Mwenyekiti Kamati ya Richmond akatiwa maji

This is embarassing and humiliating. Ule ubabe wote wa kuwa Kinara unakuja kunaswa na mtego mwepesi kama huu?

Jamani nyie kina Seleli, Kilango-Malecela, Kimaro na wengine wote mlioanza kukiuka "miiko" ya Chama anzeni kujisafisha na kutoa tongotongo zote la sivyo mtaumbuka kama Mwakyembe!

Katibu Mkuu wa chama chetu huwa anatuasa kila siku kuwa tukitaka kupambana na ufisadi sawasawa ni lazima sisi wenyewe tujitahidi kuwa wanyoofu! Sasa hili Mwakyembe kajiingiza mwenyewe. Hii ya kamati tayari ilishafanya watu wakasahau yale madudu yake ya kutetea mauaji ya Zanzibar, sasa naona amejirudisha mwenyewe na watu itabidi tukumbuke mengi yake!
 
Haya tuliokurupuka! Mwenyewe amesema! Au ndiyo ana'spin'?


Hatukukurupuka bwana, tulitumia vyanzo halali vya habari kama ambavyo wewe umetumia hii. Tutasubiri counterpunch ya DAWASCO. Kama ni ukurupukaji itakuwa ni DAWASCO au Mwakyembe, so far JF hakuna aliyekurupuka!
 
Haya tuliokurupuka! Mwenyewe amesema! Au ndiyo ana'spin'?

Mkuu,

Hapo patamu kweli kweli. Nijuavyo mimi mheshimiwa Mwakyembe anaishi hilo
eneo lililotajwa. Sasa hapo kumekuja kitu kingine, kwamba huenda huo uwanja sio wa kwake.

Ni mahakama tu inaweza kuamua maana ni ngumu kwa wengine kujua kama hapo ni kwake au sio kwake hata kama anaishi hapo.

Labda angefanunua zaidi kwa kusema yeye nyumba yake ni namba fulani na haidaiwi na hiyo iliyotajwa ni namba fulani na ni ya mtu mwingine.

Wacha tuendelee kusubiri zaidi.
 
I'll tell you what will happen:

DAWASCO watamuomba radhi kama siyo leo hii basi mapema wiki ijayo. Kwa sababu in the original story, mama Mwakyembe alienda kutaka huduma ya maji, sasa kama tayari alikuwa na huduma ya maji kwanini alienda kuomba huduma ya maji.

Sasa unaenda una shida ya maji halafu unaambiwa umeshajiunganishia maji na unatakiwa ulipe shilingi laki sita wakati hauna maji utalipa?

DAWASCO wamejiingiza katika mtego wa Agenda 21.
 
Katibu Mkuu wa chama chetu huwa anatuasa kila siku kuwa tukitaka kupambana na ufisadi sawasawa ni lazima sisi wenyewe tujitahidi kuwa wanyoofu! Sasa hili Mwakyembe kajiingiza mwenyewe. Hii ya kamati tayari ilishafanya watu wakasahau yale madudu yake ya kutetea mauaji ya Zanzibar, sasa naona amejirudisha mwenyewe na watu itabidi tukumbuke mengi yake!


mzee tukubali sote tumekurupuka kwani tuliassume kuwa Mwakyembe ndiyo mwenye nyumba kwa sababu tulitegemea habari hizo za gazeti. Tulishindwa kuuliza swali moja muhimu (kwa sababu it didn't occur to us I suppose) kwamba what if there ia big misunderstanding? Je yawezekana kulikuwa na makosa. We all assumed the story to be correct na tumeenda na kumuona Mwakyembe naye fisadi au "ndio wale wale". Tumekuwa na haraka ya kuhukumu bila kumsikiliza. Hapa tulikurupuka. At least I can speak for myself. Waandishi walipoambiwa wamechemsha kwa habari zisizo sahihi, na sisi tukubali tulichemsha kwa hukumu zisizo na facts zote.
 
