Mwenye kupinga 'kauli ya Pinda', huyo ni adui wa nchi.

Hivi jamani kumbe kuna baadhi ya watu wanafikiri kwa kutumia makalio eh? Kauli ya Pinda si ya kuungwa mkono kwa namna yoyote ile!

Ni kweli, kwa wapenda fujo na vurugu kama wewe ni lazima uwe na msimamo huo!
 
wewe ndio unajaribu kupotosha kauli ya Mh Pinda, yeye kwanza alisema wamechoka lakini nimeshangaa kwa nini hawajiuzulu kama wamechoka kuwalinda raia? alaf akasema atakaye kaidi apigwe tuu kwa kifupi Mh .Pinda ameruhusu askari kuuwa maana wakati wanatekeleza agizo la mh .Pinda ikatokea mtu akafa kwa kipigo ni wazo hawato laumiwa.

MH PINDA AMEWA RUHUSU POLISI KUUWA. PINDA NI KIONGOZI ALIYEKOSA BUSARA KULIKO WOTE NA KWA AGIZO LAKE YATATOKEA MAUJI MENGI MAANA POLISI WAMERUHUSIWA KUUWA KABISA KWA HIYO KAULI.
 
pind.jpg

mizengwe kajiharibia kabisa..
 
Lyagwa,

Umeandika mambo mengi sana tena ya msingi, ukweli ni kwamba nimesoma na nimeelewa mawazo yako kuhusiana na kauli ya Pinda.

Mawazo yako hayana tofauti na yale ya mhe Pinda, ila tu tatizo lilikuwa upotoshaji uliofanywa humu jukwaani, sumu imeshaenezwa humu na ni jukumu langu mimi na yeyote yule mpenda ukweli kuhakikisha sumu hiyo inaondolewa.

Mhe Pinda hakuwa ana halalisha mauaji kama wengi humu wanavyo lazima watu waamini. Mhe Pinda alikuwa akitoa baraka kwa jeshi la polisi liwadhibiti wale tu wakaidi wa maelekezo ya vyombo vya dola.

Kama wewe unaitambua na kuheshimu sheria, basi sheria hiyo hiyo ndiyo ina-regulate tabia ya mwanaadamu, na kama sisi wananchi tukiitii bila shuruti, sidhani kama kungekuwa na vipigo ama kitu chochote kwa polisi dhidi ya raia.

Ukiona hali ipo hivi, ujue tu kuna kundi la watu linataka kuharibu utawala wa rais Kikwete ili uonekane ni bure na hauna maana. Niamini mkuu, hii michezo ipo na ina ratibiwa na vyama vya siasa, lakini kwa bahati mbaya wanao humia ni raia na viongozi wa vyama hivyo wanabaki wanapeta tu!

RAIA, ADUI YETU SIO POLISI, SIO SERIKALI, BALI NI WANASIASA UCHWARA NDIO WENYE KUTUGOMBANISHA NA SERIKALI.

HAMY-D,

Nadhani hata kama unasema umesoma nilichokiandika vema, lakini nakuhakikishia ya kwamba hukunielewa vema, kama una muda rudi ukasome tena. Maneno aliyoyasema Pinda yako wazi wala hayahitaji utetezi wala ufafanuzi wowote ule. Binafsi nimeyasoma kwenye magazeti mbalimbali, nimemsikiliza katika redio tofauti tofauti, nimeyasoma katika social media tofauti tofauti, hivyo huwezi kunishawishi eti nikubaliane nawe kwamba kuna watu wamemuelewa vibaya ama kumunukuu vibaya.

Maneno aliyoyasema pinda ni ya kihuni kabisa, sio maneno ya kutamukwa na kiongozi wa ngazi ya juu ya kama waziri mkuu katika serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hakika hii inaendelea kumuanika waziri mkuu wetu halisi na matamko uchwara yake tena mbaya zaidi mbele ya Bunge. Kumbuka tamko juu ya mauwaji ya Albino ambalo mwisho wa siku lilikuja kumliza mwenyewe Bungeni, pia kumbuka pia tamko juu ya mgomo wa madakitari Liwalo na liwe, na athari zake ambako kesho yake aliyekuwa kiongozi wa madaktari Dr. Ulimboka atekwa na kuteswa na sasa ameamka na kuanza kuwahasisha polisi kuwapiga wananchi wa Tanzania, eti kisa tumechoka, kama amechoka anatoka ofisini (resign) kazi awapishe wengine, mbona hawachoki kukusanya kodi zetu na kujigawia miposho.

Naomba niendelee kupingana nawe juu ya thread yako ya kutaka kumtetea Pinda, kumbuka leo ni huyo mwananchi wa Mtwara, Arusha na kwingineko, labda huko kote huna ndugu, lakini amini usiamini ipo siku itakuwa zamu yako ama direct or indirect, jamani tuamke tuache upuuzi wa kutoa roho za watu kwa makusudi kwa kutumia amri uchwara kama kwamba nafsi zetu zimekufa.

Mwisho ngoja nikumbushe zamani, japo ndivyo ilivyo hadi sasa, na hii ni juu ya adhabu ya kinyongo hadi kufa, Mwl Nyerere katika moja ya speech zake aliwahi kusema, sheria inamtaja yeye Rais kusaini ili mtu anyongwe akisha hukumiwa toka mahakamani, yeye akajiuliza yaani mimi nikiweka sign yangu ananyongwa mtu, nafsi ikawa inamsumbua juu ya hilo, akamueleza Waziri wa mambo ya ndani ya nchi ili asini on-behalf, waziri akagoma, akamwambia sheria inakutaja wewe ndg Rais, utaona mtu ambaye nafsi yake i hai, sio kwamba yeye alikuwa anaenda kutenda kile kitendo, ra hasha, lakini sign tu.

