwenye Halmashauri hiyo ikiwemo mahusiano yake na wenzake.
Chatanda amesema hayo leo Septemba 21, 2023 Wilayani Busega alipokuwa akiagana na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega sambamba na watumishi kutoka ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega mara baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi wilaya humo.
"Mwambieni Mkurugenzi asimame vizuri, narudia tena Mwambieni Mkurugenzi asimame vizuri, hayuko vizuri... ashirikiane na wenzake, ashirikiane na Chama ili mambo yaende vizuri.
"Nimesikitishwa sana na tabia ya Mkurugenzi wa hapa Busega amekuwa sio mtu wa kushirikiana na wenzake, hili suala halikubaliki kwani viongozi wa Chama ndio wenye Ilani ya CCM, hivyo basi anapashwa kuwashirikisha kwenye kila suala linalohusu maendeleo kwenye Wilaya hii," amesema.
Chatanda amesema hayo leo Septemba 21, 2023 Wilayani Busega alipokuwa akiagana na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega sambamba na watumishi kutoka ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega mara baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi wilaya humo.
"Mwambieni Mkurugenzi asimame vizuri, narudia tena Mwambieni Mkurugenzi asimame vizuri, hayuko vizuri... ashirikiane na wenzake, ashirikiane na Chama ili mambo yaende vizuri.
"Nimesikitishwa sana na tabia ya Mkurugenzi wa hapa Busega amekuwa sio mtu wa kushirikiana na wenzake, hili suala halikubaliki kwani viongozi wa Chama ndio wenye Ilani ya CCM, hivyo basi anapashwa kuwashirikisha kwenye kila suala linalohusu maendeleo kwenye Wilaya hii," amesema.