I'll tell you what will happen:

DAWASCO watamuomba radhi kama siyo leo hii basi mapema wiki ijayo. Kwa sababu in the original story, mama Mwakyembe alienda kutaka huduma ya maji, sasa kama tayari alikuwa na huduma ya maji kwanini alienda kuomba huduma ya maji.

Sasa unaenda una shida ya maji halafu unaambiwa umeshajiunganishia maji na unatakiwa ulipe shilingi laki sita wakati hauna maji utalipa?

DAWASCO wamejiingiza katika mtego wa Agenda 21.

Mwanakijiji,

Mimi nilivyoelewa hiyo habari ni kwamba huyo mama alienda kuhalalisha huduma ya maji toka DAWASCO labda baada ya kusikia heka heka za kata maji.

Haya ndio mambo ya Tanzania huwa hakuna incentives za watu kuja clean, huyu mama huenda walimwadhibu sawa tu na kama wao wenyewe wangegundua kajiunganishia maji.

Mimi naona kwa watu waliojisalimisha wenyewe, adhabu ingelikuwa ndogo na kusingelikuwa hata na haja ya kuwatangaza magazetini.
 
Mwanakijiji,

Mimi nilivyoelewa hiyo habari ni kwamba huyo mama alienda kuhalalisha huduma ya maji toka DAWASCO labda baada ya kusikia heka heka za kata maji.

Hata mimi nilielewa hivyo hivyo kwamba alitaka kwenda kuhalalisha huduma hiyo. Hata hivyo baada ya kusoma hayo maneno ya Mwakyembe, nimerudi na kusoma original story na inasema hivi na kuthibitisha kuwa tulikosea kufikiri tulivyofikiri kwa sababu of our own prejudices and biases.

Akizungumzia hatua ya Dkt. Mwakyembe ambaye ni mbunge wa Mbeya kukutwa amejiunganishia maji, Ofisa Uhusiano wa DAWASCO, Bi. Badra Masoud, alisema wiki moja iliyopita mkewe alikwenda katika ofisi za kampuni hiyo kwa lengo la kujaza fomu ya kuomba huduma ya maji NDIPO (Msisitizo wangu) alipoelezwa kuwa wamejiunganishia maji isivyo halali.

Bila kumtaja jina lake, Bi. Masoud alisema walipomkatalia kumpa fomu hizo wakimtaka alipe faini kwanza alikataa.

"Kwa kuwa alikataa ndio maana leo hii (jana) tumekuja kumkatia," alisema Bi. Masoud. Alitaja faini aliyotakiwa kulipa kuwa ni sh. 600,000.

Huoni tulikosea kufikiri alienda kuhalalisha huduma ya maji tulioamini wamejiunganishia kinyemela? Story is very clear.
 
Hata mimi nilielewa hivyo hivyo kwamba alitaka kwenda kuhalalisha huduma hiyo. Hata hivyo baada ya kusoma hayo maneno ya Mwakyembe, nimerudi na kusoma original story na inasema hivi na kuthibitisha kuwa tulikosea kufikiri tulivyofikiri kwa sababu of our own prejudices and biases.



Huoni tulikosea kufikiri alienda kuhalalisha huduma ya maji tulioamini wamejiunganishia kinyemela? Story is very clear.

Mwanakijiji,

Hata kama unaenda kuhalalisha, bado unaomba maji upya kama ndio unaanza. Sasa wakati vijana wanakuja kukufungia maji ndio mnamalizana nao. Ndivyo zamani watu walivyokuwa wanafanya.

Mimi niliwahi kwenda kuomba maji, nikalipia, wakaniambia hakuna vifaa mpaka hata miezi mitatu. Nikaambiwa nikitaka nikatafute mafundi wangu wanifungie au hata hao hao wa maji wanifungie.

Kwasababu ya haraka na kutokuwa na muda, nikatafuta mafundi wangu, vifaa vyangu na kufunga maji. Hii ina maana vile vifaa nilivyolipia, jamaa walikunywa. Hiyo ndio TZ yetu.