Leo Pinda anatoa order za kijambazi kabisa, ambazo ziko totally against utawala wa sheria, ninyi mnakuja hapa kumtetea kwa nguvu, hata kama mmepewa pesa, ama mna hisa na uwaziri mkuu wake, kumbukeni roho za watu.

Utawala huu mnaojitahidi kuutetea, umekwisha shindwa kazi, kuweni wapole watanzania ni watu wapole, mnazidi kuwachefua na wataendelea kuwachukia hadi muondoke madarakani kwa aibu hata kabla ya wakati.
 
Last edited by a moderator:
Halafu wewe TAYADI ni mdini, sasa mambo ya maislamu na wakristo yamekujaje hapa?

Narudia tena!... Tunashangilia maumivu na mauti yetu wenyewe!... Ukiwa CCM ukashangilia kupigwa kwa CHADEMA usidhani wewe uko salama!...

Wakipigwa CHADEMA na kutoweshwa watakugeukia wewe unayejulikana mtandaoni!... Kipigo cha POLISI hakitachagua mkristo wala mwislamu. Wote ni kichapo tu!... Waliouawa Arusha ni wakristo na waislamu!...

Polisi pigeni tu!... Leo nipigeni mimi, kesho mpigeni HAMY-D!... Piga saaana mpaka akome!...
 
Kwa imani yangu kama ccm wataamua kutumia jeshi la polisi kuwakandamiza watanzania basi 2015 kutakuwa na mapinduzi ya aina yake,waache wananchi wachague kiongozi wanaemtaka na si kuwatishia kwa mabomu wakazi wa arusha wameonyesha hawaogopi matisho ya hii serikali...ukiubibiri amani ubiri pale ambapo hakuna maslain binafsi...nguvu ya uma siku zote hutawala
 
Ni lini Tanzania mtu kama Edward Moringe Sokoine??? Mtu atakayesimama na kusema jambo, jamii nzima ikakubali ns ardhi kutetemeka kwa kauli zake? Ni lini Tanzania itampata PM aliye mtu watu?
 
Wana-JF!

Ingawa kumekuwa na upotoshaji wa aina yake humu jamvini na kwengineko, kuhusu kauli ya mhe. Pinda, ila ukweli utabaki palepale kuwa mhe. Pinda ametoa kauli sahihi kwa wakati sahihi.

Kauli ya mhe. Pinda imepewa tafsiri ya uongo, kuwa imevunja katiba, hali iliyo pelekea wengi wenu kustaajabu kuwa ina kuwaje mwanasheria mkongwe kama mhe. Pinda kufanya hivyo, ila ukweli wa kauli yake mhe. Pinda ni huu hapa;

Mhe. Pinda alivyosema polisi wapige tu, hakuwa ana maanisha kuwa polisi wapige tu raia hovyo hovyo, lah hasha, bali alimaanisha polisi wadhibiti kwa maana ya kuwapiga raia wenye kukaidi maagizo ya dola.

Wote humu jamvini tunajua ni wajibu wa polisi kulinda raia na mali zao, lakini kwa vurugu za hivi karibuni, usalama wa raia umekuwa hatarini, kutokana na fujo za vyama vya siasa, kwa hali kama hiyo, serikali ni lazima ingetoa kauli, kauli yenyewe ndio hiyo ya mhe. Pinda.

Kauli ya mhe. Pinda imekuwa faraja kwa wapenda amani na utulivu wa hapa nchini, lakini imekuwa ni mwiba kwa wapenda fujo na maandamano yasiyo na tija yoyote kwa taifa.

Mhe. Pinda asante, TAIFA LIPO SALAMA SASA.

Tumekusikia msemaji wa serikali kwa ufafanuzi wako wa kauli ya Pinda!japo sishangai maana wahenga walisema "Akili ni nywele na kila mtu ana zake" inawezekana mwenzetu huna nywele!!
 
HAMY-D,


IKiwa unajuwa tabia ya wanasiasa ni kwamba huwa hawazitangazii kwa kuwahi nia zao za kugombea kiti kikuu. sababu kubwa ni kuepusha kujengeka kwa upinzani mkuu juu yao......

lakini kamanda wetu, wewe watetee tu ccm labda una maslahi yako huko, lakini historia inaonesha ccm tayari wametumia nguvu katika chaguzi zilizopita.

Matarajio katika 2015 watalazima kutumia nguvu zaidi na zaidi, si dhani kama watakuwa na watu wa kuwapigua kura za kutosha.
 
HAMY-D

ninashindwa kukuelewa mkuu, yaani wewe una bora kuair different opinion just for the sake of it

lakini kama kweli unamjuwa Mhe Pinda basi nitakupa mfano mmoja tu halafu utajaza mwenyewe

unakumbuka siku zile alipokwenda bungeni akasema znz sio nchi? wakatokzea wapambe kwa mfano kama wako wakaanza kufasiri kaneno yake, si unakumbuka alifanya nini? alirejea tena maneno yake na akasema hakukosea kitu na alichokusudia kusema ni kuwa znz sio nchi

na kauli hii ninahakika makusidio yake ni kusema polisi wapige tu.............sasa its up to police kuchaguwa baina ya kupiga risasi, mabomu ya machozi, bakora au maji ya mwasho yatiayo cancer
 
Back
Top Bottom