Kwenye hili suala la Dr. nafikiri ni wazi kwenye hicho kiwanja maji yaliunganishwa isivyo halali. Kitu ambacho sio wazi ni je kitendo hicho kilifanywa na Dr. Mwakyembe? Hapo mimi naona ndio kwenye utata maana Dr. anasema hicho sio kiwanja chake.

Mkewe Dr. akikataa kwamba hakuenda DAWASCO kuomba maji, wata prove vipi kwamba ni yeye alienda? Ndio maana kwa wenzetu kuna camera kila sehemu.
 
Mkuu,

Hapo patamu kweli kweli. Nijuavyo mimi mheshimiwa Mwakyembe anaishi hilo
eneo lililotajwa. Sasa hapo kumekuja kitu kingine, kwamba huenda huo uwanja sio wa kwake.

Ni mahakama tu inaweza kuamua maana ni ngumu kwa wengine kujua kama hapo ni kwake au sio kwake hata kama anaishi hapo.

Labda angefanunua zaidi kwa kusema yeye nyumba yake ni namba fulani na haidaiwi na hiyo iliyotajwa ni namba fulani na ni ya mtu mwingine.

Wacha tuendelee kusubiri zaidi.

Anachodai Mheshimiwa kuwa mahali penye deni pana banda tu na ni pa mteja wake ambaye ni marehemu! Sasa mwenzetu unatueleza kuwa Mheshimiwa anaishi sehemu hiyo. Tuseme anaishi kwenye hilo banda? Au ndiyo yale ya vijisenti, kasri kuita banda!!!! Mimi nahisi mheshimiwa ana nyumba anayoishi (pengine kapanga), kiwanja na hicho chenye matatizo. kwa sababu dawasco waliona wameishampata ( si unajua utanzaji wa kumbukumbu wa mashirika yetu) mama alipoenda kuomba kuunganishwa kwenye kiwanja chake wakaingia mkenge! Haya tuvute subira maana mkweli atajulikana tu.
 
Anachodai Mheshimiwa kuwa mahali penye deni pana banda tu na ni pa mteja wake ambaye ni marehemu! Sasa mwenzetu unatueleza kuwa Mheshimiwa anaishi sehemu hiyo. Tuseme anaishi kwenye hilo banda? Au ndiyo yale ya vijisenti, kasri kuita banda!!!! Mimi nahisi mheshimiwa ana nyumba anayoishi (pengine kapanga), kiwanja na hicho chenye matatizo. kwa sababu dawasco waliona wameishampata ( si unajua utanzaji wa kumbukumbu wa mashirika yetu) mama alipoenda kuomba kuunganishwa kwenye kiwanja chake wakaingia mkenge! Haya tuvute subira maana mkweli atajulikana tu.

Fundi Mchundo,

Wasiwasi wangu ni kwamba huenda tunaongelea nyumba (viwanja) mbili tofauti lakini pia inawezekana kuwa ni kiwanja hicho hicho.

Kama nilivyoandika juu, najua mheshimiwa anaishi hayo maeneo yaliyotajwa ila sijui kama hapo palipounganishwa maji ndio kwake.

Nafikiri Mwakyembe mwenyewe angeweza kufafanua zaidi kwa kuelezea kwamba nyumba yake iko sehemu tofauti.

Pia gazeti nashangaa kwanini walishindwa kuwauliza DAWASCO pia baada ya Mwakyembe kukanusha?

Hata juzi mimi sikuona uharaka wa kuchapisha hiyo habari bila kupata msimamo wa Dr. Mwakyembe. Hata kama asingelipatikana basi bado walikuwa na wajibu wa kueleza kwamba hawakufanikiwa kuongea na Mwakyembe.
 
Nakubali lakini ukweli kuwa reaction yetu ya mwanzo was so one sided and condemning which was unfair. Nadhani next time tujitahidi kuwa more balanced. Binafsi nimeshajifunza hilo. Let me remind you how we reacted:

Mwakyembe alijiunganishia maji kinyume cha utaratibu,huo ni wizi na ukosefu wa uadilifu,hakutumwa na RA kufanya hivyo,na siyo wakwanza kukamatwa anafanya hivyo na kutangazwa....msiwe double standard kama mtu amekosea na asemwe.

Na wewe:

Msimamo wangu juu ya hili ni kwamba kosa ni kosa tu, ukifanya kosa hakuna haja ya kutafuta mchawi.

Wale wote wanaoongoza mapambano na mafisadi lazima wafanye juhudi kubwa kuhakikisha na wao huko nje wanakuwa wasafi kadri iwezekanavyo kwa mazingira ya TZ. Ni sawa na sisi JF, tutakuwa credible kama yale tunayoyapinga, tutayapinga kwa kila mtu bila kujali chama na kuhaki,kisha sisi wenyewe sio vifisadi wadogo.

Na Kitila naye:

Hata kama nia ya ku-report hii taarifa ni ingine, lakini ni aibu sana na ujinga wa hali ya juu kwa mtunga sheria kuvunja sheria. Ni wapi mwisho wa kuvunja sheria ile nchi. Halafu nashangaa watu mnashupalia mambo mengine wakati kuna clear and utter violation of the law hapa.

Kipanga na yeye:

Mnataka kuleana sio??? hawa wanaojifanya waheshimiwa ndio wanaua nchi kwa kupenda miteremko huku wanavunja vishoka kwenye mashangingi tuliyolipia kodi zetu....Uchafu mtupu!!!

Na mimi mwenyewe:

Dr. Mwakyembe na wenzie watengeneze mambo yao kwani watakapobanwa (na tulionya hili tangu Februari) wasije kulalamika kuwa wanaundiwa "mizengwe" au kuna watu wanajaribu kuwatafuta ubaya.

Kitila akagongomelea zaidi:

Hata kama nia ya ku-report hii taarifa ni ingine, lakini ni aibu sana na ujinga wa hali ya juu kwa mtunga sheria kuvunja sheria. Ni wapi mwisho wa kuvunja sheria ile nchi. Halafu nashangaa watu mnashupalia mambo mengine wakati kuna clear and utter violation of the law hapa.

Na MaMkwe akasema hivi kwa kujiamini:

Yeye (Mwakyembe) kafanya kazi yake. Nampongeza kwa hilo. Tatizo zi kukatikwa maji. Huyu bwana ambaye Watanzania walianza kujenga imani juu yake kwa kuonekana ni muadilifu kumbe sivyo. Amejiunganishia maji kwa njia za panya na kisha kaminya kulipa bili. Hapa inaonyesha ni jinsi gani Wabongo tunatisha. Yaani kila mtu akipata upenyo kidogo tu anakwiba. Wengine wanaonekana wasafi tu kwa vile hawajapata nafasi ya kufisadi.

Wanaomtetea Mwenyekiti wa Richmond siwaelewi kabisa. Kama habari za kukakiwa maji na sababu zilizotolewa na DAWASCO ni za urongo basi na ajitetee mwenyewe.


JokaKuu hakuwa mbali naye:

..Dr.Mwakyembe yeye ni mwanasheria aliyebobea, mtetezi wa umma, anayepiga vita ufisadi, dhuluma, na uhujumu uchumi. haitegemewi kabisa mtu mwenye sifa asilipe bili zake kwa vyombo vya umma.

Hata Ogah naye akasema hivi:

Hakuna anayekataa hapa kuwa Dr.Mwakyembe kaenda kinyume na sheria ya kuunganishiwa maji kama ilivyodaiwa

Reverend naye hakuwa nyuma:

This is embarassing and humiliating. Ule ubabe wote wa kuwa Kinara unakuja kunaswa na mtego mwepesi kama huu?

sasa katika haya yote, ni wapi kuna fairness or any sense of balance? Je haioneshi kuwa sisi tunajiona ndio wenye haki zaidi na hatuna "room" for mistakes or a sense of "wait a minute, lets hear Mwakyembe before we make any judgement"? doesn't this show our own sense of twisted arrogance and self-importance? I know I was wrong.
 
Nakubali lakini ukweli kuwa reaction yetu ya mwanzo was so one sided and condemning which was unfair. Nadhani next time tujitahidi kuwa more balanced. Binafsi nimeshajifunza hilo. Let me remind you how we reacted:


sasa katika haya yote, ni wapi kuna fairness or any sense of balance? Je haioneshi kuwa sisi tunajiona ndio wenye haki zaidi na hatuna "room" for mistakes or a sense of "wait a minute, lets hear Mwakyembe before we make any judgement"? doesn't this show our own sense of twisted arrogance and self-importance? I know I was wrong.

Mwanakijiji,

JF sio gazeti au radio. Naamini muundo wetu wa sasa ni bora zaidi kuliko tukianza kujifanya waandishi wa habari wa kusomea.

Hii ya kwetu ni citizen journalism.

Kuna wakati tutakosea lakini pia kuna mara nyingi tutapatia. Ni muhimu pale tunapokosea kukubali tumekosea hata kama anayesemwa na fisadi Chenge.

Tukitaka tupate uhakika wa 100% kabla ya kuandika, JF itapoteza lengo lake
la kukusanya, kuchambua na kuiwakilisha habari kwa haraka iwezekanavyo.
 
Mwanakijiji,

JF sio gazeti au radio. Naamini muundo wetu wa sasa ni bora zaidi kuliko tukianza kujifanya waandishi wa habari wa kusomea.

Hii ya kwetu ni citizen journalism.

Kuna wakati tutakosea lakini pia kuna mara nyingi tutapatia. Ni muhimu pale tunapokosea kukubali tumekosea hata kama anayesemwa na fisadi Chenge.

Tukitaka tupate uhakika wa 100% kabla ya kuandika, JF itapoteza lengo lake
la kukusanya, kuchambua na kuiwakilisha habari kwa haraka iwezekanavyo.


tatizo haliko kwenye kuripoti habari, nadhani habari zinakuja sawasawa tu na hilo linafaa.. la maana ni sisi kupima reactions zetu na kukubali kuwa kuna wakati tuna overeact with very little facts na reactions zetu zinaongozwa na our own prejudices and biases to the point that we present them as authoritative. Inapohusu character ya mtu, we have to be measured. Tukubaliane kuwa reaction yetu kuhusu Mwakyembe was unfair, biased, and indeed unfounded. Na huo ndio uungwana.

Nadhani hata kichwa cha habari kibadilishwe, aidha kwa kuongeza alama ya kuuliza au kwa kukibadilisha kabisa ili kireflect upande wa pili wa hoja za Mwakyembe pia kuliko kilivyo sasa ambapo kinaonekana kuwa ni factual which is not.
 
tatizo haliko kwenye kuripoti habari, nadhani habari zinakuja sawasawa tu na hilo linafaa.. la maana ni sisi kupima reactions zetu na kukubali kuwa kuna wakati tuna overeact with very little facts na reactions zetu zinaongozwa na our own prejudices and biases to the point that we present them as authoritative. Inapohusu character ya mtu, we have to be measured. Tukubaliane kuwa reaction yetu kuhusu Mwakyembe was unfair, biased, and indeed unfounded. Na huo ndio uungwana.

Nadhani hata kichwa cha habari kibadilishwe, aidha kwa kuongeza alama ya kuuliza au kwa kukibadilisha kabisa ili kireflect upande wa pili wa hoja za Mwakyembe pia kuliko kilivyo sasa ambapo kinaonekana kuwa ni factual which is not.

Mwanakijiji,

Huwezi kukwepa hilo suala la mwanadamu kuwa biased. Faida ya JF ni kwamba
inajuimuisha biases kutoka kila angle na ambazo zina ji cancel (total sum inakuwa zero) na matokeo yake unapata a balanced discussion.

Kwenye hili la Mwakyembe nafikiri kama kuna makosa basi wa kulaumiwa ni hao DAWASCO na sio JF. Sisi tulikuwa tunachangia news na maoni yetu yanaenda na hiyo habari. Kama hiyo habari ni sahihi basi maoni yetu pia ni sahihi, kama hiyo habari ni uwongo basi maoni yetu yanakuwa irrelevant.

Vinginevyo sioni kitu cha kubadilisha hapa, muhimu ni kuendelea kumkoma nyani bila kumwangalia usoni.
 
Kwanini hatutaki kujihukumu wenyewe kwa makosa yetu na tunataka kuwalaumu wengine. Why are we so harsh on others but lenient on ourselves. We messed up big time and we have to own up to that. Huko ndiko kumkoma nyani giledi siyo nyani wa wengine tu hata wa kwetu.

I own up to my own mistakes. I over reacted and I'll try do do better next. Wengine muamue wenyewe lakini ukweli unabakia pale pale we overreacted without any basis.
 
Kwanini hatutaki kujihukumu wenyewe kwa makosa yetu na tunataka kuwalaumu wengine. Why are we so harsh on others but lenient on ourselves. We messed up big time and we have to own up to that. Huko ndiko kumkoma nyani giledi siyo nyani wa wengine tu hata wa kwetu.

I own up to my own mistakes. I over reacted and I'll try do do better next. Wengine muamue wenyewe lakini ukweli unabakia pale pale we overreacted without any basis.

Mwanakijiji,

Kwenye hili la DAWASCO sioni kabisa makosa ya JF, wala siwezi hata kuondoa
comments zangu.

Huwezi kujihukumu kwa comments ambazo umeitoa kwa kuamini habari inayojadiliwa ni kweli.

Kitu ninachoweza kufanya ni baada ya kuona kuna utata, kuacha kumlaumu mhusika kwa kosa analodhaniwa kulitenda.

Tungelikuwa tunajadili hili kwa kutumia sources ambazo sio wazi, hapo JF kweli ingeweza kusema tumekosea. Lakini sio kwa kujadili habari kama hii.

Hata Mwakyembe mwenyewe hawezi hata kuthubutu kuishitaki JF au gazeti maana
sisi wote tulikuwa tunajadili taarifa ambayo imetolewa kiwazi na chombo ambacho ni halali.
 
Mtanzania, nimekubaliana na msimamo wako wa kutokosea kwenye hili.

Binafsi naamini nilikosea kwa kutolea maoni ya ukali wa upande mmoja kwa sababu ya kushindwa kusubiri upande wa pili. Kwamba nilimhukumu Mwakyembe bila ya kumpa nafasi ya kujitetea ati kwa sababu nimeambiwa na chombo kimoja chenye maslahi katika sakata lenyewe. Binafsi sizungumzii makosa ya JF bali ya mwanachama mmoja mmoja aliyetolea maoni ya kuhukumu kwenye suala hili. Sijailaumu JF hata mahala pamoja bali nimeonesha ni jinsi gani tulikuwa na jazba ya kujiona tuko sawa na kusema pasipo subira maneno niliyoyaonesha kwenye nukuu.

Kama nyinyi mnaona mlikuwa sahihi kwa hukumu hizo binafsi dhamira yangu inanikataza kujihalalishia hilo.

Naamini kwa upande wangu haikuwa sahihi, lakini naelewa kwa upande wako ilikuwa sahihi. Tusonge mbele.
 
Ningependa kujua kama misamahama mnayoombana hapa pia inawafikia watu wote ambao wamehukumiwa hapa JF bila kusikia utetezi wao. Naanza na Chenge, na Billal. Na Mkono na Rashid Othman. Na Lowassa na Mkapa. Na Apson na Wahindi wa Railways.

Hawa hawahitaji kusikilizwa kama Mwakyembe?

Sijasema lolote kuhusu, na isieleweke kama nimemaanisha, mwenye hatia na asiye na hatia. Ni swali tu. Ahsante.
 
Back
Top Bottom